Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, na mimi niungane na wenzangu wote kukupongeza na kukushukuru kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia. Ni Mara yangu ya kwanza kusimama katika Bunge hili tukufu. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Malima tumefurahi kwa sababu kiti ulichokikalia ndio kilekile cha Mpwapwa. (Makofi/Kicheko)

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, nilipoambiwa asubuhi nilifurahi sana. Nimeambiwa kiti hiki Senetor alikuwa analia sana kwa ajili ya barabara, barabara ya kutoka Kongwa kwenda Mpwapwa na mimi leo nimesimama mbele ya Bunge lako kushukuru sana kwa ajili ya nafasi hii, lakini pia nishukuru Chama changu cha Mapinduzi ambacho kilinipa ridhaa ya kugombea na nilishinda kwa kishindo, lakini pia nimshukuru Mheshimiwa Rais. Kusema kweli hotuba yake ndio imebeba mustakabali wa Taifa letu. Ni wajibu wetu sisi kama Wabunge, mawaziri tumasaidie Rais kutafsiri maono yake katika njia ya utekelezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wenzangu wote wamesema habari ya TARURA na mimi ni muhanga wa TARURA. Kwenye jimbo langu la Mpwapwa barabara ni mbaya sana kwa sababu kwanza jiografia ya Mpwapwa ni eneo lenye vilima vingi, kwa hiyo, mvua zikinyesha maji yanaporomoka yanakata barabara, leo hali ya barabara za vijijini kule Mpwapwa ni mbaya sana na mimi nisiseme sana, ningependa tu kusema naomba sana bajeti ya TARURA iongezwe na niseme tu ifike hata asilimia 45 inaweza kusaidia kupunguza tatizo la barabara za vijijini.

Mheshimiwa Spika, lakini tatizo lingine kubwa ni la upande wa TANROADS. Barabara hii ya kutoka Kongwa kwenda Mpwapwa ni barabara yenye urefu mfupi sana, ni barabara yenye takribani kilometa 32, lakini barabara hii imedumaza sana uchumi wa Mji wa Mpwapwa na watu wake. Hakuna mtu angependa kwenda Mpwapwa leo kwa sababu ya ubaya wa barabara ile. Barabara hiyo Senator Lubeleje amelia sana miaka ya nyuma. Sasa naomba Serikali ifike wakati kilio chetu cha watu wa Mpwapwa kisikike ili barabara hii itengenezwe, ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi. Na mimi naamini Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi itasaidia barabara hii kujengwa.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ningependa kuzungumza ni wazo zuri la Mheshimiwa Rais kuamua kutoa elimu bure kwa watoto wetu wa kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne. Wazo hili ni jema sana, lakini wasiwasi wangu nimeona kwamba tusipomsaidia Rais sisi kama Serikali wazo hili mwisho wa siku tutakuwa na wanafunzi wengi wanamaliza shule darasa la saba na wengine wanamaliza kidato cha nne hawajui kusoma na kuandika kwa sababu idadi ya wanafunzi wanaoingia katika darasa la kwana na kidato cha kwanza haiendani na idadi ya walimu.

Mheshimiwa Spika, walimu hawatoshi kwa kipindi kifupi nilichokaa Jimboni nimegundua kuna upungufu mkubwa sana wa walimu karibu kila shule walimu hawatoshi naomba sana Wizara ya Elimu ijaribu kutafuta namna ya kuongeza walimu katika shule za msingi na shule za sekondari.

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo ningeweza kuzungumza ni juu ya umeme, nataka nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Nishati kwa kazi njema sana ambayo ameifanya kuleta umeme katika nchi hii. Lakini mimi naomba nimshauri Mheshimiwa Waziri ukiangalia, ukipita kwenye vijiji umeme umepita kwenye centers za vijiji haujapanuka nimesikia asubuhi kwamba mpango wa Serikali ni kujenga mpaka kwenye vitongoji kuweka umeme, basi wanapoenda kuweka umeme kabla ya vitongoji, lakini vile vijiji vikamilike ukienda kila kijiji bado kuna kilio watu wanataka umeme umepita katika eneo la center lakini maeneo mengine bado hayajafikiwa. Kwa sababu ya kazi nzuri ya Waziri naamini mpaka miaka mitano itakapofika kazi hii itakuwa imekamilika.

Mheshimiwa Spika, tatizo la maji ni tatizo ambalo pia katika Jimbo langu linaendelea na ni kubwa naomba sana Serikali ushauri wangu ni kwamba wakati mwingine tunataka kupata miradi mikubwa sana kwenye vijiji ya maji, lakini hebu nishauri badala ya kushauri miradi mikubwa ya kuweka network ya maji kwenye vijiji tuchimbe angalau kisima kimoja tu wakati tunasubiri upembuzi yakinifu, tunasubiri tathmini watu wawe wanakunywa maji hata kwenye kisima pale tu peke yake, halafu hayo mengine yatafuata kuweka networking na nini sasa hivi maeneo mengi hakuna maji vijijini watu wanaendelea ku-suffer na Mheshimiwa Rais amezungumza kwamba inapofika 2025 kila kijiji kitakuwa na maji.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga hoja 100%.