Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. JUMANNE A. SAGINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda wa dakika tano, naomba nijielekeze moja kwa moja kwenye kuchangia. Mpango ulioandaliwa na Serikali kwa ujumla wake ni mzuri hasa huu wa miaka mitano. Kwanza niwapongeze Wizara ya Fedha kwa namna walivyochambua zile changamoto, maana yake wameainisha ni vitu gani vilisababisha Mipango miwili iliyopita na hususan Mpango wa Pili kushindwa kutekelezeka kikamilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ninayoiona tu ni ile mikakati inayowekwa ya kushughulikia hizo changamoto ili mpango wa III uweze kutekelezwa kwa ufanisi. Ushauri kwenye eneo hilo waichambue vizuri ile mikakati ya utekelezaji katika ku-deal na zile changamoto kwa kuwa kuainisha nani anafanya nini, wakati gani, kinahitaji rasilimali kiasi gani ili changamoto kama hizo zisije zikajitokeza kwenye utekelezaji wa Mpango wa Tatu, kinyume chake tunaweza tukaingiza statement tutafanya hivi ukajikuta hizo statement hazijachambuliwa vizuri, changamoto hizo zikaendelea kuathiri utekelezaji wa Mpango unaofuata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuzungumza ni juu ya ile mikakati ya utekelezaji wa Mpango. Changamoto kubwa ninayoiona hapa ni kuainisha Mipango ya Wizara, Idara Zinazojitegemea, Taasisi na Serikali za Mitaa, Mikoa na kadhalika. Serikali ni pana kweli, ukizungumza kwa ujumla tu kuainisha mipango ya MDAs na Mpango Mkuu wa Serikali, kumbukumbu zangu wakati niko Serikalini kuna tendency ya ku-cut na paste, mtu atakwambia Mpango huu umezingatia MKUKUTA, Vision 2020 – 2025, sijui SP ya Wizara, lakini ukienda kuangalia mambo yaliyozungumzwa huoni moja kwa moja kama yana-linkage zozote na hiyo mikakati mikubwa ya kitaifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ushauri wangu kwamba Wizara ya yenye dhamana na fedha ifanye kama ilivyowahi kufanya huko nyuma, kutaka hizi MDAs zichambue unaposema umezingatia MKUKUTA, Vision 2020 – 2025, Mpango wa Miaka Mitano, awamu ya tatu, aoneshe kindakindaki nini kiko wapi na eneo gani. Kwa kufanya hivyo Mpango unaweza ukajikuta unatekelezwa, lakini vinginevyo inaweza kuwa ni wishful statements ambazo utekelezaji wake unaweza kuwa na changamoto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa takwimu; imetajwa kama ilikuwa changamoto. Ningetamani waainishe sababu zilizosababisha kuwe na changamoto ya upatikanaji wa hizi takwimu na sasa tumejipangaje hizi takwimu ziweze kupatikana hasa kutoka kwenye private sector. Kama pamekuwa na changamoto na hatujaijua itakuwa ngumu awamu ijayo pia kuzipata hizo takwimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye muundo wa utekelezaji ambapo Wizara, Tawala za Mikoa na Halmashauri na private sector zinaingizwa, tuonyeshe details kama nilivyosema mwanzo kwani wakati mwingine unaweza kukuta hakuna link kati ya vinavyotokea kwenye Serikali za Mitaa na hivi vinavyokuja kuzungumzwa ngazi ya Serikali Kuu. Ili mpango uwe jumuishi ni vizuri hizo linkage zionekane bayana, badala ya kuwa na jedwali tunaloonesha local government lakini huioni vizuri kama ina match na yale matakwa ya kisekta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Sekta ya Kilimo, nataka nishauri jambo; kwenye vijiji, kwenye kata ndiko shughuli za kilimo zinakofanyika, lakini Maafisa Ugani, wataalam wa kilimo kule ni wachache sana. Kuna kata moja Mheshimiwa mmoja alizungumza hapa ina barabara ya umbali zaidi ya kilomita 250, kata moja ina vijiji 16, hivi kweli kama una Afisa Ugani mmoja anawezaje kuwa effective kutekeleza shughuli za ugani kwenye kata kubwa kama hii? Ni ushauri wetu kweli kama tunataka kilimo kilete tija tuwe na vijana wanaojua eneo lao la kilimo, lakini tuwapeleke kule kilimo kinakotekelezwa hasa vijijini vinginevyo tutakuwa bado tuna changamoto tukidhani tutaongeza tija kwenye kilimo, lakini kisifanye hivyo kwa sababu ya uhaba wa wataalam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ugharamiaji wa Mpango, nadhani wadau wanaotajwa na Serikali ni wengi sana, lakini utaona kuna future tutafanya hivi, litatokea hivi, nilidhani kwa vile Mpango unaanza 2021/2022 mpaka 2025/ 2026 hizi engagement zote zimeshafika, vinginevyo itafika Julai tutatumia muda mrefu sana ku-engage hawa wadau wote, halafu utekelezaji sijui utakuja kuanza lini. Kwa vile kuna dalili za kuchelewa, ni ushauri kwamba sasa Serikali ifanye haraka ku-engage na hizi Taasisi za Serikali, Taasisi Zisizo za Kiserikali, Wadau wa Maendeleo na kadhalika na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kwenye kuianisha mifumo ya Serikali na ya sekta binafsi; unajua kwenye Serikali kuna urasimu, kuna junior officer anaandaa dokezo senior officer analipokea, Mkurugenzi Msaidizi anaweka comments, Mkurugenzi halafu liende kwa Katibu Mkuu, wakati mwingine inaweza ikachukua hata mwezi kufikia uamuzi, lakini kwenye sekta binafsi vitu vinaenda haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni maoni yangu kwamba pengine katika usimamizi wa Mpango huu kuwe na mfumo wa tofauti, tukifuata huu mfumo wa Serikali wa madokezo kupita kwa watu saba kabla ya uamuzi, tunaweza tukajikuta tumechelewa kutekeleza Mpango wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante, kengele imeshagonga.

MHE. JUMANNE A. SAGINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)