Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kusema kidogo kuhusu huu Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Nchi yetu. Nimepitia makabrasha yote ya Mpango huu na hotuba mbili za Mheshimiwa Rais, ya 2015 pamoja na hii ya mwaka 2020 ambayo tulisomewa tarehe 13 Novemba hapa wakati wa kuzindua Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uhakika kabisa Mpango huu wa Tatu nina hakika utafanikiwa na unakwenda kutuinua kwa viwango vya juu zaidi na kuboresha maisha ya mwananchi wetu. Hii inatokana na kwamba Mpango wa Pili wa Maendeleo pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ambao ulisimamiwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, umefanikiwa sana kwa hali ya juu. Kwa mafanikio yale nina hakika kabisa kwamba Mpango huu unakwenda kuinua maisha yetu na utaboresha maisha ya Watanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nita- comment kwenye maeneo mawili; miundombinu; tulishuhudia barabara zikijengwa, madaraja yakijengwa, lakini barabara zetu zikishamalizika kujengwa, kule zinakopita unakuta ukihama barabarani mita mbili tairi linazama. Kwa hiyo niruhusu nilishauri Bunge hili na Serikali yetu kwamba kuanzia sasa tutakwenda kujenga barabara nyingi sana ambapo tumelenga kujenga barabara kilomita 6,600 ifikapo mwaka 2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye miradi hiyo kila barabara itakayojengwa tufanye extension kwenye vijiji na kata ambazo zitakuwa zimepakana na zile na barabara kwa kiwango cha kilomita tano kila kijiji kiweze kufaidi. Hali hiyo niliweza kuiona kwenye nchi fulani nilikwenda kutembelea, nikaona kwamba ilifungua sana maisha ya wananchi ambao wako kwenye vijiji ambavyo vimepakana na zile barabara. Nikaona hilo jambo ni zuri na niishauri Wizara ya Ujenzi iliweke kwenye sera zetu ili barabara zote zitakazojengwa kuanzia sasa zifanye extension, zifanye matawi kwenda kwenye vijiji na tunaamini kwamba itafungua maisha na maendeleo ya wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wakati wa kampeni Mheshimiwa Rais alitoa ahadi nyingi sana, nishauri kipaumbele kipelekwe kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais. Hii itaondoa minong’ono ambayo nimekuwa naisikia mara kwa mara kwamba ooh ahadi za kisiasa tu, ahadi za kutafuta kura na kadhalika, lakini zile ahadi alizitoa mbele ya wananchi wengi kwa hiyo nashauri kwamba zipewe kipaumbele kwenye huo Mpango wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka pia niseme kitu kwenye kilimo. Tangu nasoma kulikuwa kuna kitengo cha umwagiliaji kule Wizara ya Kilimo, lakini mpaka leo bado hatujaweka nguvu kubwa kwenye umwagiliaji…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Shukurani sana kengele imegonga Mheshimiwa.

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru san ana naunga mkono hoja.