Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Rose Vicent Busiga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ni kwa mara yangu ya kwanza kuchangia kwenye Bunge lako tukufu. Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyeniwezesha kuingia kwenye Bunge hili tukufu, ni kwa mara yangu ya kwanza na ninamshukuru Mungu na nawashukuru pia na watumishi wa Mungu walikesha kuomba usiku na mchana ili mimi niweze kuingia kwenye Bunge tukufu hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru baba yangu mzazi na familia yangu nzima na mume wangu kwa kunipa ruhusa hii kuja kutumikia Bunge hili tukufu maana si kawaida kwa wanaume kumruhusu mwanamke kuja kwenye Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zaidi ya yote…

SPIKA: Jamani mmesikia Waheshimiwa karuhusiwa huyo. Makofi/Kicheko)

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Spika, nina furaha kubwa sana na nilikuwa natamani nipate nafasi hii ikiwezekana naomba uniongeze dakika mbili tu kwa ajili ya kusema haya. Napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kwa kuongoza vizuri Chama chetu cha Mapinduzi kwa kuipatia heshima kubwa iliyotukuka katika Tanzania hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Rais huyu niwa kuigwa, hajawahitokea toka Tanzania iumbwe, napenda kulisema mbele ya Bunge lako tukufu hili 2015 mara tu baada ya Rais ya Jamhuri ya Muungano kupata nafasi ya kuwa Rais ninaamini kabisa kwa watu ambao wanamtegemea Mungu, Rais huyu aliamua kuichukua Tanzania na kumkabidhi Mungu aliye hai na ndio maana watu wengine wanaweza wakasema uchaguzi ulikuwa hauna haki, lakini kwa mtu ambaye anamtegemea Mungu, Rais aliamua kuichukua Tanzania na kuipeleka kwa Mungu kwa malengo tu, ukimtumikia Mungu utapata hekima, utakuwa na maarifa, utakuwa na busara. Ndio maana leo hii Tanzania sisi ni matajiri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kuunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais nikiamini hata yaliyobakia kwa miaka mitano hii yote yanakwenda kukamilika. Jamani naomba nizungumze hili mwaka 2020 ninaamini kabisa Watendaji wa Kata nchi nzima na mimi nikiwemo niliingia kule Ikulu kwa mara yangu ya kwanza na Bunge hili mimi ni Mtendaji wa Kata na kila Mheshimiwa Mbunge namwambia mimi ni Mtendaji wa Kata najivuna kwa kazi niliyokuwa nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, asingekuwa huyu Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli wa wanyonge, mimi ningeingia humu? Jamani lazima tujiulize, na ndio maana jina langu lilipita kwa kila Kamati jina langu lilikuwemo mimi mnyonge na leo hii naunga mkono kwa asilimia mia moja miaka iliyobakia yote ambayo hatujafanikiwa Rais kuyafikia yote yatafika na zaidi nasema nawaunga mkono Mawaziri, baba yangu hapo Waziri Mkuu usiogope, Mungu amekuteua wewe, lakini pia na Mawaziri wote na Naibu Mawaziri wote chapeni kazi mtangulizeni Mungu mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Tanzania tumejaliwa kuwa na Rais simba, akiunguruma baba watu ameunguruma na mimi naidhihirisha Tanzania nitamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano asilimia mia moja, na sitaona haya kusema mazuri yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndio maana nikakwambia naomba dakika mbili ninayo mazuri mengi, ,una daraja la Busisi kule Geita.

SPIKA: Mheshimiwa Rose ngoja, hebu ongezeni dakika mbili hapo. (Kicheko/Makofi)

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa tulivyoenda kule Ikulu, nilipofika Dar es Salaam, nikajua ni Dar es Salaam ya sasa ni kama Marekani kumbe ni Tanzania. Mheshimiwa Rais kwa upendeleo kabisa akatupa na pocket money tukatembee tembee, nani kama Dkt. Magufuli jamani?

WABUNGE FULANI: Hakuna!

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Spika, nazungumza haya kutoka kwenye vilindi vya moyo, nataka niwaambie watanzania mnaweza mkasema wakati tunatafuta kura za Chama cha Mapinduzi, kwa wanawake wa Geita, kwanza ninawashukuru sana wapiga kura wangu wanawake wa Mkoa wa Geita kwa kuniamini kama Mbunge wao na sitawaangusha, wanawake wote yaani ukishataja tu tunaomba kura za Mheshimiwa Rais tulikuwa tunapita wote na Wabunge, na ndio maana hakuna kura iliyoibiwa, hakuna kura iliyoibiwa kwa Tanzania nzima. (Makofi)

Mheshismiwa Spika, jamani tunaangalia kule Mwanza, daraja la Busisi, tunategemea sisi Wasukuma tutakuwa tunapita pale huku tuna baskeli tumepakiza tunakula na muwa, ilikuwa haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja na nitazidi kuongea kwa kumuunga mkono amefanya mengi, anatupenda Watanzania naombeni tumuelewe, naombeni tumtie moyo pamoja na Serikali yake na Waziri. Ahsante sana. (Makofi)