Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga mkono hoja, na ningependa kuchangia kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza kwa changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika hoja hii. Elimu ndiyo msingi wa mambo yote hapa Duniani, yapo mambo ambayo yanatakiwa kuboreshwa ili tuzidi kuongeza ubora wa elimu yetu. Kwa mfano, mitaala yetu inabidi iangaliwe upya, tujaribu kuangalia mitaala ya nchi zingine zinazofanya vizuri ili tuiboreshe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitengo cha Ukaguzi cha Wizara inabidi kiimarishwe, sikumbuki au kusikia Wakaguzi wamekuja Muheza. Hawa ndiyo wanaweza kuboresha mambo mengi ni watu muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna upungufu mkubwa wa Walimu Muheza. Ingawa ni suala lililopo TAMISEMI shule za msingi na sekondari zote, ninaomba uliangalie kwa umuhimu wake, kuna shule zingne zina walimu wawili na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara sasa ni vizuri ifikirie kuanzisha mitihani mara mbili kama wenzetu wengi badala ya kungojea mwaka mzima kwa O- level na A- Level. Pia maslahi ya walimu yaangaliwe kwani inaonekana kama wamesahulika sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msisitizo mkubwa naona Muheza High School ambayo ni hiyo tu Wilaya nzima ifanywe ya kutwa na bweni ili iweze kuhudumia ongezeko la wanafunzi wa „O‟ Level Wilaya nzima. Shule hiyo ilijengwa kwa nguvu za wananchi na ina uwezo mkubwa wa kuchukua wanafunzi wengi zaidi. Wizara isimamie TAMISEMI kuona vifaa vya maabara shule za sekondari vinapelekwa.