Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi ya kusimama ndani ya Bunge hili. Naishukuru familia yangu, Wajumbe wote na wananchi wote wa Buchosa walionipa nafasi ya kuwa hapa, Chama changu Cha Mapinduzi, Mwenyekiti, Katibu wa Chama chetu cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nachukua nafasi hii kuwashukuru sana viongozi wa nchi yetu waliotangulia ambao kwa uwepo wao, maisha yangu leo ni bora zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi yetu leo hapa ni kujadili hotuba mbili za Mheshimiwa Rais. Nami nimepata bahati ya kuzisoma kama walivyozisoma wenzangu wote, nimezisoma na nimezielewa. Katika kuzisoma kuna kitu kimoja kikubwa nilichokigundua kwamba Mheshimiwa Rais anawaamini sana Wabunge wake na anaamini kwamba hakuna kiongozi duniani anayefanikiwa peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, Musa alichagua wazee; Yesu Kristo alikuwa na wanafunzi wake 12; na Mtume Muhammad alikuwa na Maswahaba wake. Kwa hiyo, sisi hapa ndani ni Maswahaba wa Mheshimiwa Rais, ametuamini, amekuja kutusomea hotuba hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusoma, nimekumbuka kitabu kimoja nilikisoma kinaitwa Checklist Manifesto. Kwa wale ambao wamekisoma watagundua kwamba hotuba hizi mbili za Mheshimiwa Rais ni Checklist Manifesto mbili; ya kwanza ilikuwa ya 2015 – 2020 ambayo inaonyesha mambo ambayo Mheshimiwa Rais alitaka kuyafanya kwenye kipindi cha miaka mitano. Nikiwauliza kwenye Checklist Manifesto, kazi yako ni ku-list mambo yako, unatiki moja baada ya lingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikikuuliza wewe na Waheshimiwa Wabunge kwamba kwenye miundombinu, Mheshimiwa Rais ametiki au hajatiki?

WABUNGE FULANI: Ametiki! (Makofi)

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwauliza kwenye umeme, Mheshimiwa Rais ametiki, hajatiki? Kwenye barabara, ametiki hajatiki? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni mengi yametikika. Sasa tuna Cheklist Manifesto ya pili ya mwaka 2020 – 2025, ni checklist ngumu zaidi ya checklist tuliyomaliza. Ni ngumu kwa sababu nchi yetu iko kwenye uchumi wa kati. Ni checklist ambayo siyo rahisi kama iliyopita. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuja kwenu na nazungumza mbele yako na mbele ya Watanzania wote kuwakumbusha kwamba kasi tuliyonayo ni kubwa. Mengi yamefanyika, kazi kubwa imefanyika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wetu, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu, nawapongeza Waheshimiwa Wabunge wote, lakini nataka niwakumbushe kwamba kazi tuliyonayo mbele ni kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mtu mmoja aliwahi kusema kwamba the smallest of implementation is better than the biggest of intensions. Kama hatutatekeleza hotuba hii, tukabaki na mazungumzo ya hotuba nzuri, hakika hotuba hii ya Mheshimiwa Rais itabaki ni intensions peke yake, hakuna matokeo yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi natokea private sector. Kwenye private sector hatuna hotuba nyingi sana, tuna utendaji peke yake. Nazungumza hapa nikiwaomba Waheshimiwa Wabunge, katika Checklist Manifesto ya pili 2025, tufanye kazi, tumuunge mkono Mheshimiwa Rais, tusimvunje moyo Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma katika hotuba yake, ukurasa siukumbuki vizuri, lakini amesema kwamba mazao ya bahari yangeweza kuiingizia nchi yetu shilingi bilioni 320 na kitu hivi kwa mwaka. Tunazozipata ni kidogo mno kwa sababu tulishindwa kudhibiti na kusimamia vizuri, (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia nyuma ya statement hiyo kwa mimi mwanafasihi, nagundua kwamba Mheshimiwa Rais alikuwa na manung’uniko, alikuwa na masikitiko. Nawaomba Waheshimiwa Mawaziri walioko hapa ambao mmepewa jukumu, mmefanya kazi nzuri sana kwenye checklist manifesto ya kwanza. Mmeaminiwa, fanyeni kazi, tumikeni, tengenezeni historia, tuko hapa kujenga historia yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, watoto wetu watakapokuja baada ya miaka 20 waseme maisha yao ni bora sana kwa sababu Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuwa kaka yangu Majaliwa. Watoto wetu wasimame waseme maisha yao ni bora kwa sababu sisi tulioko ndani ya ukumbi huu leo tutafanya maamuzi sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa kuwaomba ndugu zangu, Watanzania wanatuamini, dunia inatutazama, tutakachokifanya hapa ndani katika kipindi cha 2025 ni kufanya maamuzi ambayo tutatekeleza ndoto ya Mheshimiwa Rais wetu. Viwanda ni ndoto ya Rais wetu lakini hakuna viwanda bila kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikomee hapo. Ahsanteni sana, naunga mkono hoja. (Makofi)