Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa nafasi hii. Moja kwa moja nijielekeze kwenye kuchangia lakini sababu dakika tano ni chache sitaingia ndani sana ila nataka nitoe ushauri mmoja kabla sijatoa maelezo yangu ya jumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ambao nataka nitoe, kuna suala hapa limezungumzwa sana nalo ni la maji. Sera ya Taifa ya Maji ya mwaka 2002 pamoja na Sheria ya Maji Na. 5 ya mwaka 2019, Sheria hii ya Maji ya mwaka 2019 ndiyo ilianzisha RUWASA lakini kana kwamba haitoshi ikaenda mbele ikaleta Mfuko wa Maji wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alipokuwa anazunguka kufanya kampeni kwenye hotuba yake amekiri, namnukuu anasema: “Hata hivyo, napenda nikiri nilipokuwa kwenye kampeni moja ya changamoto kubwa niliyoelezwa na wananchi ilikuwa ni shida ya maji hususan maeneo ya vijijini”. Kwa sababu Mheshimiwa Rais ameshaliona hili, nashauri Serikali iirejeshe hapa ile Sheria ya Maji, Na. 5 iliyotungwa na Bunge letu ya mwaka 2019 ili tuirekebishe kidogo. Marekebisho yake yaweje? Tumeweka pale source ya fedha za huu Mfuko; tumesema tutatoza shilingi 50 kwenye petrol na shilingi 50 kwenye diesel. Nachoomba ili tuweze kuisaidia RUWASA lazima sheria ije hapa tuitengeneze iweze ku-state ni asilimia ngapi iende kwenye maji katika hiyo shilingi 100 inayotozwa kwenye petrol and diesel. Kwa sababu tukiiacha hivi miradi ya mjini inatumia fedha nyingi kuliko miradi iliyopo vijijini. Kwa hiyo, kuna haja ya kufanya hayo marekebisho ya hiyo sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la jumla sana mimi nataka tu niseme kwamba ndugu zangu unapopanga la kwanza unatumia takwimu na pili unatumia assumptions. Kwenye hili eneo la takwimu tusipojizatiti vizuri kuboresha namna ya upatikanaji wa takwimu kwenye nchi yetu kila tunapopanga tutakuwa tunajikuta tuko nje ya malengo. Kwa hiyo, ni vema tuboreshe sana eneo hili la takwimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwenye huu Mpango ambao ndiyo mpango wa mwisho kuelekea Vision yetu ya 2025 kama Taifa kukamilika wakati nimekuwa nikiusoma mara kwa mara na kuurejea sijaona mahali ambapo Mpango huu umeweka provision kwamba baada ya Vision 2025 kukamilika inayotekelezwa mwishoni kwenye huu Mpango ni kitu gani kitafuata? Vision nyingine itakapotengenezwa, sijaona provision kwenye Mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine tunapopanga ni vema tukajua financing mode ya hii miradi tunayoipanga especially hii miradi ambayo tunaita flagship projects. Ukifanya tathmini vizuri kwenye Mpango uliopita utagundua tulikuwa na miradi karibia 20 na yote ni mikubwa. Miradi 20 yote hii hatuwezi kui-finance na kodi za wananchi za kwetu za ndani. Kwa hiyo, ni vema tujikite kama taifa na ni wakati muafaka sasa tukubali tu kwamba ili tuitengeneze hii miradi ni lazima tutafute sources nyingine, namna nyingine ya kuitekeleza ama kwa partnership au kwa kukopa lakini tuifanye. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huohuo lazima twende na tahadhari, tumejaribu kufanya partnership pale Liganga na Mchuchuma na mradi huu umezungumzwa sana tokea tuko shule na bado mpaka leo haujatekelezeka. Naishauri Serikali yangu sikivu kama hili la Liganga na Mchuchuma limeshindikana kwa mwekezaji huyo tuliyenaye, ni vyema tukaenda mbele tukatafuta mtu mwingine kwa sababu dunia kwa sasa ni chuma na mafuta. Ni bidhaa mbili tu zinazotawala soko la dunia za mafuta na chuma. Kwa hiyo, tunapochukua muda mrefu miaka 7 toka 2014 tunafanya mazungumzo tunajichelewesha tu wenyewe. Tunahitaji tu- mobilize fedha kutokana na hii miradi ya kimkakati ambayo tunayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, mimi ya kwangu yalikuwa hayo machache. (Makofi)