Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami ni mmoja kati ya Wajumbe wa Kamati ya Bajeti. Nimepata nafasi nzuri sana ya kuupitia Mpango huu. Nimeuona, tumeujadili, nasema ni Mpango mzuri ambao Serikali imekuja nao, lakini naiomba Serikali iweke room for improvement. Haya maoni ambayo yanatolewa yote ni maoni mazuri, wayachukue, isiwe kama ni taratibu zile nyingine kwamba tunazungumza lakini bado wanakuja na Mpango ule ule, mapendekezo yale yale, hilo haitakuwa jambo jema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najikita zaidi katika private sector. Ningependa sana huu Mpango uje waziwazi kwenye private sector, tuwe na vibrant private sector, hakuna uchumi unaoweza ukaendelea bila ya kuwa na private sector ambayo ina nguvu, inayochochea exports, lakini vile vile inachochea domestic spending, bila mambo haya tutakuwa tunajidanganya. Tutakuwa tunazungumza lakini tunajifanya kama tunasahau kama private sector ni mbia mkubwa sana wa maendeleo katika nchi yetu. Tumeangalia na figure zimetolewa na Wizara. Tuchukue tu mfano wa ule Mpango ambao umemalizika 2021. Contribution ya private sector ilikuwa inatarajiwa trilioni 48 karibu asilimia 45 ya kile kinachotarajiwa. Huyu si mtu wa kawaida. Huyu ni mbia ambaye lazima tuhakikishe tunakuwa nae na tunamuamini, private sector lazima iaminiwe. Tusitengeneze private sector ambayo hatma yake tunapeleka wrong waives, wrong information or wrong message kwa investors nje kwamba kufanya kazi au biashara Tanzania ni jambo gumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni wazi, hebu angalia hawa wataalam wa World Bank, kuna huyu mtaalam anaitwa Simeon Diankov na Gerald Paul, Wachumi wa World Bank hawa walivyotengeneza ile ease of doing business index, Tanzania katika kuangaliwa, tuko watu wa 141, tumewekwa kama medium. Sasa jamani tunashindwa, Rwanda is very easy to do business, Rwanda jamani? Kitu gani kinatufanya Rwanda wao iwe ni easy to do business, sisi iwe ni medium, basi hata Zambia? Zambia nao wanafanya vizuri, wako easy, Kenya wako easy, sisi tunafunga wapi kiasi kwamba kwetu sisi ionekane tuko katikati, tunachotafuta ni nini? Tunatafuta industry ya private iwe inapewa nafasi zake. Sasa hivi iko suffocated, it is a fact, nimepata bahati ya kufanya kazi Serikalini, nimefanya kazi katika Private Sector, sasa hivi na mimi eti nami ni mwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sikiliza, kampuni moja inazungukwa na regulators si chini ya sita au saba. Huyu anamuuliza hiki, yule anamuuliza hiki, yule anamuuliza hiki. Hajui aende wapi, who is the core regulator, aende wapi. Akipata matatizo, akiwa aggrieved huyu mtu anapata shida kubwa sana. Kampuni zinapata shida kubwa sana na haya ambayo yalikuwa yakizungumzwa kwamba business zinafungwa, naomba Serikali iangalie. Haiwezekani kampuni moja itaangaliwa na TRA, BOT, TCRA, OSHA, Fair Competition and Filling Company, hiyo ni mfano wa kwenye betting, huko usifikiri kuna Gaming Board of Tanzania peke yake, hawa ninaowatajia wako nyuma kila siku wanagonga milango. How can you do business?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunachohitaji ni kuona kwamba mtu ambaye anafanya business Tanzania asababishe mwingine aliye nje avutike kuja Tanzania. Kwa kufanya hivyo tutapata kodi nyingi, tutaajiri watu wengi, lakini vile vile tutaondoa manung’uniko. Leo hii mtu akiwa aggrieved anakwenda wapi? Kwa nini tusiwe na regulatory ombudsman? Wafanyabiashara hawataki kwenda Mahakamani kushindana na Serikali. Katika vitu ambavyo wafanyabiashara hataki ni ugomvi na Serikali, lakini angekuwepo mtu hapo kama vile wa tax ombudsman hata regulatory ombudsman amekuwa aggrieved na chombo fulani cha Serikali huyu bwana anakwenda kwa ombudsman, anakwenda pale anazungumza mambo yake yanawekwa sawa, mambo yanaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tutaendelea na utaratibu tulionao sasa hivi, tuna suffocate private sector na private sector kama nilivyosema awali ni eneo moja ambalo ni mbia mkubwa sana wa biashara, mbia mkubwa wa maendeleo na ni maeneo ambayo tunahitaji kuyaangalia kwa nguvu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. Mungu atubariki. (Makofi)