Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, na mimi naomba nichangie hotuba ya Mheshimiwa Rais zote mbili, lakini pia naomba nichukue nafasi hii kwanza niwashukuru wananchi wa Jimbo la Kigoma Kusini kwa kunileta Bungeni kwa kura nyingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi naomba niseme na niungane na wananchi wengine ambao wanasema kwamba Rais Magufuli ni chaguo la Mungu na ni kweli Rais Magufuli ni chaguo la Mungu. (Makofi)

Mimi kwenye Jimbo langu eneo kubwa ni eneo la maji, lakini Mheshimiwa Rais amekubali kukarabati meli ya Mv Liemba. Hivi sasa imeanza kukarabatiwa, lakini Mheshimiwa Rais siyo hivyo tu amekubali kutengeneza meli mbili moja itabeba watu na mizigo yao, lakini moja itabeba mizigo peke yake. Jimbo langu ni wahanga wa usafiri wa maji kwa maana hiyo wanatumia usafiri wa mitungwi ambayo inatumia mbao, kwa maana hiyo kumekuwa na ajali nyingi sana, lakini meli hizi zikitengenezwa zikikamilika tutakuwa wananchi wa Kigoma Kusini tumepata ufumbuzi na watu watasafiri kwa raha mstarehe kwa maana kutakuwa hakuna ajali lakini pia watasafirisha mizigo yao vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wakati anapita jimboni kunadi sera za Chama cha Mapinduzi kuomba kura na kuniombea kura mimi alikubali kuongeza zahanati, kuongeza Hospitali ya Wilaya nyingine kwa maana Jimbo langu ni kubwa sana katika majimbo ya Mkoa wa Kigoma, alikubali kuongeza hospitali nyingine ya Wilaya maana yake mimi nakwenda kuwa na hospitali mbili za Wilaya ni jambo la kumshukuru sana Mheshimiwa Rais katika jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie katika habari ya uvuvi. Katika jimbo langu wananchi wanajishughulisha na uvuvi, namshukuru Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi aliweza kuwasikiliza wananchi wangu waliotoka jimboni kuja kuzungumzia malalamiko ya suala zima ya kanuni zilizokuwa siyo rafiki na wao na Mheshimiwa Waziri alionesha kabisa kusikitishwa kwa nini hizo kanuni ziliwekwa vile, kwa hiyo, nina imani Mheshimiwa Gekul ambaye ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi hili jambo anakwenda kulitatua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili jambo litakwenda kuleta uchumi mzuri katika Jimbo la Kigoma Kusini kwa maana ya uvuvi, lakini pia Mheshimiwa jimbo langu wananchi wanajishughulisha na kilimo cha mpunga pamoja na mahindi na mihogo. Lakini ipo changamoto moja ambayo kwa kweli naomba Serikali iweze kusaidia, ni wanyama kwa maana ya mamba katika majaruba yale ya mpunga kwa mfano Kyala yaani watu wanakufa kwa sababu ya mamba ni wengi sana, tumejaribu kuwaambia watu wa mifugo wajaribu kupunguza wale mamba yaani mamba wale wana uwezo wa kuchukua binadamu yaani mmoja kwa kila siku, sasa fikiria kwa mwaka mzima ni watu wangapi.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naomba niunge mkono hoja kwenye hotuba hii ya Mheshimiwa Rais. (Makofi)