Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naomba nianze kwa kusema kwamba jana Mheshimiwa Gambo aliuliza swali ambalo lilikuwa linahusiana na tozo mbalimbali ambazo zimeongezwa kwenye Hifadhi zetu za Taifa. Nami nikataka kuongeza kidogo mawazo yangu hapo kwamba wakati COVID inaingia duniani, tuliwashauri watalii tukasema don’t cancel your trip to Tanzania, postpone.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake ni kwamba wako watu walikuwa wamelipa, fedha zao zilikuwa tayari kwenye account za wateja; na kwa kuwa wali-postpone wanatarajia siku watakapokuja watahudumiwa kwa gharama ile ile waliyolipia mwaka 2020. Sasa haya mabadiliko yaliyofanywa, nataka kuwaambia Wizara ya Maliasili na Utalii wafahamu kwamba mteja aliyelipia mwaka 2019 aka-postpone safari akitarajia kuja Tanzania kukamilisha safari yake anatarajia kuhudumiwa kwa gharama ile ile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kukumbusha hapa pia kwamba liko tatizo kubwa kwamba tunataka kufikia watalii milioni tano, jambo jema kabisa, lakini watalii hawa wanalipia muda na ukarimu. Ukarimu wanaolipia ni pamoja na consistency ya makubaliano mnayokubaliana tangu siku hiyo unam-convince kuja Tanzania mpaka siku anapopata huduma na kuondoka. Mabadiliko yoyote katikati baada ya kulipia yanafanya watalii wengi zaidi wasije kuliko waliokuja Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nataka kuongeza jambo lingine moja. Sasa hivi requirement ya airline ni kwamba tunatakiwa tufanye COVID Test. Hii inafanyika nchi nzima lakini laboratory iko Dar es Salaam. Mtalii anahitaji siku tatu mpaka nne kwenda kufanya COVID Test Arusha kusubiri majibu na baadaye kupanda ndege kurudi kwao. Matumizi haya ya muda kwa watalii hayasaidii Tanzania kuongeza idadi ya watalii. Tufanye mabadiliko, tupeleke watumishi kule, tuchukue test tuwapelekee wataalam waweze ku-test. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, liko tatizo hapa linazungumzwa kuhusu tatizo la TRA. Nawapongeza sana kwa kukusanya fedha nyingi, lakini iko shida. Nimemsikiliza mtu mmoja wa TRA kwenye TV akiwa anahojiwa TBC, anasema sawa biashara zinafungwa, lakini zinafunguliwa nyingi zaidi. Tumesema kwa miaka mitano, kuna tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, iko hii kitu inaitwa Task Force. Tulifanya Mkutano na Mheshimiwa Kalemani pale Geita, tukaita wafanyabiashara wa Mkoa mzima wa Geita. Wanalalamikia TRA makadirio yao siyo rafiki. Kwa nini siyo rafiki? Inawezekana ni kwa sababu ya target kwamba ni kubwa kuliko survey ilivyofanyika ya uwezo wa walipa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuna tatizo na Regional Manager wa TRA, wasaidizi wake huku chini, wanaweza kukukadiria shilingi milioni 400, mwisho mkaishia shilingi milioni 30. Maana yake ni nini? Kuna room hapa katikati ya negotiation na Serikali inapoteza fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Task Force inafanya jambo moja. Wanakuja wanafanya special audit, wakishafanya wanakwambia unatakiwa kulipa shilingi bilioni tano. Wakati huyu mteja ana-appeal wanazuia account, wanachukua fedha zote kwenye account. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukikuta kuna fedha kwenye account ya mfanyabiashara leo, kwa mfano, biashara ya utalii; fedha siyo zake, ni za wateja wanaosubiri huduma. Unapozizuia maana yake unamzuia asitoe huduma kwa huyo mtalii, unazuia asilipe mishahara, unazuia asiendelee kufanya kazi. Ushauri wangu kwenye jambo hili, unapofanya special audit, ukagundua huyu mtu anatakiwa kulipa shilingi bilioni tano, akakata rufaa, wewe kabla hujatoa majibu ya rufaa ya aliyekata rufaa, umeshazuia account, umemnyang’anya passport, umepeleka maaskari pale kuzuia biashara. Kodi haitafutwi hivyo. Huwezi kutafuta kodi wakati compliance tax payers duniani wanabembelezwa. Dunia nzima ukiwa na compliance tax payer unawapa stimuli wakati wa shida ili waweze ku-survive walipe kodi. Sisi tunachokifanya tunatumia nguvu nyingi ku-meet target, matokeo yake tunawafanya watu wengi wana-exit business, tunafikiri wanaongezeka, lakini watu wanapungua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kushauri kwamba lazima tutafute namna bora ya kukusanya kodi, namna bora ya kuwalea wafanyabiashara tulionao. Leo na hapa getini wapo, wafanyabiashara walikuwa wanaingiza vitenge; analipa shilingi milioni 125, karudi ghafla anakuta container shilingi milioni 350, ameacha kulipa. Kesho yake atakachokifanya, akilipa anafunga duka, anatafuta machinga, anagawia watu barabarani. Akishindwa anahamia nchi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli tunataka kuisaidia Serikali kukusanya kodi, lazima Wizara ya Fedha watusikilize, tunazungumza na wananchi. Inawezekana hawana taarifa sahihi. Biashara zinakufa na watu wana…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. CONSTATINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

MWENYEKITI: Kengele imeshagonga, lakini acha nikuruhusu. Unasemaje Mheshimiwa?

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimuongezee Mheshimiwa Kanyasu kuhusu wafanyabiashara wa Kariakoo. Kwa kweli hilo ni tatizo kubwa kwa sababu sasa hivi ma-container mengi sana ya vitenge yako bandarini inapata labda miezi minne au mitano wameshindwa kulipa kodi kutokana na hilo ongezeko kubwa sana la kodi. Kodi imefikia mpaka milioni 400 kwa container moja wakati siku za nyuma walikuwa wakilipa milioni 165 au 160. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wanaweka zuio, wafanyabiashara tayari walikuwa wameshaweka order viwandani kule China. Mzigo unafika bandarini tayari kuna ongezeko la karibia shilingi milioni 200 na kidogo. Kwa hiyo, sasa mizigo hiyo iko bandarini mpaka sasa hivi hawajui wafanye nini. Kwa hiyo, mimi naiomba Serikali iangalie jinsi ya kuwapunguzia kodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naikubali kabisa Taarifa hiyo. (Makofi)