Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua Serikali imejipangaje katika mambo yafuatayo kwa Wizara hii:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyuo vya Ualimu baada ya kupelekwa NACTE vimekuwa vikikosa wananfunzi wa kutosha kulingana na capacity ya Chuo na ukilinganisha na idadi kubwa ya wananfunzi wanaosajiliwa katika shule za msingi kutokana na Sera ya Elimu Bure. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha nchi yetu inakuwa na walimu wa kutosha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyuo vya Ualimu vimeingia NACTE, lakini stahiki za Wakufunzi bado hazijabadilishwa kuendana na mfumo wa NACTE. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Wakufunzi nao wanapata stahiki zao vizuri bila ubabaishaji?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Je, Serikali imejipangaje kuzuia ombwe kubwa la Walimu kuacha kazi na kutafuta kazi nyingine hivyo kupelekea ukosefu wa Walimu hasa katika shule za Vijijini mfano, katika Mkoa wa Mtwara, ambao mimi ninauwakilisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vyuo vingi vya Ualimu vinafundisha masomo ya sayansi, lakini havina maabara. Hivyo, kufanya ufundishaji na ujifunzaji uwe mgumu na kadhalika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha maabara hizo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi kuwakopesha wanachuo, ambao wanasoma katika vyuo vya ualimu masomo ya sayansi, lakini haijafanya hivyo, ni kwa nini na kuna mpango gani uliowekwa kuhakikisha ahadi hiyo inatekelezeka kwani inawanyima haki wanachuo hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, vyuo vingi vya Ualimu havina mtandao wa internet wa uhakika. Je, Serikali inalijua hilo na imejipangaje kuhakikisha mtandao unapatikana ili kuwezesha ufundishaji na ujifunzaji unaenda vizuri ukizingatia hakuna vitabu vya kutosha katika vyuo hivyo.