Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. FLATEY G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kusema jioni hii ya leo. Kwanza naomba nimshukuru Mungu kwa kutujalia na kutupatia uhai, lakini pia nikishukuru chama changu kwa kunichagua na kuniteua jina langu na kupigiwa kura na wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini. Niwashukuru sana kwa kunipa kura na kunileta humu ndani. Nikushukuru na wewe sasa kuwepo tena kwenye Bunge hili la Kumi na Mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika mchango wangu wa kuchangia hizi hotuba mbili za kufunga Bunge la Kumi na Moja na kufungua la Kumi na Mbili, ukiangalia sasa jinsi ambavyo Rais wetu anavyofanya kazi mimi namuombea Mungu ampatie afya njema, aendelee kumpa nguvu ili hizi ndoto ambazo amekuwa akizizungumza katika hotuba yake Mungu asaidie na sisi tumsaidie twende naye kufanya Tanzania ambayo sasa tumeingia kwenye uchumi wa kati, twende zaidi ili wananchi wetu waondokane na kero ambazo zipo katika maisha ya kawaida ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu dakika ni chache naomba niende kwenye upande huu wa kilimo. Ukiangalia ukurasa ule wa 27 kilimo chetu wananchi wanakitegemea sana, zaidi ya asilimia 75 wanategemea kilimo. Sasa naomba nishauri kwa sababu Wizara sasa ndio wana kazi ya kuhakikisha kwamba wanaangalia ile vision ya Mheshimiwa Rais wakati anaitoa hotuba hii. Ukiangalia leo mvua zinanyesha na mimi niishauri Wizara nayo iangalie iende katika kuwekeza kuzuia maji yanayotokana na mvua na kuchimba mabwawa, ili mabwawa yanapochimbwa basi itasaidia zaidi kufanya kilimo cha uhakika. Tukichimba mabwawa, tukaweka fedha na fedha hizi tukasaidia kuziwekeza katika mabwawa na maeneo mengi ya wafugaji na wakulima mabwawa haya yatatumika kwa mambo mawili, kwanza yatanywesha mifugo, lakini pili tutakuwa na kilimo cha uhakika wa kupata mazao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia Mheshimiwa Rais amezungumza sana na ameahidi kwamba, katika wakati huu atahakikisha pembejeo zinafika kwa haraka. Na pia, ukiangalia sasa kwa hali ya saa hizi tusipoweza kuishauri Serikali vizuri na mimi naomba niwashauri, ukiangalia leo hii bei ya mbegu katika maeneo yetu ni kubwa zaidi kuliko debe moja. Kwa mfano, kilo moja saa hizi au mbili katika mfuko mmoja ni shilingi 13,000/= mpaka shilingi 14,000/=. Debe unapokuwa umevuna mazao linakuwa na shilingi 6,000/=; kwa hiyo, basi mimi nishauri tuone namna gani pia ya kuanzisha mashamba ya mbegu humu nchini kuliko mbegu kutoka nje ya nchi kuja kuuzia huku. Kwa nini tusizalishe mbegu sisi tukawauzia wakulima? Na hili linawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini linguine kutokana na muda twende kwenye TARURA. Mimi nina kilometa 1,300 kwenye Jimbo la Mbulu Vijijini, tunapata shilingi milioni 696 haziwezi kutengeneza barabara hii. Sasa niombe wakati tunatunga sheria ya kuisaidia Serikali kutumia mfumo huu wa bei ya soko yaani force account, kwa kutumia miradi hii ya afya na miradi mingine ya kujenga majengo ya shule wataalam hawakukubali sana; mimi niombe Serikali ije na mpango, ione namna gani ya kusaidia hii TARURA maana tunaweza kuwa katika ukandarasi tunapigwa sana. Sasa ili kuona namna ya kusaidia Serikali hebu tujaribu twende kwenye force account pia kwenye TARURA naamini katika njia hiyo tunaweza kusaidika.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia barabara zetu nazo zimekuwa na halimmbaya sana, ni ngumu. Tuone namna gani mwaka 2016 tumezungumza Habari ya TARURA, mwaka 2017 tumezungumza hivyo, mwaka 2020 tumezungumza hivi hivi, tunaenda mwaka wa 2021 naomba sasa tufanye namna ya maamuzi makubwa tuamue ili TARURA ikafanye kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naona muda umeisha, basi kwa sababu, muda umeisha tutakutana kwenye mpango, niunge mkono hoja. (Makofi)