Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, naomba niungane na Watanzania wenzangu kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu mpendwa, Dkt. John Pombe Magufuli. Mheshimiwa Rais amefanya kazi nyingi kubwa na wataalam wa Kiswahili wanasema mwenye macho haambiwi tizama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi hizi zinatoka ndani ya nchi na nje ya nchi. Ukiwa nje ya nchi unaposema tu unatoka Tanzania kwanza lazima upokee salama na pongezi za Mheshimiwa Rais. Utaambiwa tunampenda sana Mzee Magufuli, anafanya kazi na amekuwa ni mfano ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Afrika na duniani kote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niwashukuru wananchi wa Njombe kwa ridhaa yao ya kunirudisha tena mjengoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kwa moja niende kwenye suala nzima la kilimo. Mikoa ya Kusini kwa asilimia kubwa sana wamejikita kwenye masuala ya kilimo na Mkoa wa Njombe kuna kilimo cha mazao mengi kama viazi, mbao zinakwenda mpaka nje nchi ndani ya Jumuiya ya Africa Mashariki ambapo kuna masoko mengi sana lakini pia kuna suala nzima la mahindi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze sana Serikali ya Awamu ya Tano eneo la mahindi na pembejeo wamefanya kazi nzuri lakini tuendelee kuangalia bei za mbolea ni namna gani tutaweza kufanya ili mbolea iendelee kuzalishwa nchini ili bei ipungue. Sasa hivi mfuko mmoja kwa mbolea ya kukuzia ni Sh.50,000 hadi tumalize kilimo, mkulima anakuwa amewekezq sana. Kwa hiyo, eneo la pembejeo za kilimo hususani zao la mahindi, naomba tuendelee kuliboresha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo, nipongeze kwa masoko ambayo yako na masoko mengi sasa hivi ni soko huria lakini kwa kweli tunahitaji kuona intervention, ni namna gani tunahakikisha wananchi wakishalima zao hili la mahindi wanapataje masoko ya uhakika. Nilete salama kutoka Mkoa wa Njombe, nadhani Waziri wa Kilimo ananisikia, yupo hapa jirani yangu wanaomba mahindi yakanunuliwe. Kuna mahindi mengi sana, ili yasiweze kupotea kutokana na upotevu unaotokea mara baada ya kilimo na kwenye hotuba imesekana wakati mwingine 40% ya mahindi wakati mwingine yanapotea (postharvest) basi tuone namna ya kuyanunua mahindi haya. Kuna mahindi mengi wanaomba SGR, NFRA ikiwezekana wakayanunue na wawaunganishe wakulima wa Mikoa hii ya Kusini na maeneo mbalimbali kama World Food Program, FAO, tuna kambi nyingi za wakimbizi wanahitaji chakula cha kutosha tuone namna gani ya kuunganisha eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine naanza na pongezi ni suala nzima la elimu. Sasa hivi uandikishwaji wa watoto umetoka asilimia 93 mwaka 2015 sasa hivi tuko takribani asilimia 110. Tunapoelimisha vijana wengi maana yake wanakuwa na ubunifu, wanaweza wakabuni bidhaa na huduma mbalimbali na kuzalisha. Kwa hiyo, eneo hili ni muhimu lakini sasa tuangalie na vyuo vya maendeleo, kuna maeneo ambayo tuna miradi ya mkakati (flagship projects) tunahitaji vyuo vya maendeleo ambavyo vitasaidia ku-boost miradi ile. Kwa mfano, maeneo ya Miradi ya Mchuchuma na Liganga, Mwalimu Nyerere Hydroelectric Power, tuhakikishe tunavyo vyuo vya kutosha ili kuimarisha vijana ili waweze kupata ajira na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Ludewa mpaka sasa hawana chuo cha VETA. Nitumie nafasi hii kwenye mpango huu tuone namna gani tunaweza tukatumia force account ili waweze kuweka VETA pale ambayo ita-boost Miradi ya Mchuchuma na Liganga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nipongeze sana Mradi wa Mchuchuma na Liganga upo kwenye Ilani na pia umeelezwa vizuri sana kwenye Mpango. Pamoja na hiyo, tuangalie suala zima la fidia kwa wananchi kama tumeshalikamilisha siyo tu katika Mradi huu wa Mchuchuma na Liganga lakini na miradi mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika maeneo ya madini kuna suala la wachimbaji wadogo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)