Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii, lakini kabla ya yote nimshukuru sana Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kunipa afya hii njema hadi leo niko Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili niwashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Kiteto kwa imani kubwa na wamenichagua kwa kura nyingi sana. Nawaahidi kabisa kwamba nitawajengea heshima kubwa hapa Bungeni haijawahi kutokea. Vilevile nikishukuru Chama changu Cha Mapinduzi kwa kuniteua na nikapeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijielekeze kutoa maoni yangu kwa Mpango huu wa Maendeleo. Mpango wa Maendeleo ni mzuri sana na kwa kweli katika kupitia zipo taarifa kama tatu hivi ambazo ni kubwa kweli. Kwa hiyo, maoni yangu ya kwanza nafikiri kama hatutayatendea haki sana mapendekezo haya kwa siku zilizopangwa kama nne hivi. Document ya kwanza ina kurasa karibu 164; ya pili 51; nyingine 107. Sasa ukichanganya zote na dakika tano hizi utajua kabisa kwamba pengine tungehitaji wiki mbili hivi za namna ya kuzungumza ili tuweze kuishauri Serikali vizuri sana katika mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na muda kuwa mchache, nijielekeze kwenye kilimo. Kilimo hapa tumeambiwa kwamba pato la Taifa ni 27% na kinawaajiri Watanzania zaidi ya 65%. Nimshukuru sana Rais kwamba mapendekezo ya maendeleo mwaka huu ni kuwekeza nguvu kwenye kilimo. Tukiwekeza nguvu kwenye kilimo na hususan mbegu zipatikane kwa wakati na kuwaondoa wakulima kwenye jembe la mkono na ku-mechanize, tutaweza kulikwamua Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mahusiano katika kuendeleza kilimo siyo tu yana tija kwenye uchumi, lakini vilevile na mahusiano makubwa sana ya kupunguza umaskini kwa Watanzania walio wengi. Kwa hivyo kwa kweli naomba Wizara ya Kilimo isilale katika hii miaka mitano, tuwekeze nguvu kubwa sana kwenye kilimo na kwenye mbegu, unajua nchi zile zilizoendelea sasa wana-patent hizi mbegu, kwa hiyo tusiwekeze tu kwenye kufanya utafiti, lakini pia tu-patent mbegu zetu ili tuweze kulinda masoko yetu huko mbele ya safari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwekeza kwenye kilimo, kwenye mifugo, kwenye uvuvi na tukaweka nguvu zetu zote huko tutakuwa tumeshughulika na vitu wanavyoita watu wengine the really economies kwa sababu ndiyo Watanzania wengi wako huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni umeme na ningemwomba sana Waziri wa Nishati anisikilize vizuri hapa, Hotuba ya Mheshimiwa Rais ukurasa wa nane na nimeshamwandikia Mheshimiwa Waziri memo nyingi sana kuhusu suala la umeme. Nafurahi sana tumewekeza kwenye umeme na nawapongeza sana na Wizara wakati wanajibu maswali hapa walisema hivi, kwamba wamejiwekea miezi 18 kumaliza tatizo la umeme kwa vijiji vyote vilivyobaki. Hii ni ishara nzuri sana, lakini ni lazima sasa tuangalie umeme tulionao, Mheshimiwa Rais alisema hivi na naomba ninukuu, ukurasa wa nane wa hotuba ya 2015; “Mheshimiwa Spika eneo lingine ni TANESCO, TANESCO pamekuwa ni suala la kukatikakatika kwa umeme mara kwa mara na kuwepo na umeme wa mgao na hilo limelalamikiwa sana na wananchi wetu.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiteto kwa miezi mitatu sasa umeme ni kukatikakatika halafu hatupati taarifa yoyote ile. Sasa wakati tunawekeza huko kutengeneza umeme, lazima sasa tuwe na uhakika wa umeme tulionao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda naunga mkono hoja lakini…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante kengele imeshalia

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA: Ahsante sana.