Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii kwa ajili ya kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kunipatia nafasi hii ya Bunge ni nafasi adimu, mimi ninaisema ni kwa neema yake Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Pia nakishukuru Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Lindi na kutokana na juhudi na kazi zilizoonekana za Dkt. John Pombe Magufuli zimetia imani kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi hata mwaka jana tumepata majimbo yote kwa Chama cha Mapinduzi ukilinganisha na mwaka 2015. Pia nashukuru familia yangu na rafiki zetu wote kwa support walionipatia kwa muda wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika napenda kuchangia kwa muda mchache huu hotuba ya Mheshimiwa Rais kwenye ukurasa wa 32, 33 na 34 kwa maeneo ya sekta ya afya, maji na elimu. Napongeza kwa kazi zote alizofanya na ndiyo maana zimeandikiwa kwenye taarifa hii na pia hata kwenye Ilani ya Uchaguzi kwamba nini tutaenda kufanya kwa miaka hii mitano mpaka mwaka 2025.

Mheshimiwa Spika, sekta ya afya kwa mafanikio ni makubwa, mimi mwenyewe nina uzoefu mkubwa kwenye sekta ya afya ndio nilipokulia mpaka sasa hivi, kwa sababu zaidi ya miaka 30 nimeendelea kuudumu huko kama mwalimu muuguzi, na mkunga kwa hiyo, ninauzoefu mkubwa sana na maendeleo yaliyotokea na mafanikio yaliyotokea kwakweli ni makubwa sana huwa ninamwangalia Dkt. Johh Pombe Magufuli huyu ni daktari, huyu ni muuguzi ama yaani ana kila kila sifa, lakini nikiangalia kumbe ni sababu wa utegemezi wake kwa Mungu aliye hai. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini napenda kuchangia kwa machache tu katika huduma za afya, pamoja na mafanikio yote hayo lakini kuongezwe ajira za wafanyakazi wa Wizara ya Afya ama idara hiyo ya afya ili tupate skilled personnel.

Mheshimiwa Spika, kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu ukiwa na wafanyakazi wa kutosha hata huyu mama nikitolea mfano mama mjamzito au mama anayekuja kujifungua au mtoto anayekuja kupata huduma pale watakuwa na muda mfupi wa kukaa pale kwa huduma kama ni huduma za kutwa ama hata za kulazwa hospitali lakini kutakuwa na muda mzuri wa hudumu hawa kuwaudumia hawa wagonjwa na pia hata stress za wafanyakazi zitapungua, kwa sababu wafanyakazi wako wengi na hata huduma atakayopata yule mgonjwa ama mama yeyote basi itakuwa ni nzuri.

Mheshimiwa Spika, lakini pia katika eneo hilo hilo afya mimi kama Mbunge kwenye mkoa wangu au popote nitakaopita na utaalamu wangu nitaendelea kuwahamasisha akinamama wajawazito na watoto hata na jamii kwa ujumla waende kupata huduma za hospitali.

Mheshimiwa Spika, lakini pia napenda kuchangia kwenye sekta ya afya mafanikio mengi yamepatikana lakini tumeona changamoto hata Mheshimiwa Rais aliiona wakati wa kampeni kwamba maji bado vijijini. Kwa hiyo hata vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Lindi vile vijiji vingine bado havijapata maji, nikiangalia yule mama mjamzito bado anaenda kuhangaika kutafuta maji bado anaangaika ili na lile kuangalia familia hivyo basi ni tatizo tunaomba maji, mwanamke huyu tumtue maji angalau hata anapokuwa mjamzito asihangaike kutafuta maji, akihangaika huku na kule bado hata uzazi wake hautakuwa salama.

Mheshimiwa Spika, pia nachangia kwenye sekta ya elimu kwa haraka haraka, nashukuru kwa elimu bila malipo hata mwanafunzi hata mtoto wa Mkoa wa Lindi anapata elimu na hata Tanzania nzima kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne. Lakini katika hili ninashukuru pia kwa kuzingatia masomo ya sayansi. Kwa uzoefu wangu wa vyuo vya afya mara nyingi tunakosa wanafunzi wazuri kwa sababu hawakufaulu sayansi kwa hiyo hilo nalo nalipongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia katika elimu tunaomba elimu ya juu kwa Mkoa wa Lindi hakuna Chuo Kikuu kwa hiyo naomba kuwe na compass ya Chuo Kikuu Mkoa wa Lindi ili nako tupate elimu ya hali ya juu ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)