Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana. Nami nichukue fursa hii kumshukuru sana Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema. Pia nikishukuru chama changu, niwashukuru pia wananchi wa Jimbo la Singida Mjini kuniamini tena kwa mara nyingine ya pili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nijikite ukurasa wa 25 eneo ambalo linazungumzia kukuza ujuzi. Kulikuwa na Tume imefanya utafiti iliyokuwa inaitwa Tume ya Mipango mwaka 2014 ilifanya utafiti wa kuangalia hali ya soko la ajira nchini, lakini matokeo ya utafiti ule umeonesha iko tofauti kubwa ya uhitaji wa ujuzi kwenye soko lakini na ujuzi unaotolewa katika vyuo vyetu vya elimu ya ufundi. Wameenda mbali zaidi wakaamua kufanya reference kwenye nchi za wenzetu za China, India, South Africa na nyingine, lakini huko wamekwenda mbali sana walipaswa watueleze tulikwama wapi kabla ya kwenda kufanya reference. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nieleze hapa, tulikuwa na vyuo vya kati (FDCs) ambavyo leo tumezi-transform kuwa university. Mtu anapopata degree unamuandaa kuwa manager, kuwa administrator, lakini hawezi kuwa mtu mwenye ujuzi ambaye anahitaji kusimamiwa, sasa tumehama kwenye eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nishauri hapa na nitoe mfano. Naibu Waziri kule China, wenyewe wanaita Vice Minister, anaitwa Lu Xin, mwaka 2014 aliamua kwa dhati kuridisha universities 600 kuwa polytechnic. Sisi leo tunatoa hivi vyuo vya kati tumevipeleka kuwa university, kitu ambacho sio sawa lakini hatujachelewa. Nataka niombe Mpango huu sasa uamue vile vyuo vilivyokuwa vya kati vimekuwa university virudi kuwa vyuo vya kati, tutakuwa tume-solve tatizo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Korea Kusini alikuwepo Rais anaitwa Park Chung-hee amefariki mwaka 1979 alikuja na mpango maalum, mpango huu aliamua wawekeze kwenye chuma. Korea Kusini population yake inafanana na sisi lakini ardhi yake asilimia 70 ni milima, asilimia 30 tu ndio wanayoitumia kwa makazi, lakini hawana resource yoyote, resource tulizonazo sisi hata hizo Asian countries hazina, sisi tunazo za kutosha sana; wakaamua kuwekeza kwenye chuma na chuma hiki wana-import. Sisi tuna Mchuchuma na Liganga kwenye Mpango hauelezwi, hatuweki mkakati wa Mchuchuma na Liganga tunategemea kufanya mapinduzi gani ya viwanda? Tunategemea kufanya mapinduzi gani ya kilimo kama hatuwekezi kwenye chuma na chuma tunacho, wala hatuhitaji ku-import chuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niiombe Serikali kwa nia njema kabisa, huu ndio wakati sahihi wa kutumia Serikali zetu kwa sababu uwekezaji mkubwa umefanyika na tunatumia vitu vya nje wakati sisi tunavyo ndani. Naomba tufanye mabadiliko kwenye eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nishauri eneo moja dogo sana; leo kilimo chetu hiki wanaotuwezesha ni wakulima wadogowadogo na wanaofaidika na kilimo hiki ni makampuni makubwa. Lazima tutengeneze ukuaji wa dhana ya pamoja, shared growth principle na lazima tuwe na authority tutengeneze mamlaka ambayo itasimamia ukuaji wa dhana ya pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumaanisha nini? Makampuni makubwa ni lazima tuwe na mamlaka ya kuya- control kuyalazimisha yafanye biashara na makampuni madogo. Natoa mfano mdogo, leo nenda Lushoto, Muheza kote kule, matunda yanazagaa lakini Azam yule anaweza kuyanunua yale matunda yote na tukainua kile kilimo cha watu wetu wa chini. Nenda Singida kule leo alizeti inazagaa, lazima aje mchuuzi ndiyo aweze kuuza alizeti, tunawezaje ku-promote hii peasant economy? Hapa ndipo tunafanya wakulima wetu wanafeli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba sana Serikali, umefika wakati wa kuanzisha mamlaka itakayosimamia mikataba ya makampuni makubwa na kwa ajili ya makampuni madogo ili kuweza kufanya biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)