Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nami nitoe shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais kwa kunipa fursa hii na kwa wananchi wangu kwa kunirejesha tena Bungeni tena kwa kura za kishindo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ajili ya muda, sitaenda kwa kina kati ya yale ambayo nilikuwa nimekusudia kuyasema kufuatana na mpango wa Wizara, lakini pia kufuatana na hoja zilizotolewa na Wabunge. Nitafanya hivyo wakati nitakapokuwa nachangia kwenye mpango tutakapojadili baada ya ajenda hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa leo niwaambie tu Waheshimiwa Wabunge, kama mnataka mali mtaipata shambani. Naawaambia Waheshimiwa, vijana wenzangu, wahitimu wa Vyuo pamoja na Watanzania kwa ujumla kama mnataka mali mtaipata shambani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miaka kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kutoka vijijini kwenda mijini. Leo niwaambie, ni wakati wa vijana kutoka mijini kwenda vijijini. Huko ndiko utajiri uliko na huko ndiko mali iliko. Mashambani kuna ufugaji, kuna uvuvi na kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu katika miaka mitano ya Rais aliyepewa dhamana na Watanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kitakuwa ni kipindi cha kuweka mabadiliko katika sekta nzima ya kilimo na kuipa hadhi inayostahili ambayo kila wakati tumekuwa tukisema ndiyo uti wa mgongo na ndiyo inayotoa ajira kwa asilimia kubwa kwa Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wameongelea matatizo mengi. Moja, wameongelea upande wa wafugaji. Nitaenda kwa undani, lakini tunalopanga kama Wizara, tunapanga ni kuondoa utaratibu wa wafugaji kuzunguka na mifugo na hivyo kuleta ugomvi kati ya wafugaji na wakulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, namna ambavyo tunapanga kwenda kulifanya jambo hili, tunataka kufanya kama ambavyo katika Taifa kuna Ranchi zilizobainishwa miaka na miaka, kuna hifadhi ya mapori yaliyobainishwa miaka na miaka, tunakwenda kubainisha na maeneo ya wafugaji katika maeneo hayo tutakwenda kuweka miundombinu inayostahili ya mahitaji ya huduma za mifugo ili kuondoa tatizo la wafugaji kuzunguka zunguka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye jambo hili tunao uwezo wa kushirikiana hata na wafugaji wenyewe kuweka miundombinu, iwapo tu watakuwa wameambiwa kwamba hili ndilo eneo na wakagawiwa kama vitalu na kuweza kufanya shughuli hizo za kuweka miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua fedha wanazodaiwa bahati mbaya na baadhi ya watumishi ambao sio waaminifu, wakazitoa kwa namna ya rushwa, ni nyingi kuliko fedha ambazo zingeweza kutumika kuendeleza miundombinu na wafugaji wakawa katika eneo salama, la uhakika na ambalo hata lingeweza kutupa takwimu ambazo zingewezesha hata mwekezaji anayetaka kuwekeza kwenye maziwa akajua katika ukanda huu kuna mifugo ya aina hii na inaweza ikatoa maziwa kwa kiwango kile.
Mheshimiwa Naibu Spika, ilivyo sasa ni ngumu sana kwa Mheshimiwa Mwijage kumshawishi mtu kuweka kiwanda cha maziwa kwa watu wanaohama kwa sababu haijulikani kama mpaka wiki ijayo watakuwa katika eneo hilo. Nitaenda kwa undani wake tutakapokuwa tunajadili Mpango. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa pembejeo, Waheshimiwa Wabunge wameongea kwa uchungu sana. Na mimi katika kuzunguka katika kipindi kifupi, nimegundua utoaji wa pembejeo, ruzuku ambayo Serikali imekuwa ikitoa, uwianio wa fedha ambayo imetumika kwa takwimu na faida ambayo imetokana na utoaji wa ruzuku wa aina hiyo, haviendani.
Kwa hiyo, fedha imekuwa ikipotea kwa namna mbili; moja, ni kwa baadhi ya Maafisa pamoja na Mawakala wasio waaminifu kucheza deal. Wanapeleka mbegu, wanapeleka mbolea, wanapeleka mifuko ya kuonesha tu, baada ya hapo wanawapatia wananchi wengine ambao wameshapanda, wanawapatia kama ni 2,000 au 5,000, wanaondoka na mifuko ya mbolea na mifuko ya mbegu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara na Serikali kwa ujumla tunaangalia uwezekano wa kuwa na utaratibu mpya ambao utatoa majawabu ya kudumu ya tatizo hilo la upotevu wa ruzuku inayotelewa na Serikali. Tunaangalia uwezekano wa kuangalia kwenye makato, kwenye vitu vinavyosababisha bei ya mbolea inakuwa ya juu, tuweze kushughulika na bei hiyo na mbolea inayopatika iwe ya bei sawasawa na ya ruzuku na iweze kupatikana kwa wakulima wote badala ya wachache ambao wamekuwa wakilengwa kwa aina hii ya ruzuku. Nitalifafanua kwa kirefu wakati wa Mpango. (Makofi)
Jambo lingine ambalo ambalo Waheshimiwa Wabunge wameliongelea na lilimkera sana Mheshimiwa Rais wakati anazunguka na aliwaahidi Watanzania kwamba litafanyiwa kazi, ni jambo la makato mengi kwenye mazao ya wakulima. Tutalifanyia kazi, na niwaahidi tutakapokuja kujadili Mpango, nitaleta hayo mapendekezo na hatua ambazo Wizara inapanga kuzichukua.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata wewe nikukumbushe, kama mnataka mali mtaipata shambani. Ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)