Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. JANEJELLY J. NTALE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa jicho lako kuniona, kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ameniwezesha kuwa mmojawapo wa Bunge la Kumi na Mbili. Lakini niwashukuru wakinamama wa UWT Mkoa wa Dar es Salaam na Baraza Kuu la UWT Taifa na wajumbe wengine wako humu ndani ya Bunge kwa kuniamini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nishukuru Chama cha Mapinduzi kwa sababu ndiyo chama pekee kinatupa nafasi watumishi wa Serikali ndani ya Bunge hili, ahsanteni sana. Lakini nimesoma risala zote mbili, Mheshimiwa Rais anaongelea maboresho ya watumishi na maslahi ya watumishi, tunashukuru sana alivyohamishia Serikali Dodoma ametekeleza kilio cha watumishi wa Serikali na vyama vyao ambavyo tulikuwa kila siku tukishauri hilo, tunamshukuru sana.

Lakini tumshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye alisimamia zoezi hilo aliposema kila mtumishi kuondoka Dar es Salaam ahakikishe akaunti yake imesoma, tunakushukuru sana. Lakini tunampongeza Rais kwa jinsi alivyojenga mji wa Kiserikali Mtumba, mji huo umeleta mahusiano kazini kwa kufanya Wizara kati ya mtumishi na mtumishi kufahamiana.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais kwenye risala yake anasema ataboresha maslahi ya watumishi, lakini niombe kushauri ili maslahi ya watumishi yaboreshwe turudi kwanza tuangalie sheria za kiutumishi, kuna baadhi ya sheria yatafanya zoezi hili liwe gumu. Kuna sheria moja inaitwa sheria ya re-categorization…

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Ntale ukae chini upokee taarifa, Mheshimiwa Esther Matiko.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, ahsante sababu ya muda nitaenda kwa kifupi sana.

Mheshimiwa Ntale ningependa kukupa taarifa kwamba umesema Chama cha Mapinduzi ndiyo cha pekee kutoa fursa kwa watumishi wa umma, ujue kwamba tulikuwa tuna Mbunge anaitwa Dkt. Sware Semesi alikuwa ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu, alikuwa ni Mbunge wa CHADEMA, alikuwepo mama Lyimo alikuwa ni Chancellor wa Chuo Kikuu pale alikuwa ni Mbunge wa CHADEMA, mimi peke yangu nilikuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni Mbunge, kwa hiyo usipotoshe, na wengine wengi.

SPIKA: Mheshimiwa Janejerry James Ntale unaipokea hiyo taarifa?

MHE. JANEJELLY J. NTALE: Mheshimiwa Spika, naomba nisiipokee hiyo taarifa kwenye Chama cha Mapinduzi kimetenga nafasi mbili kabisa kwamba ni nafasi za watumishi wa Serikali kutoka kwenye vyama vya wafanyakazi na humu ndani tuko wawili mimi na Dkt. Alice, sipokei hiyo taarifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naongelea sheria ya re- categorization. Sheria hii kama haijaumiza mtumishi yeyote aliyehumu itakuwa imeumiza mtoto wako au mpiga kura, ile sheria mtumishi akijiendeleza, akiomba kufanyiwa re- categorization anashushwa mshahara na kwenda kuanzia kwenye cheo kile cha wale wengine waliopo.

Mheshimiwa Spika, binafsi sisi hatupingi mtu kwenda kuanzia pale wanapoanzia wataalam wale, lakini aachwe na mshahara wake. Kwa sababu nimefanyakazi Wizara ya Fedha kila mtumishi ana budget line yake ya mshahara huyu mtumishi hakuna anapoongeza bajeti, mshahara wake unakuwa ni ule ule, alichobadilisha ni kada, niombe hiyo sheria, Menejimenti ya Utumishi wa Umma mkaiangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Jenista ni shahidi tumekuwa tukikulilia kilio hiki cha sheria hiyo inaumiza sana watumishi. Lakini kuna na miundo ambayo siyo rafiki tena kwa watumishi, leo hii Mheshimiwa Rais tunamshukuru ameunda Wizara ya TEHAMA.

Lakini kwenye muundo wa ma-executive assistant ambao ndiyo wasaidizi wenu bado wamekamatwa na hati mkato.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. JANEJELLY J. NTALE: Mheshimiwa Spika, naona muda umeniiishia lakini nitalileta kama swali naomba kuunga hoja mkono. (Makofi)