Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa name ni mara yangu ya kwanza kusimama katika Bunge lako Tukufu, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ameniwezesha kufika kwenye Bunge hili leo. Pia naomba nikishukuru Chama changu Cha Mapinduzi, Jumuiya ya Wanawake pamoja na wanake wema sana wa Mkoa wa Pwani ambao waliridhia kunisindikiza na kunifanya niweze kuwa Mbunge wao kuwawakilisha. Navishukuru Vyama vya Wafanyakazi; pia nashukuru familia yangu, Mama yangu, ndugu, jamaa na marafiki kwa ujumla wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikijielekeza kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais, nimesoma hotuba zote za 2015 na 2020; Mheshimiwa Rais ameonyesha nia njema na dira katika kuiendeleza Tanzania, lakini ameonyesha dhamira ya wazi kwenye kulinda amani yetu na pia kuudumisha Muungano wetu. Nina sababu zote za kushukuru Vyombo vya Usalama na Ulinzi ambavyo kwa pamoja na wananchi wenye nia njema wameweza kushirikiana kuendelea kulinda amani ya nchi yetu. Wanastahili pongezi kubwa sana vyombo vya Ulinzi na Usalama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, tumeona suala nzima la huduma za jamii katika ujumla wake, wenzangu wamezungumzia, lakini naomba nijikite kwenye suala la afya. Ukiangalia kwenye Ilani na hotuba yake, Mheshimiwa Rais ameeleza nia njema kabisa ya kuboresha huduma za kibigwa na pia kuongeza miundombinu pamoja na vifaa vya kutosha vya kisasa. Siyo suala la kupinga kabisa lipo wazi kwa jinsi ambavyo huduma za kibigwa zimeimarika. Ukiangalia taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, halina ubishi wote tunafahamu. Muhimbili hiyo hiyo mpaka sasa wanapandikiza figo, wanaweka masikio, cochlear implant, wanafungua kichwa ubongo bila kufungua fuvu. Kwa hiyo, huduma nyingi zimeimarishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nayasema hayo kwa sababu nina jambo moja la kulisema. Katika suala nzima la magonjwa la kiharusi (stroke) imekuwa ni tatizo ambalo ni kubwa sana kwa siku admission au wanalazwa wagonjwa watano mpaka sita Muhimbili, acha Mlonganzila au hospitali zingine za rufaa. Kwa hiyo nina wazo moja, tunaomba taaisisi ya Stroke ianzishwe; wagonjwa wale wanakaa muda mrefu, wanachangwanywa na wagonjwa wengine, immunity yao ni ndogo. Kwa hiyo kuna uwezekano kama wakianzisha stroke center kama wenzetu South Africa na Egypt wanafanya pawe na stroke nurse, pawe na wataalam, kwa hiyo itakuwa ni kitengo kinachojitegemea, kitafanya outreach, elimu kwa jamii pamoja na kuwa na Manesi katika hospitali zingine ambazo ni kubwa ili kupunguza tatizo la stroke ambayo sisi wote ni wahanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye Hospitali yetu ya Mirembe. Hii ni hospitali ya muda mrefu, ina miaka 93, imeanzishwa mwaka 1927. Hii hospitali inachukua Watanzania wa kawaida na sisi ni wahanga hatuwezi kukwepa kuingia pale siku moja. Hii hospitali ni ya muda mrefu ina miundombinu chakavu, mikongwe, lakini inasababisha kupata taswira nzima ya huduma njema inayotolewa pale. Pili ipo katika Makao Makuu ya Nchi. Mazingira mazuri yanawatia moyo wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii na Watanzania wale ingawa afya yao ina matatizo lakini wanastahili kukaa kwenye mazingira mazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, bed state kwa siku wagonjwa hawapungui mia tano, kuna Isanga, kuna Mirembe Proper na vituo vingine vya kutolea dawa za kulevya, vyote hivyo viko chini ya Mirembe. Naomba sasa ufike wakati bajeti yao iongezwe, ikiwezekana sasa iwe taasisi, kwa mwezi wanatumia zaidi ya milioni 280, kwa maana ya huduma za kila siku kwenye taasisi ile. Naomba iangaliwe taasisi ya Mirembe kwa sababu sisi sote ni wahanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja (Makofi)