Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona na kwa kunipatia nafasi hii ya kuchangia. Napenda kumshukuru Mungu sana kwasababu ni mara yngu ya kwanza kuwa katika Bunge hili na kuchangia hotuba ya Rais. Hotuba ya Rais hii nimeipitia yote na ni hotuba yenye maono mazuri sana, yenye mwelekeo mzuri, iliyosheheni kila aina ya maendeleo ambao wananchi wowote wangehitaji kuwa nayo katika nchi yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli amejipambanua katika Afrika kuwa Rais ambaye ni wa peke sana, vyombo vya habari vimekuwa vikimsema sana kwa muda mfupi na haijawahi kutokea kwa Rais kama yeye kusemwa na nchi mbalimbali. Hiyo ni dalili tosha kwamba ameleta mabadiliko ya kutosha na tumeona katika miaka hii mitano akiwa anashughulikia nyanja mbalimbali japokuwa yeye kama alivyokwisha kusema mtu mmoja ni msomi katika eneo moja. Lakini amekuwa mtaalam katika maeneo yote karibu ya nchi yetu hii. Kwa hiyo, pongezi nyingi sana nazitoa kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile kwa safari hii pia napenda kumshukuru sana kwa sababu ukiangalia hata baraza lake la Mawaziri wengi tulitegemea, wakati bahasha inaletwa Waziri Mkuu nilijua atarudi yuleyule. Kwa sababu kwa kazi aliyoifanya Mheshimiwa Kassim Majaliwa nilitegemea tu angerudi, na wengine nilijua watarudi na wamerudi kweli. Kwa hiyo, ninamuona kabisa kwamba Rais amewaamini na hata wale ambao wengine wamefanya kazi pamoja naye amewaamini sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nichangie suala la elimu. Elimu imetolewa sasa ni bure kuanzia darasa la kwanza mpaka form four na hii imesaidia sana katika kupunguza mambo mengi. Kwa mfano tulikuwa na wasichana wengi waliokuwa wanamaliza darasa la saba, uwezo wa wazazi wao ulikuwa ni wa chini ndio walikuwa wanategemewa kuwa ma-house girl katika sehemu mbalimbali na kwa kweli hawa walikuwa wananyanyasika sana, ma-house girl wengine walikuwa wanapata mishahara midogo na mwisho walikuwa wanaishia tu katika kuhangaika, lakini sasa hivi katika umri huo wa utoto wengi watakuwa shule, kwa hiyo, hayo ni mafanikio makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, vilevile hata upatikanaji wa mimba kwa watoto wa kike utashuka sana kwa sababu umri huo wa watoto wa chini ya miaka 18 watakuwa mashuleni, kwa hiyo, hii elimu bure itakuwa na faida kubwa sana. Lakini vilevile hata vijana wa kiume ambao wengi walikuwa wanajiingiza katika makundi makundi ya kuwa wezi na wadokozi, sasa nao watakuwa shule, kwa hiyo, baadae watakuwa wakubwa na watakuwa ni wa kuwajielewa.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni katika upande wa afya, afya pia imeamirika sana kulikuwa kuna changamoto sana ya wananchi hasa ya kinamama kuogopa kwenda hospitali na kwenda kwa waganga wa kienyeji kwenda kupata tiba huko kwa sababu walikuwa wakifika hospitalini walikuwa wanapata changamoto. Lakini kutokana na Chama cha Mapinduzi ambacho kimeongeza hospitali nyingi hadi kufikia katika vijiji sasa imebaki kazi moja kuwahamasisha wananchi wote kuzitumia hizi huduma afya na kubadilisha mtizamo ule wa kuamini maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, changamoto ambayo pia ninaweza labda nikaiona je, Serikali sasa iweze kujikita katika kuwasaidia wananchi katika kubadilisha mtazamo, kubadilisha mtazamo ni jambo ambalo ni gumu kitu mtu anachokiamini tangu amezaliwa ni ngumu hospitali inaweza ikawepo, dawa zikawepo, wahudumu wakawepo lakini bado mtu asiende kule kwa sababu zake binafsi labda alihaminishwa kwamba hospitali sio sehemu sahihi ya kwenda ukienda kwa mtu fulani ndiyo atakayekuhudumia au hasa katika wazazi unakuta mama mjamzito haendi kwenda kujifungua hospitalini au anakwenda hospitalini baada ya hatua imeshafikia mbaya na mwisho wake ndio vile vifo vichache ambavyo tunavisema wakati ambapo huyu mama kama angeweza kwenda mapema angeweza kupata huduma ambayo ni sahihi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, sasa ni kazi yetu sisi kuweza kuhamasisha wananchi wetu kuanzia chini kabisa kubadili tabia zao ili kuweza kuepuka magonjwa yale ambayo yanaweza kuzuilika na kuzitumia huduma zetu za afya ili waweze kupata afya njema na kuweza kupona magonjwa ambayo yanazuilika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuchangia. (Makofi)