Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nawashukuru wananchi wa Mafinga na kila mmoja ambaye kwa namna moja ama nyingine amefanikisha mimi kurejea hapa na mimi kama ulivyosisitiza suala la TARURA, tumelisema sana, ni wakati sasa kama walivyosema watu wengine, tuje na ubunifu wa kutafuta chanzo ambacho kitasaidia TARURA kupata fedha ya kutosha ili angalau watu tuwe na uhakika wa kurudi hapa mwaka 2025. Kwa sababu pale Mafinga bila kuwa na barabara za lami maana yake ni kwamba wakati huo ukifika bora nisiende. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikiunganisha na jambo hili, jana nilikuwa na swali nikiuliza Serikali, ni lini wataanza ujenzi wa barabara za lami? Majibu kutoka TAMISEMI ni kwamba Serikali iko katika hatua za mwisho za kuhakikisha kwamba ile miji 45 chini ya utaratibu wa uendelezaji miji, itakwenda kuanza kunufaika muda siyo mrefu ujao kwa sababu wako katika mazungumzo ya hatua za mwisho. Kwa hiyo, naisihi Serikali na kuiomba basi mazungumzo hayo yaende kwa haraka ili kusudi miji hiyo 45 ianze kunufaika na hivyo kupunguza mzigo kiasi fulani wa TARURA katika kuhudumia barabara zetu.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu mimi ni mwanamichezo, najielekeza moja kwa moja katika ukurasa wa 37 wa hotuba ya Mheshimiwa Rais ambaye wamesema, katika miaka mitano ijayo tutakuza sanaa, michezo na utamaduni.

Mheshimiwa Spika, sanaa, michezo na utamaduni imekuwa chanzo kikubwa cha mapato katika dunia ya sasa ambapo matumizi ya internet yamekuwa makubwa sana. Nina takwimu hapa, projection ya PWC inasema kwamba mwaka 2017 mapato yaliyotokana na media and entertainment industry katika Tanzania yalikuwa takribani dola milioni 496. Projection kufikia 2022 itakuwa bilioni 1.1 ambayo ni sawa trilioni 2.5. Kwa hiyo, hii ni sekta ambayo ni chanzo kikubwa cha mapato, lakini pia ni chanzo kikubwa cha kuchangia ajira, katika zile ajira milioni nane ambazo Mheshimiwa Rais amepanga tuzizalishe katika mwaka 2020 – 2025.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kuwapongeza TCRA, baada ya kuwa wamewafungia Wasafi Tv, sasa wamesema kwamba adhabu imepungua. Najielekeza katika COSOTA na BASATA. Mheshimiwa Rais alielekeza nami nimezungumza karibu miaka mitano, imekuwa sasa under one roof, lakini haitoshi. Ikiwa TCRA, NEMC wako mpaka level ya kanda, kwa nini BASATA na COSOTA wasirudi hadi level ya kanda kuwapunguzia wasanii safari na gharama za kusafiri mpaka Dar es Salaam?

Mheshimiwa Spika, tazama msanii atoke Kongwa, aende Dar es Salaam, anaingia gharama nyingi. Atoke Tandahimba, Ilemela au Mafinga, kwa hiyo, ushauri wangu ni kwamba kama hii ni sekta ambayo inazalisha mapato ya kiasi cha shilingi trilioni 2.2 na ni chanzo cha ajira, ukiangalia hapa matamasha mbalimbali ambayo huwa yanafanywa hapa nchini kwetu, yamekuwa ni chanzo kikubwa cha ajira.

Mheshimiwa Spika, nitatoa mfano, nawapongeza Wizara ya Habari, wana tamasha hili la Serengeti Festival, ukienda pale Jamhuri kuanzia mama ntilie, muuza mahindi, muuza Big G atapata pesa. Matamasha mbalimbali kama muziki mnene EFM, kama tamasha la Tunawasha la Wasafi, matamasha kama Fiesta la Clouds, mtikisiko la Redio Ebony kule Iringa, yaani wakati ule wa tamasha, mzunguko wa fedha unakuwa umeongezeka sana.

Mheshimiwa Spika, sasa tunaposema tumsaidie Mheshimiwa Rais, taasisi ambazo zinalea sekta hii, ninashauri zishuke mpaka ngazi ya chini, BASATA, COSOTA na Bodi ya Filamu waende mpaka kiwango cha angalau ngazi ya kanda ili ku-facilitate wasanii, kusudi lile lengo la kuzalisha ajira milioni nane na kuongeza mapato katika Serikali na mtu mmoja mmoja yapate kutimia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunaposema easy way of doing business maana yake ni kupeleka zile huduma karibu na wale ambao wana contribution na mapato na kuzalisha ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya maneno hayo, naunga mkono hoja, nitachangia ipasavyo na kikamilifu katika Mpango. Mungu atubariki sote. (Makofi)