Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi na nawashukuru wote kila mmoja kwa nafasi yake aliyechangia uwepo wangu mahali hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kupokea Hotuba ya Rais kwa mikono miwili na nampongeza sana kwa sababu sisi kama Wabunge, tumepokea dira na tumepata kitendea kazi cha kufanyia kazi katika uwakilishi wa wananchi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, naanza na sekta ya utalii, katika ukurasa wa 46, Mheshimiwa Rais ameongea kwamba ni sekta ambayo itawekewa mkazo mkubwa kutokana na umuhimu wake katika Taifa letu; kwanza, katika mchango wake mkubwa katika kuongeza pato la Taifa, pia ni sekta ambayo itatoa ajira kwa vijana wetu kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza upande wa Serikali; wenzetu hili wameshalianza, nasi watu wa Kanda ya Kusini au Southern Socket Tourism tunawashukuru sana kwa sababu tumeletewa mradi mkubwa wa REGROW ambao umetengewa dola milioni 150 kwa ajili ya kuendeleza utalii kusini; Iringa pia haikuachwa, itakuwa hub ya utalii huo, nasi tumepewa dola milioni sita kwa ajili ya kuanzisha Tourist Resource Center pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunawashukuru sana kuhusu msitu wa Kihesa Kilolo. Namshukuru Waziri wa Maliasili, tumeongea hili na amelifanyia kazi kwa haraka sana. Naamini ujenzi unaanza pale mara moja ili nasi southern socket au ukanda wa kusini tuwe sehemu ya kuchangia pato la Taifa kupitia utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba, ili utalii uweze kuwa mzuri, tunahitaji kuboresha huduma zetu kwa watalii. Kwanza, naomba tuboreshe huduma ya upatikanaji wa ubadilishanaji wa fedha za kigeni. Watalii wetu wengi wanapokuja kwenye zones za utalii wanakosa huduma hii kutokana na mchakato ambao ulipitishwa kwenye maduka yetu ya kubadilisha fedha za kigeni. Kwa hiyo, tunaomba Serikali iangalie hasa kwenye hizi nyanda za utalii, ni namna gani inalegeza masharti ili tuweze kuwahudumia watalii na lile neno lao, watakaporudi tutapata watalii zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kuhusu kuboresha huduma za miundombinu, tunaomba barabara. Tumeshaanza kuboreshewa kiwanja cha ndege, sasa tunaomba barabara ile ya National Park, watakaposhuka pale ile barabara ya kutoka Iringa mpaka Ruaha National Park ya kilometa 104 basi nayo iboreshwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye suala la elimu. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa ukarabati mkubwa uliofanyika kwenye Shule za Sekondari kongwe, tunaomba juhudi zile zile zielekezwe kwenye shule zetu za msingi kwani nazo zimechakaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mtaala haliepukiki, tunaomba Wizara ya Elimu tujipange kubadilisha mtaala kwa watoto wetu ili watoto wetu waweze kuajirika na kujiajiri nje na ndani ya nchi yetu. Tunaomba sana elimu ya kujitegemea irudishwe kwenye shule zetu ili watoto hawa wanapotoka waweze kujifunza kujitegemea. Vile vile tunaomba kuwe na masomo compulsory kama ya ujasiriamali kuanzia kwenye level ya shule ya msingi ili watoto waweze ku-develop visions zao wenyewe tangu wakiwa wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru sana kwamba kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais pia amesema kutakuwa na program mbalimbali za mafunzo ya ujuzi na maarifa ili kukuza uchumi. Tunaomba sasa vyuo vikuu vilivyoko kwenye zones zetu na mikoa yetu, kama kile Chuo Kikuu cha Mkwawa, kiwe independent, kiweze kusimama chenyewe ili kisaidie kutengeneza program zao kwenye kanda zetu zile ili kuwasaidia watoto wetu waweze kupata maarifa ya kufaidika na mazingira yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tusiendelee kuwa ni Vyuo Vikuu Shirikishi halafu vinaendelea kupokea program zinazopangwa Dar es Salaam wakati kule kule zinge-scan mazingira ya kule, zingepanga program za kule kule, zitawasaidia wananchi wetu. Tunaomba sana hili lichikuliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye suala la uchumi, tunashukuru kwa ajili ya uzalishaji, lakini tunaomba sana mafunzo ya ujasiriamali yatiliwe mkazo kwa sekta binafsi lakini kwa informal sector na formal sector. Tunaomba makundi yale ya Madereva, Wamachinga, makundi ya bodaboda, yapewe mafunzo ya ujasiriamali ya kimkakati kutokana na kazi zao. Mafunzo ya ujasiriamali yasiandaliwe tu kwa ujumla, lakini yaende specific. Kwamba hawa ni Mama Ntilie, katika sekta yao tunawaboresha vipi? Hawa ni madereva wa bajaji, katika sekta yao tunawaboresha vipi? Tusitafute kupeleka mafunzo ambayo ni mafunzo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa kengele imeshagonga.

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, dakika moja. Kulinda tunu za Taifa, naomba hili niliseme. Hapa yameongelewa masuala…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Jesca kuna majina mengi hapa mbele. Ahsante sana.

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)