Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nafurahi kupata nafasi hii niweze kuchangia kuhusu Mpango huu uliowasilishwa na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu zaidi nataka nijikite kwenye suala zima la kilimo. Wachangiaji wengi wameonesha namna gani tunaweza kuendelea kwenye suala zima la kilimo. Ni dhahiri kwamba, nchi za Afrika tumekuwa tuna-export zaidi madini kwa maana ya extractive lakini tumekuwa hatufanyi vizuri katika ku-export mazao ya kilimo. Kwa hiyo, nataka nirudie na kusema kilimo tunahitaji wawekezaji lakini vilevile tunahitaji Serikali iwekeze kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu nataka nijikite zaidi kwa Mkoa wa Dodoma. Mkoa wa Dodoma unachukuliwa ni mkoa ambao hauwezi kustawisha mazao na kilimo kiko chini lakini tujiulize ni kiasi gani cha maji kinachopotea katika mkoa huu. Nianzie tu karibu pale Kibaigwa, lile bonde linavyotoa maji kwenda kule. Nenda Mpwapwa ile milima na mabonde yale, nenda hadi Mto Ruaha pale, anza kushuka njoo huku Dodoma, ingia Chalinze hapa uende hadi Bahi kule na swamps zote zile, lakini maji haya miaka nenda rudi yamekuwa yanapotea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimewahi kwenda Egypt. Ukifika Egypt huwezi ukadhani kama uko kwenye jangwa. Egypt baadhi ya watu hawajawahi kuiona mvua maana mara nyingi inanyesha mara moja tena ni vinyunyu kwa mwaka na kama umelala huioni tena, lakini ni nchi ambayo it is very green kuanzia Cairo mpaka Alexandria, nchi yote imestawishwa kwa umwagiliaji. Naichukulia Dodoma iko sawasawa na Egypt na Israeli. Tena nazilinganisha tu basi lakini sisi hatuwezi kulinganishwa na Israel na Egypt, sisi tuko better off.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu za mwaka 2017, export value ya Egypt katika mazao ya kilimo ilikuwa ni Dola bilioni 2.2. Ukija Tanzania export ya mazao ya kilimo ilikuwa ni Dola 8,000,030 na hiyo siyo kwenye hotculture products ni mazao ya pamba, chai na kahawa. Kwa hiyo, nachotaka kusema ni kwamba tuna nafasi kubwa ya sisi kuweza kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Dodoma hapa tuna zao la zabibu lakini hatujalitendea haki. Nchi ya Israel imeweza ku-export ule mchuzi kwa thamani ya Dola milioni 240 kwa mwaka lakini zabibu ya Dodoma ndiyo zabibu ambayo unaweza kui-train izae muda wowote unavyotaka. Zabibu ya Dodoma wanasema ni nzuri katika dunia nzima kwa maana ya sukari lakini na namna ya ku-train kwamba iweze kuzaa. Unaenda hivyo hivyo Egypt, wenzetu wako mbali kwenye kuuza mchuzi wa zabibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije kwenye hoja yangu kwanini nataka kusema kwamba Serikali iwekeze kwenye kilimo. Tunahangaika kuchimba maji ya chini, tunatafuta maji underground huko kwenye miamba maji ambayo hatuyaoni ndiyo tunahangaika nayo, lakini maji yanayopita kila mwaka hapa mwaka huu yatapotea na mwakani yatapotea, hivi hatuwezi kweli tuka-tap maji haya yakutosha na tukaweza kulima kwa uhakika muda wote. Naamini kabisa Mkoa wa Dodoma huu unaweza hata ukalisha kwa kiasi kikubwa kulisha hata nchi yetu kwa maana ya umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna ardhi nzuri, ina rutuba lakini tunaenda hadi lini kwa utaratibu huu, maji yanapotea muda wote na nataka niseme wenzetu wamejikita zaidi kwenye hotculture ambayo kwanza hutakiwi kutumia maji mengi, ni maji yanaenda kwa utaratibu,acha hii massive kama tunavyomwagilia katika mazao mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo, nataka niishauri Serikali kwamba hebu tutoke kwenye kutafuta maji chini ya ardhi, tutumie maji haya ambayo tunayo kwenye mito.Wakati tuko Egypt nilikuwa kwenye delegation, mkuu wetu wa msafara aliulizwa kwanini Tanzania mna maji lakini bado hamfanyi vizuri kwenye kilimo. Tulienda kwenye shamba la ng’ombe 35,000 jangwani Egypt, kwanza yule mwenye shamba alihojiwa akaulizwa na Waziri wetu kwamba...

MWENYEKITI: Ng’ombe 35,000?

MHE. ERNEST K. NOLLO: Ndio ng’ombe 35,000.

MWENYEKITI: Kongwa Ranch ng’ombe hawafiki 10,000, endelea tu Mheshimiwa.

MHE. ERNEST K. NOLLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo shamba lile linalima nyasi kwa umwagiliaji jangwani na sera ya Egypt ni kwamba unaweza ukapata maji kwenye Mto Nile, lakini mtu wa Egypt anasema unatakiwa uchimbe kama hujayapata hujachimba. Kwahiyo mtu wa Egypt ataenda chini miles na mile lazima ayapate maji. Hii spiritna maji tuliyonayo hata Mwenyezi Mungu nataka niseme anatushangaa na atatushangaa kweli kweli.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka miujiza gani na maji haya tuliyonayo, ile pale nimetoa mfano pale Kibaigwa, kuna kipindi utadhani ni bahari, lakini maji yale yanapotea. Njoo kwetu Bahi sasa tuna-swamp ambayo imejaa maji kwelikweli, lakini hatuwazi kulima nyasi kwa kumwagilia, tupate maziwa yakutosha muda wote, hatuwazi maji yenyewe yatutosheleze, hatuwazi maji kwa ajili ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tungefanya hata anasa kama Kazakhstan, walichofanyawalihamia mji mpya ule wa Almaty, wakasema sasa tutengeneze kabahari, wakatengeneza bahari, maana waliona watu wengi wakiwa wana-relaxkama ilivyo Dar es Salaam wanaona bahari, ikaja kujengwa bahari, ni matumizi ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa uwekezaji kama wa umeme na reli ni gharama kubwa sana, lakini na hili nalo tulifanye, hivi kweli Serikali kwa maana tumetoa sasa ma- exavetor mwezi mzima wanachimba, hatuwezi kupata bwawa kubwa ambalo tutaweza kumwagilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka hapo wenzangu wengi wamesema kwa habari ya mafuta,edible oil. Tumeongea sana, hivi ukatoa viwanda viwili tu pale Singida viwe vya bilioni 700, bilioni 500 tunamaliza kabisa habari ya edible oil kwenye nchi hii. Tuache habari ya kwamba tukuze michikichi baadaye tuanze kupata mafuta, lakini alizeti tukiamua miaka miwili hii tunamaliza habari yaku-import edible oil.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii,lakini kwa kweli nataka niseme Serikali jambo hili la uwekezaji kwenye kilimo tulichukulie serious, kwa maana ya kwamba hatuwezi kuwekeza kushindana kama alivyosema muwasilishaji alisema tunataka tuwe na ushindani wa kibiashara, lakini nashindana na nani katika sekta ipi? Sisi mashindano yetu yawe kwenye kilimo, tulikuwa na wenzenu akina Malaysia, akina Hongkong na akina Singapore, wale walikuwa ni wenzetu, lakini sasa wameshatoka kwenye uzalishaji wa kilimo wako kwenye teknolojia lakini sasa sisi tuko na wenzetu washindani kwenye sekta ya kilimo bado tuna lag behind, kwahiyo tunashindana vipi? Nataka niseme kwenye mambo elekezi seriouskwa maana ya kwamba sisi tuko kwenye stage ya uzalishaji kwenye teknolojia hatupo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio kile ulichokuwa unasema kwamba ku-exportbrain, ile ni serviceindustryambayo sasa dunia ya wajanja na wameshafikia hapo tunawapataje akina Heron Max, tunawapataje hawa jamaa wa facebook,kile ndiyo kitu cha msingi sasa, unatengeneza kitu kidogo lakini unatoa bilions of money, sasa huko sisi hatujafika, lakini mambo mengine haya kwa mfano ya uwekezaji wa watu wetu, tunaweza tukafanya na tukaweza kupiga hatua kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)