Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuchangia hotuba hii ya Mheshimiwa Rais. Kwanza kabisa kama utamaduni wetu Watanzania kushukuru na mimi naomba nishukuru kwa sababu ni mara yangu ya kwanza kusimama kwenye Bunge hili tukufu, naomba nikishukuru Chama changu cha Mapinduzi kikiongozwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, Mwenyekiti wa chama chetu, Wajumbe wa Kamati Kuu, lakini pia nawashukuru akinamama wa Mkoa wa Tanga kwa kunichagua kuwa mwakilishi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia naishukuru Kamati yangu ya Utekelezaji Mkoa wa Tanga na Taifa pamoja na familia yangu kwa kuni-support. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nichangie hotuba ya Mheshimiwa Rais kwenye kipengele cha elimu. Kutokana na muda sasa hivi ni mchache, dakika tano, nitakwenda moja kwa moja kwenye elimu, sitaweza kugusa vitu vyote na kwa kuwa mambo mengi yameshaongelewa na Waheshimiwa Wabunge wengi toka tumeanza mpaka leo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye suala la elimu, Serikali ya Chama chetu cha Mapinduzi ikiongozwa na Jemadari wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, tumefanikiwa kwa kiwango kikubwa; kutoa elimu bure ndani ya kipindi cha miaka mitano. Kuanzia 2016 mpaka leo tumetoa shilingi trilioni
1.01 ambayo imesababisha ongezeko la wanafunzi wa shule za msingi na sekondari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mbali na elimu bure, pia Rais John Pombe Magufuli chini ya uongozi wake ameongeza idadi ya madarasa katika shule za msingi kutoka madarasa 16,899 tuliyokuwa nayo hapo awali mpaka kufikia madarasa 17,804. Pia tumeongea shule za sekondari kutoka shule 4,708 mpaka shule 5,330. Pia tumekarabati shule kongwe na wengi tunaotoka huko mikoani ni mashahidi kati ya shule 89, shule 73 zimekarabatiwa na zimebaki shule 16 na ni Imani yangu kwa Serikali hii na kasi hii ya Awamu ya Tano tutakwenda kumalizia shule hizi 16 kwa kipindi hiki cha miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia mabweni 253 yamejengwa, kwa hiyo, ni mafanikio makubwa. Vyumba 227 vya maabara vimejengwa na maabara 2,956 zimepatiwa vifaa. Tumeona ongezeko la madawati la asilimia 200. Hayo ni mafanikio makubwa kwa Rais huyu mtetea wanyonge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, idadi ya wanafunzi nimesema kutoka 1,648,359 mpaka 2,185,037 kwa shule za sekondari. Kupitia kipengele hicho cha elimu na mafanikio hayo makubwa na kazi kubwa naomba nishauri kitu. Naomba nishauri upande wa mtaala. Tumeona mambo ni makubwa yaliyofanywa lakini kwenye kipengele cha mtaala iko haja ya ku-review mtaala wetu, malengo ya mtaala.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante nashukuru, naomba niunge mkono hoja kwa mafanikio hayo makubwa yaliyopatikana kwenye elimu na Wizara nyingine zote. Ahsante nashukuru. (Makofi)