Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama kwenye Bunge hili, nipende kumshukuru kwanza Mwenyezi Mungu kwa nafasi niliyoipata. Pia niwashukuru sana wananchi wa Jimbo la Makete kwa kuniamini na kunichagua kuwa Mbunge wao. Kubwa zaidi nimpongeze Mheshimiwa Rais na Wabunge wote wa Chama cha Mapinduzi kwa ushindi mkubwa walioupata, ni kitu ambacho mimi kama Mbunge kwa kweli niseme hongereni sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais naomba kuchangia mambo matatu. Jambo la kwanza naomba kuchangia kwenye sekta ya barabara. Tumeona jitihada za Rais akipambana kuhakikisha kwamba barabara zinajengwa kwenye kila kona ya nchi hii, wilaya na kila mkoa. Kwa kule Makete sisi tumepata barabara kutoka Njombe kuelekea Makete ambayo imekamilika kwa kiwango cha lami. Naomba kuishauri na kuiomba Serikali tuna barabara ya kutoka Makete kuelekea Mbeya, moja kati ya barabara ambazo zimebeba msingi wa uchumi wa Wilaya ya Makete, nawaomba na nawasihi sana wahusika ambao ni Wizara ya Ujenzi waiangalie barabara hii kwa jicho la karibu ili wananchi wa Makete waweze kupata huduma hiyo ya barabara ya lami, kwa sababu uchumi wa Makete unakua lakini unakwamishwa na barabara hiyo ambayo kwa kweli ni barabara muhimu wa Wilaya ya Makete.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, naomba nichangie kwenye sekta ya kilimo. Sisi Makete ni wilaya ya kazi kama ambavyo wananchi wengi wa Tanzania wanafahamu wananchi wa Makete ni watu wa kazi. Kwenye kilimo Mheshimiwa Rais ameonyesha kwenye hotuba kwamba ana lengo la kuboresha kilimo. Changamoto ya kwanza kwa wananchi wa Makete tunalia na lumbesa kwa ajili ya wananchi wetu na wakulima wetu wa Makete. Wakulima wanalima lakini tatizo la lumbesa kwa wananchi wetu ni kubwa. Naishauri Serikali mambo matatu; ushauri wa kwanza kwenye Serikali ni jambo moja, kwanza Wakala wa Vipimo waoneshe kipimo kipi ni rasmi kwa ajili ya kuuzia mazao yetu ya mahindi pamoja na viazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, naomba Wizara husika ya Kilimo waanzishe sales point (vituo vya kuuzia) ili wakulima wetu waweze kuwa controlled kwenye biashara kuondokana na suala la lumbesa. Lumbesa ni kilio, wananchi wangu wa Matamba, Makete na Ujuni wanalia na lumbesa, tunaomba sana ili tuweze kumboresha mkulima huyu lazima tuondoe suala la lumbesa na nawasihi na kuwaomba sana Wizara husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo langu la tatu, naomba kuchangia kwenye suala la mapato. Rais amezungumza mambo mengi sana; hapa tuna mambo ya ujenzi wa barabara, tuna mambo ya umeme, tuna mambo mengi ya kiuchumi ambayo yanahitaji fedha, lakini kuna eneo moja ambalo tumeliacha kwa muda mrefu fedha nyingi zinapotea, nako ni kwenye suala la tozo, kwa maana ya kwamba non tax revenue. Rais amepambana kwa level yake, kwa maana ya kwamba ukiangalia kwenye eneo kama la vitambulisho vya wajasiriamali, mambo ya magawio saa hizi tumeanza kuyapata, naiomba na kuishauri Serikali waanzishe authority kwa maana non tax revenue authority ili iweze kukusanya tozo hizi ambazo zimekuwa zikipotea. Mambo ya fees na mengine yanapotea huko na wafanyabiashara wetu wengi wanahangaika kuona kwamba wanafuatwa fuatwa sana na watu ambao ni wa tozo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ili tuwasaidie wafanyabiashara, ukifuatilia wafanyabiashara wengi ndani ya nchi yetu ya Tanzania wanaotaka kuanzisha biashara ndogondogo, wanafuatwa na watu wa tozo wengi wengi sana, mtu anaanzisha biashara, hajatulia anaingia mtu wa TBS, anaingia mtu wa NEMC, anaingia mtu wa OSHA, anaingia mtu wa Fire, anaingia mtu wa TFDA, mfanyabiashara huyo ambaye tunatamani awe bilionea kama Rais anavyotaka, atawezaje kama hatuwezi kuanzisha kitu ambacho ni kimoja, tuweza kuweka single point, huyu mtu akilipa kwa pamoja Serikali itafute jinsi gani inaweza ikagawana hayo mapato, siyo kufunga safari kwa kwa mfanyabiashara mmoja watu 20 kwenye Serikali ile ile. Naisihi na naiomba Serikali ianzishe Non Tax Revenue Authority ili tuweze ku-control hizi tozo ndogondogo ambazo zinapotea.

Mheshimiwa Naibu Spika, zaidi ya hapo niendelee kumpongeza Rais hata kwa wenzetu tulionao humu ndani ya Bunge, wa upande wa pili, ni kwa sababu Rais aliruhusu demokrasia kwenye nchi hii ndiyo maana na wao wapo. Ninachowasihi ni jambo moja, wawe watulivu, walikotoka wanalaumiwa na hapa wanatulaumu sisi, sasa hawajielewi walipo, wafanyiwe counseling tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)