Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. BONIFACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Kwa mara ya kwanza nasimama katika Bunge lako Tukufu, naomba nimpongeze Mheshimiwa Spika na wewe Naibu Spika kwa kuchaguliwa kuwa viongozi wetu katika Bunge hili Tukufu. Pia nitumie fursa hii kukishukuru Chama changu Chama Cha Mapinduzi kwa kuniteua na kupeperusha bendera ya Chama changu Cha Mapinduzi na hatimaye kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Kishapu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kuwashukuru pia wananchi wa Jimbo la Kishapu kwa namna ambavyo wamenipa kura nyingi za kishindo kwa asilimia 87.4. Vile vile niwashukuru sana Wanakishapu kwa ujumla, lakini niishukuru familia yangu, kwa namna ya pekee nimshukuru mke wangu, lakini niishukuru na familia yangu kwa ujumla kwa namna ambavyo wamenipa ushirikiano kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunapata kura za ushindi na hatimaye kufika katika Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe mchango katika Mpango huu wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka mmoja na miaka mitano. Kwanza nianze kwa kuishukuru sana Serikali yangu kwa jitihada kubwa ambayo imekuwa ikifanya. Sote tuna macho ya kawaida na hatuna macho yenye miwani ya mbao, kwa sababu yako mambo mengi ambayo dhahiri na wazi yamekuwa yakionekana ni mafanikio makubwa kwa Serikali yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sekta ya Elimu; sote tunafahamu elimu ya sekondari kwamba sasa hivi tuna sekondari katika kila kata na baadhi ya kata zingine tumeanza kuongeza sekondari. Pia shule zetu za msingi zimeboreshwa, ukilinganisha na hali halisi ya kipindi cha nyuma. Yapo mambo mengi vile vile kama vile ujenzi wa Standard Gauge, ambao sasa hivi unaendelea kwa kasi kubwa; uboreshaji wa huduma ya Shirika la Ndege. Shirika hili lilikuwa limekufa na sasa hivi maendeleo ni makubwa, sote tunanufaika na huduma hii ya usafiri wa anga; kuna mradi huu mkubwa wa ufuaji wa umeme wa Mwalimu Nyerere, ni hatua kubwa ambayo Serikali yetu imewekeza na kufanya mradi huu unakwenda vizuri; na suala zima la uanzishwaji wa viwanda vikubwa, viwanda vya kati na viwanda vidogo. Hii ni hatua kubwa ambayo ni dalili tosha kwamba hatua ya kimaendeleo katika nchi yetu tunakwenda vizuri..

Mheshimiwa Mwenyekiti, haitoshi kwa sababu sisi siyo wananchi isipokuwa ni taasisi za kifedha za kimataifa ndizo zilizofikia hatua ya kuiona Tanzania inastahili kuingia katika uchumi wa kati. Kwa hiyo tupo assessed kwa utaratibu wa kitaaluma kabisa kabisa na ndiyo maana tumefika mahali tumeingia katika uchumi wa kati.

Kwa hiyo ni jukumu letu Watanzania kuweka mbele uzalendo ili mradi tuhakikishe uchumi wa kati lakini katika kipato cha juu, sisi wenyewe Watanzania kama wazalendo tuhakikishe kwamba tunapambana na tunakuwa wamoja kuhakikisha kwamba maendeleo ya uchumi wetu yanapaa inavyotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie tu mafanikio haya yanaonekana kwenye Jimbo langu la Kishapu, huwezi ukaamini kwa miaka nane ya nyuma na huko nyuma zaidi coverage ya maji ilikuwa chini ya 20%, lakini leo tunavyozungumza nina Mradi mkubwa wa Maji ya Ziwa Victoria ambao kwasasa hivi coverage ya maji pale iko kwenye asilimia 50. Miradi inayotekelezwa baada ya miezi kama minane nina uhakika nitaweza kufikia coverage ya 70%. Hii ni hatua kubwa sana,

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna barabara zinazojengwa kwa kasi kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuzungumza haya nataka niseme kwamba, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)