Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami kwa niaba ya wananchi wangu wa Jimbo la Pangawe, nipo hapa kwa ajili ya kuchangia Mpango wa Taifa wa mwaka 2020/2021 pamoja na Mipango yote miwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nami sina budi kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwasilisha Mpango huu ambao ulikuja na theme ya uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya watu. Sasa mpango huu kwa kweli nauunga mkono na kwa kweli nasema kwamba jitihada kubwa zimefanyika katika Serikali hii ya Muungano na mambo mengi ambayo nimeyaona katika Mpango uliopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika uchumi wowote ule wa dunia kitu kikubwa ambacho unaangalia ni suala la amani. Amani yetu tuliyokuwa nayo katika nchi yetu ya Tanzania inatosheleza kuweza kufanya uchumi wa aina yoyote. Bahati nzuri katika nchi yetu ya Tanzania, kwa mujibu wa jinsi tulivyo katika maumbile yetu, maana yake tuna uwezo wa kufanya kitu chochote. Tukija katika suala la elimu, tuna uwezo wa kuwasomesha vijana wetu na kuweza kufikia katika hatua kubwa sana ya kimaendeleo katika nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu nilichokuja nacho kwa pamoja katika ushirikishwaji wa nchi mbili kwa pamoja ni suala la utalii. Bahati nzuri nchi yetu ya Tanzania ikiwemo Tanzania Bara pamoja na Visiwani ina kitu ambacho ni cha kimaumbile ambacho tukija katika suala la kiutalii, tuna uwezo wa kuziunganisha nchi hizi mbili zote tukasema kwamba tuwe na utalii wa pamoja ambao ni kwa maendeleo ya nchi zote mbili. Kwa sababu kwa maumbile ya nchi yetu, kwa upande wa Bara tuna mbuga ambazo tunaweza tukazitangaza kwa pamoja na zikaleta matunda kwa ajili ya maendeleo ya watu wote. Kwa upande wa visiwani kule, tuna utalii unaotokana na fukwe pamoja na bahari tuliyokua nayo, tukizishirikisha nchi hizi, maana yake kwa Tanzania tutaleta uchumi ambao ni endelevu na mkubwa sana. Vilevile kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeunga mkono ile azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika ule uchumi wa bluu ambapo ndiyo theme ambayo kwa sasa hivi inazungumzwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwamba kuna vitu vitakuwa vinaonekana kwamba siyo shirikishi, lakini kimaumbile yake na kwa mujibu wa nchi yetu ilivyo, hivi ni vitu ambavyo ni shirikishi. Kama tutaweza kuunganisha utalii wa Tanzania ukawa ni utalii tunaoutangaza kwa pamoja, nadhani tunaweza tukafanya kitu ambacho ni kikubwa sana kwa mujibu wa maumbile ya nchi yetu ambayo tunayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa rai katika Mpango huu, pamoja na kwamba yamezungumzwa mengi; kulizungumzwa suala la utalii hasa kwa upande wa vivutio vya mbuga, ila mimi napenda zaidi tukauzungumzia katika utalii wa fukwe, tukaipa nguvu na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa kuichanganya ili tuwe na utalii wa pamoja. Pato litakaloweza kupatikana maana yake litaweza kuleta tija kwa nchi zetu zote mbili. Hii itaweza kufanikisha ule umoja wetu ambao tumekuwa nao katika nchi zetu kuweza kuwa shirikishi hasa katika maendeleo ya pamoja. Tanzania ni moja, watu wa Tanzania ni wamoja. Hiki siyo kitu cha ubishi. Maendeleo yoyote yale ambayo yataweza kufanyika kwa upande wa Bara, ikiwa ni kilimo maana yake faida itakuwa ni ya kwetu sote (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naunga mkono Mpango wa Maendeleo, ahsante sana. (Makofi)