Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Awali na yote na mimi nianze kwa kumshukuru Mungu kwa afya na kwa hatua hii.

Nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa kunipa upendeleo huu tena wa kuendelea kumsaidia katika nafasi hii ya Waziri wa Katiba na Sheria. Pia niwashukuru wapiga kura wangu wa Jimbo la Iramba kwa kunirejesha tena Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikirejea kwenye hoja zilizojitokeza hapa leo, hoja ambayo iko mbele yetu ni Hotuba ya Rais na sisi kwa upande wa Mawaziri Hotuba ya Rais ni maelekezo na ni dira na sisi tumepokea twende tukaifanyie kazi. Kwa hiyo, kitu pekee ambacho nitazungumzia hapa, niwapongeze sana Waheshimiwa Wabunge ambao wamechangia katika mwelekeo huo wakitambua kwamba jambo hili ni la kisera. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitafafanua tu mambo machache yale ambayo yaliguswa katika Wizara ya Katiba na Sheria. Kuna baadhi ya mambo ambayo yameongelewa, niongee huku nikiwa natoa rai kwa Waheshimiwa Wabunge sisi kama viongozi tuwe watu wa kwanza kuzingatia masuala yanayohusu sheria na katiba ya nchi yetu. Kuna hoja hapa zilizokuwa zinatolewa kwa muundo wa nchi yetu na mipaka ya kikatiba iliyowekwa kwenye taasisi zetu na hata kikanuni humu humu ndani ya Bunge hayapaswi kuongelewa. Sitataja moja baada ya lingine lakini kuna masuala ambayo yameongelea kesi ambazo ziko mahakamani ambazo ziko kwenye mhimili mwingine wa kutoa haki.

Mheshimiwa Naibu Spika, masuala ya aina hiyo Waheshimiwa Wabunge yanapokuwa yako kwenye mhimili ambao unasimamia masuala tena uliopewa mamlaka haya ya kikatiba ni masuala ambayo hayapaswi kuongelewa kwa hisia tu na hayapaswi kuongelewa tunapokuwa hapa kama kanuni zetu zinavyoelezea.

Kwa hiyo, kwa hoja zile zilizojitokeza zilizokuwa zinalenga masuala ambayo yako kwenye mahakama zetu tuache utaratibu wa kikatiba, sheria na kanuni tunazozitumia uweze kufanya kazi yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata kuna mambo mengine baadhi ya wachangiaji walitaka kuyajenga kama vile yanafanyika kwa hisia kama wao walivyobeba hisia. Wanasema kuna watu wetu wamewekwa ndani, kuna watu wetu wamebandikwa kesi, kuna watu wetu wamekamatwa na wengine wanafika hatua ya kusema tu Waziri anayeshughulikia awaachie. Tunawatengenezea Watanzania hisia kana kwamba kuna watu wanaweza wakawekwa ndani bila makosa na kana kwamba kuna watu wanaweza wakatolewa bila kufuata taratibu zetu za kikatiba na za kisheria tulizoziweka. Huu siyo utaratibu uliosawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wengine wanasema ni kesi za uchaguzi, niwaambieni na sote tuwe na uelewa wa pamoja, kesi za uchaguzi ni zile zinazohusu rufaa zinazopinga matokeo ama zinazopinga mwenendo. Makosa yoyote ya jinai yanayotokea wakati wa uchaguzi hayafi kwa sababu ulikuwa ni wakati wa uchaguzi. Jinai si kesi ya uchaguzi ni kesi ya makosa ya jinai na taratibu zake za jinsi ya kufanyiwa kazi tumeweka kwenye Katiba na sheria zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mengine yako kwenye mamlaka ambayo imepewa mamlaka yake ya kuchunguza kikatiba na kisheria, hatuyafuti kwa hisia. Mamlaka ya Mkurugenzi wa Mashtaka na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka iko kikatiba na imepewa mamlaka ya kuangalia kesi ambazo hazifai kuendelea ikazifuta na kesi ambazo zinafaa kuendelea ziendelee. Hatuzifuti kwa hisia wala hatuzifuti kwa maelekezo, ni mamlaka inayojitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuyaelewe haya na tuwaelezee wananchi wetu ili waelewe mipaka ya utawala wa kisheria. Utawala wa kisheria unaendeshwa kwa sheria siyo kwa hisia. Tukiendelea na utaratibu huu wa kusema kwa hisia tunaichafua nchi yetu ambapo wengine sisi hatuna mbadala wa nchi, nchi yetu ni hiihii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niliona mengine yanaibuka watu wanasema haki, haki, haki. Kati ya jambo ambalo nina uhakika nalo hata lisingeandikwa kwenye kakitabu kokote kale kwa Rais Magufuli limeandikwa moyoni ni jambo la haki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wengine wanasema Tume, Tume. Hivi kwa kazi zote hizi zilizoorodheshwa unaenda kushindana kwenye uchaguzi huu na Rais Magufuli utashindaje, unataka Tume ikusaidieje? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wote tushuhudieni tulipokuwa Majimboni walikuwa wanasema tushindane Udiwani na Ubunge kwa Rais tiki. Wewe unaenda kwanza huna agenda, pili huna mgombea, mgombea wako ana tiketi ya kuja na ya kuondokea, unategemea Tume ya Uchaguzi ikusaidie, inakusaidia wapi? Lazima uanze kuanzia mwanzo uangalie ulikuwa una agenda gani kwenye uchaguzi huo na ulikuwa na mgombea gani, mgombea anayeangalia tiketi, anaangalia nitawahi vipi ndege hii halafu unategemea umpambanishe na mtu ambaye usiku na mchana anashughulika na maisha ya Watanzania, hili haliko sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mnaongelea uchumi wa kati eti tumeingizwa uchumi wa kati, ama tumedanganywa, sijui takwimu haziko sawa. Sikilizeni, uchumi wa kati hatuingii kwa kupigiwa kura, hii siyo Bongo Star Search, ni jambo la maisha ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama miaka mitano zaidi ya vijiji 9,800 vimepata umeme na wananchi wake wameunganisha umeme ule. Kama ndani ya miaka mitano zaidi ya trilioni tatu zimekwenda kwenye elimu, zaidi ya trilioni mbili zimekwenda kwenye maji, zaidi ya trilioni moja imekwenda kwenye afya, zaidi ya trilioni moja imekwenda kwenye utawala bora, zaidi ya trilioni tisa zimekwenda kwenye miundombinu ya kuunganisha hawa watu wasafirishe mazao yao, wewe unashangaa kwamba eti tumeambiwa tumeingia, hujui hata kama umeshaingia! Wale ambao wanapata mashaka na jambo hili ombeni darasa muelezewe tu masuala ya uchumi wa kati yanaendaje ili tuache kuichafua nchi yetu wakati inapiga hatua. Hata wale wanaoweka vigezo hivi wanatuheshimu ndiyo maana hata kwa lugha yao kila wakipata tatizo wanasema we need a person like Magufuli ninyi mnakwama wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi, mengine tutaongea kwenye mpango wa maendeleo wiki inayofuata. Ahsante sana, naunga mkono hoja 100%. (Makofi)