Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Aloyce Andrew Kwezi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ALOYCE A. KWEZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi naomba nianze kwa kuwashukuru sana wananchi wangu wa Jimbo la Kaliua lakini pili naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais na Chama changu Chama cha Mapinduzi na tatu nishukuru familia yangu kwa kusimama na mimi katika kipindi chote cha uchaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesimama hapa ili niweze kuishukuru sana Serikali kwa michango mizuri ambayo imeweza kutusaidia. Suala la kwanza ni kama alivyotoka kuliongelea Mbunge mwenzangu hususani maji. Tabora tumepata Mradi wa Ziwa Victoria wa shilingi bilioni 617 na tunaamini kabisa kuanzia mwezi wa Tano tunatarajia kabisa maji yale yataelekea katika jimbo la Kaliua, Sikonge na maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, kwa fadhila hizo tunaishukuru sana Serikali kwa upendo wa wananchi hususani kuwatua akinamama ndoo kichwani, naomba nichukue nafasi hii kushukuru kwamba Hospitali ya Wilaya ya Kaliua kwetu tulikuwa hatujakamilika, lakini hivi karibuni tumepokea zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya kukamilisha Hospitali ya Wilaya ya Kaliua. Lakini tumepokea fedha za madarasa tumepokea, fedha za maabara na tumepokea fedha za ukumbi kwa Mkurugenzi, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais, na nishukuru watendaji wote wa upendo kwa niaba ya wananchi wote ambao tunaendelea kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi ningependa kuboresha sehemu ambayo Wabunge wenzangu wamechangia wengi wamechangia hususani suala nzima la barabara. Barabara naona changamoto kubwa kwanza ni kubadilisha ceiling ya TARURA lazima fedha ziongezwe TARURA ili wananchi waweze kunufaika na barabara za vijijini. Hivi tunavyoongea, zipo kata mpaka sasa hivi hazifikiki kata kama Usinge kwenye jimbo langu barabara imekatika, kata kama Useni kilometa 60 barabara imekatika kwa kweli hiki kitu kinatuumiza sana na mimi nilikuwa najiuliza kwa sababu nilikuwa Mtendaji kipindi cha nyuma, hivi zile fedha za emergence ziko wapi siku hizi? Mimi ninajua ni Mfuko wa Dharura inapotokea dharula basi una-take cover muda ule ule, barabara inakatika kata zaidi ya watu 60,000 inaachwa Mfuko wa Dharura tunakwenda kwa stahili gani hii.

Mheshimiwa Spika, emergence fund iwe kwenye level ya mkoa ili taarifa zinapofika ndani ya wiki moja basi tunapotoa taarifa kwamba kuna barabara imekatika kule wananchi wasibaki kisiwani, kwa hiyo nilikuwa nashauri hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lapilli ningelipenda kushauri ni suala nzima la afya. Sisi wote tuko hapa kwa sababu mama zetu walijifungua vizuri ndiyo maana tumefikia level hii na ninaipongeza kwa kuanza vituo vya afya vile 487 ambavyo tumeanza navyo. Mimi nina uzoefu kidogo kwenye sekta hii, operation kwenye kituo cha afya kimoja natoa mfano wa Kilolo kilikuwa kinaitwa Kidabaga, ndani ya miezi mitatu mama zangu waliokuwa wanajifungua walifanyiwa operation akinamama 158; sasa nilikuwa najiuliza hivi kwa kweli tunashindwa kwenda kama tumeweza kwenye kata, kama tumeweza kujenga shule za kata, ni kwa nini tusiongeze nguvu zaidi kwenye vituo vya afya ili kila kata iwe na kituo cha afya? Kwa sababu ajali nyingi za bodaboda zinatokea, operation zingeweza kutusaidia x-ray zinakuwepo pale kwenye kituo cha afya, lakini akinamama wanaojifungua ndiyo naona ni shida kubwa sana kutoka Makao Makuu ya Wilaya mpaka ukafike kijiji cha mwisho kilometa 250 kituo hakipo. Ni lazima tuangalie hiki kitu na tukipe kipaumbele cha pekee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la tatu ambalo mimi ningeweza kushauri Serikali nilikuwa naishauri Serikali kuhusiana na suala zima la hifadhi, nakushukuru sana Waziri Mkuu Mungu akubariki sana ulipotoa ufafanuzi kuhusiana na mipaka ni kweli kabisa ni changamoto na ningeshauri pamoja na Waziri wa Maliasili, lakini ashirikishwe Waziri wa Ardhi kwa sababu unaweza ukakuta unasema mpaka huu hapa, wananchi wanasema mpaka wetu unahishia hapa siku zote, professionally watu wa ardhi watuambie kwamba huu mpaka unapita eneo fulani kwa kweli kumekuwa na changamoto sana hususani Kaliua kwenye suala nzima la hifadhi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niseme naunga mkono hoja nashukuru sana. (Makofi)