Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. MARIAMU M. NYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii kwani ni mara yangu ya kwanza leo kuchangia katika Bunge lako Tukufu. Awali ya yote, naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia kuiona siku hii ya leo. Pili, naomba niwashukuru wazazi wangu, familia yangu, watu wangu wa karibu, Chama changu cha Mapinduzi na wanawake wa Mkoa wa Ruvuma kwa kunipa moyo na kuniamini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Awamu ya Tatu wa miaka Mitano 2021/2022 - 2025/2026 wenye dhima ya kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu. Katika Mpango huu, mambo muhimu yamezingatiwa kama kuchochea uchumi shindani na shirikishi; kuimarisha uwezo wa uzalishaji viwandani na utoaji huduma; kukuza biashara; kuchochea maendeleo ya watu na kuendeleza rasilimali watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mapitio ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka 2016/2017 na 2020/ 2021, tumeona jitihada kubwa za Serikali za kuwashirikisha wanawake katika nyanja mbalimbali ili kuleta usawa na kuondoa ukatili wa kijinsia, kuongeza fursa za kiuchumi, kuwajengea uwezo wa kufanya biashara, upatikanaji wa mitaji, upatikanaji wa masoko na upatikanaji wa mikopo yenye riba nafuu kwa baadhi ya mikoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ifike wakati sasa wanawake wa mikoa yote wapate fursa sawasawa wakiwemo wanawake wa Mkoa wa Ruvuma ili na wao waweze kujikimu kimaisha pamoja na familia zao kwa kuwapatia mikopo hiyo yenye riba nafuu na fursa nyinginezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mapendekezo ya Mpango wa Tatu, naomba kushauri mambo matatu yafuatayo. Moja, ianzishwe kanzi data itakayokuwa na vikundi vya wanawake nchini kimkoa ikionesha madaraja ya vikundi, mahitaji yao na namna ya kuyafikia mahitaji hayo kwa mfano mikopo yenye riba nafuu. Mbili, itolewe taarifa ya Benki ya Wanawake iliyohamishiwa Benki ya Posta, ni namna gani fursa za mikopo kwa akina mama zinatolewa kwa madaraja tofauti na fursa hizo zinapatikanaje kupitia benki hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba nitamke kama ifuatavyo. Wanawake hawa ili waweze kuchangia uchumi wanatakiwa wajengewe uwezo wa kujiamini kwa kuendeleza juhudi zao za kujitegemea na hatimaye waweze kuchangia Pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante. (Makofi)