Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza kabisa napenda nimshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema aliyeweza kunipa uhai leo nimesimama mbele ya Bunge lako Tukufu. Kipekee zaidi naomba niwashukuru wanawake wa Mkoa wa Mara walioweza kunichagua mimi kuwa mwakilishi wao katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikishukuru Chama changu Cha Mapinduzi kwa kuweza kuniteua mimi kuwa Mbunge. Pia nakushuru wewe kwa kunipa nafasi leo nimesimama kwa mara ya kwanza katika Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile naomba nimpongeze Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya Mwaka 2015 – 2020. Mheshimiwa Rais wetu mpendwa amefanya kazi kubwa sana katika nchi yetu. Kikubwa zaidi Mheshimiwa Rais wetu katika Mkoa wangu wa Mara amejikita kufanya mambo mengi makubwa sana ambayo yamesababisha nchi yetu imepiga hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nijikite katika suala la afya. Mheshimiwa Rais wetu wetu mpendwa katika Mkoa wangu wa Mara amefanya mambo makubwa katika Sekta ya Afya hasa upande wa hospitali, amejenga zahanati takriban 45 mpya, lakini pia vituo vya afya 13 vipya, amejenga hospitali za wilaya saba mpya. Kipekee kabisa Rais wetu ameweza kutupatia takriban zaidi ya bilioni 15 kuhakikisha tunajenga hospitali ya rufaa maarufu kwa jina la Kwangwa iliyokuwa imekaa zaidi ya miaka 40 sasa inafanya kazi katika kitengo cha mama na mtoto. Mheshimiwa Magufuli apewe sifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa basi naomba niende kuchangia katika hotuba aliyoitoa ya ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili. Mheshimiwa Rais wetu aliongea hotuba ambayo ilisababisha sisi kutupa dira, maono na mikakati mikubwa ya mstakabali wa Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba Mheshimiwa Rais wetu kwa hotuba hii ambayo Rais aliitoa imegusa kila eneo la Taifa hili ambayo naomba nielekee katika kundi la wanawake, lipewe fursa kubwa kwenye taasisi za kifedha kama mabenki. Nina Imani ili akinamama hao ambao wamekuwa ni sehemu kubwa mama zetu hawa ambao wamekuwa ni sehemu kubwa katika kulijenga Taifa letu waweze kupata fursa kubwa katika kupunguziwa masharti ya kupewa mikopo ya nafuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa uhakika nilionao niwaombe masuala ya kuhakikisha wanawake wanapata fursa ya kukopeshwa, naamini watakaoweza kukopeshwa wataweza kuonekana katika ujenzi wa Taifa hasa katika suala la Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, najua mama zangu wana changamoto kubwa hasa katika masuala ya kiafya. Nijikite kwenye kusema kwamba masuala ya tatizo la kiafya hasa ugonjwa wa akinamama wa kansa ya matiti na ya kizazi, hawa akinamama wanapata tabu sana hapo bada ya kuwa wanakosa huduma pale ambapo Madaktari wanakuwa hawapo pale. Sasa naomba niishauri Serikali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa, kengele imeshagonga.

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)