Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, kwanza na mimi nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenijaalia kuwa sehemu ya Bunge hili la Kumi na Mbili. Lakini pia nichukue fursa hii kuwashukuru wananchi wa Biharamulo walioniamini na kunichagua kwa kura nyingi za kishindo niwe muwakilishi wao katika Bunge hili, lakini bila kumsahau mke wangu mpenzi Engineer Ebzenia kwa support kubwa ambayo amenipa na watoto wangu wawili Isack na Ebenezer. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa haraka haraka mimi ningependa kuchangia kwa sababu ya muda nimekuwa katika viwanda kwa muda mrefu kidogo takriban miaka 14 nimekuwa nafanyakazi katika viwanda kama engineer, kwa hiyo ningependa nijikite hapa zaidi. Nimejaribu kuangalia tumetengeneza ajira takribani 480,000 katika viwanda 8,447 ambavyo tumevizalisha katika muda huu wa miaka mitano. Sasa nikijaribu kuangalia average ni sawasawa na kila kiwanda kimetengeneza ajira 56, sasa najaribu kuangalia tuna-target ya kutengeneza ajira milioni nane na tukisikiliza au kupitia hotuba ya Rais aliyoitoa hapa focus kubwa tuna target kuangalia integration ya mazao ya kilimo yaweze ku- integrate na viwanda ili tuone sasa mambo ambayo tunayachakata hapa katika kilimo, mifugo na uvuvi ambao umeajiri Watanzania wengi ndiyo viweze kuwa vyanzo vikubwa vya ku-integrate ajira hizi katika viwanda.

Sasa nilikuwa najaribu kupiga hesabu let’s say tunataka ku-create ajira milioni mbili tu kutoka katika viwanda maana yake tunahitaji tutengeneze viwanda takribani 33,000 tukienda na mwendo huu viwanda vile vya kawaida. Sasa ninachojaribu kukichangia hapa ni nini au maoni yangu ambayo ninayo ni nini? Tujaribu kujikita zaidi katika kuwezesha watu wenye viwanda ambao wanaviwanda tayari.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano Breweries wana-import ngano hapa na tumeangalia hotuba ya Rais inasema tunaingiza ngano takriban tani 800,000 kwa mwaka. Sasa tukiongea na Breweries tukajipanga tukawapa mashamba wao kwanza wawe ndiyo watu wa kwanza wa kulima kama wanavyofanya watu wa miwa na watu wengine yeye mwenyewe azalishe raw material kwa ajili ya ku-feed viwanda vyake huyo atatutengenezea ajira, ataajiri vijana wetu ambao wanasoma katika vyuo kwa mfano SUA na sehemu nyingine hiyo tu ni ajira tosha kwanza itazuia importation ya ngano, lakini vilevile itatengeneza ajira kwaajili ya vijana.

Mimi nimekuwa katika viwanda vya sukari nimekuwa naona kwa mfano kiwanda kimoja unakuta kimeajiri takribani Watanzania 10,000 wanaofanyakazi katika kiwanda cha Kagera au Mtibwa, ni watu wengi sana hawa ambao wamekuwa wameajiriwa huko. Kwa hiyo nikawa nasema same applies kwenye alizeti, niko katika Kamati ya Viwanda na Biashara, Mheshimiwa Waziri uliongelea suala la Kiwanda cha Singida kwamba kina-operate katika 35% of installed capacity sasa kiwanda ambacho kinafanyakazi katika 35% of installed capacity, kama tungekiwezesha kwanza kiwanda chenyewe tukakipa eneo la kulima kama kiwanda, kikalima alizeti yake yenyewe maana yake kiwanda kile kingeajiri Watanzania katika mashamba yake ya alizeti watu wengine pia wangeweza kulima na kuuza katika kiwanda kile maana yake kiwanda tungeweza ku-boost production yake ikapanda zaidi kwa sababu raw material ipo na kiwanda hakifanyi kazi katika installed capacity kwa sababu malighafi ya ku-supply katika kiwanda kile huenda ina scarcity yake pia. Same applies kwenye sehemu kama za kwetu…

SPIKA: Engineer Ezra mbegu ya alizeti hakuna, mbegu ya alizeti iko wapi? Endelea tu.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, najua mbegu ya alizeti hakuna ndiyo tunapohitaji sasa Wizara ya Kilimo ijikite katika hili kwa sababu kama tunategemea ajira ya Watanzania wengi iko katika kilimo tukasema mbegu ya alizeti hamna, halikadhalika tutasema na mbegu ya michikichi Kigoma hamna na bado tunaagiza mafuta it’s a shame kwa nchi kama hii juzi meli ya mafuta inakuja hapa Waziri anashangilia anasema meli ya mafuta imekuja hapa wakati wale watu kule bado tunaweza tukaongea nao hata wao wenyewe wanachokifanya kule tukaweza kuki-copy hapa tulete wawekezaji kule wanaozalisha mafuta ya mchikichi tuwaleta Kigoma pale, tuwaambie na sisi tuna michikichi hapa hebu waweke kiwanda Kigoma halafu tuwahimize watu wao wenyewe wenye kiwanda kwanza watalima mashamba yao, wataajiri jirani zangu wa Kigoma, halikadhalika walio na mashamba ya michikichi pale wataweza kuuza kwenye kiwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata mimi nina maeneo makubwa, Biharamulo tuna mapori ambayo yamekuwa yanateka Watanzania wanaumia kwa muda mrefu tunaweza kulima alizeti pale au tukaweka mwekezaji akalima alizeti ndugu zangu wa Biharamulo pale wakaweza kuajiriwa. (Makofi)

Lakini ajira tunapoipata ile maana yake tunabeba wakulima watu wa chini kabisa ambao wanashida ni wakulima hata mimi mtu atalima heka moja, atalima heka mbili, kwa sababu anajua kiwanda kiko pale ataweza kuuza kwenye kiwanda.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, naona muda hautoshi naomba kuunga hoja 100% nadhani nitaongea kwenye mipango pia. (Makofi)