Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii. Nikipongeze Chama changu cha Mapinduzi kwa uwepo wangu hapa, kikiongozwa na Mwenyekiti wetu, Mheshimiwa Rais, Dkt. Magufuli; lakini zaidi niwashukuru sana wananchi wa Jimbo la Handeni pamoja na familia yangu kwa kunifanya niwepo mahali hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yamezungumzwa mengi hapa kuhusu hotuba ya Mheshimiwa Rais. Hotuba yenyewe ilijielekeza kutoa uelekeo wa nchi yetu kwa miaka mitano ijayo, pamoja na yote ambayo Mheshimiwa Rais anayafikiria ni ya muhimu na ambayo yatatuvusha kama taifa kuelekea miaka mitano na pamoja na hoja zote ambazo Wabunge wamezichangia. Kimsingi ukiangalia ni kwamba mambo haya mwisho wa siku yanahitaji fedha; ili tuweze kuyafanya yanahitaji fedha.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi nataka nichangie ili kujaribu kuishauri Serikali ni namna gani kama nchi tutajidhatiti kuweza ku-raise hizi fedha ambazo zinahitajika kwa ajili ya kuyatekeleza mambo haya ya kutuvusha miaka mitano ijayo.

Mheshimiwa Spika, la kwanza ambalo nataka nilishauri kwa Serikali yangu, tutakumbuka mwaka 2019 Bunge lako lilipitisha Finance Act yenye maboresho ya kikodi mengi sana, na moja kati ya maboresho hayo ilikuwa ni kupendekezwa kuanzishwa kwa Ofisi ya Tax Ombudsman, jambo ambalo mpaka leo halijafanyika.

Mheshimiwa Spika, ninaishauri Serikali yangu sikivu ianzishe ofisi hii muhimu ili kuendana na hotuba ya Mheshimiwa Rais ukurasa wa 12 ambapo ameelekeza kwamba lazima tuwe tunafanya business disputes, njia pekee ya kufikia hapo ni kuanzisha ofisi hiyo muhimu ya Tax Ombudsman.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo nataka nilishauri ni structure yetu ya chombo chetu muhimu cha TRA. Yote tunayotategemea yanategemea makusanyo ya ndani yanayofanywa na ofisi hii ya TRA. Ninachoishauri Serikali yangu ni kwamba TRA isiogope kuajiri vijana kwa sababu waajiriwa wa TRA siyo sawa na waajiriwa wengine wa pande nyingine za idara za Serikali, hawa unaajiri watu ambao wanakwenda kuzalisha moja kwa moja, wanatusaidia kukusanya kodi. Haiwezekani eneo la kimkakati kikodi kama ilivyo Ilala unakuwa bado una ofisi zenye watumishi wasiotosha, tunajichelewesha wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo nataka nilishauri ni habari ya informal sector. Informal sector inafanya biashara kubwa sana lakini haiwi captured kwenye mifumo ya kikodi. Hili ninapendekeza ufanyike utafiti mzuri na wa kutosha ili watu wetu wa TRA waweze kutoza kodi sehemu zote zinazozalisha ambazo ziko kwenye informal sector. Tusipojaribu kuli-balance hili litakuja kutuingiza matatizoni kwa sababu formal sector inayolipa kodi itakuja nayo kugeuka kuwa informal sector, ni lazima tufanye utafiti na tujaribu kuya- balance haya mawili.

Mheshimiwa Spika, pamoja na makusanyo mazuri yanayofanywa na TRA, ninashauri tusiwe tunapima ufanisi wa TRA kwa kuangalia increment ya makusanyo yao, kwamba mwaka jana walikusanya hapa, mwaka huu wameongeza kiwango hiki, hicho si kipimo peke yake cha kuonesha ufanisi wa taasisi hii muhimu kwetu.

Mheshimiwa Spika, naomba TRA na Serikali yetu kupitia Wizara ya Fedha wawe wanaangalia ratio kati ya taxes zinazokusanywa kwa uwiano na GDP ya kwetu. Tusipofanya hivyo hatari yake ni kwamba tutakuwa tuna- impose tax burden kwa walipakodi wachache kwa sababu increment hiyo unaweza ukakuta ni kwa sababu ya vertical raise kwa kuongeza tu makadirio ya kodi kwa wafanyabiashara walewale waliopo badala ya kui-spread ile kodi kwa uchumi wote.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nataka nilishauri ni habari ya mamlaka za Kiserikali. Mamlaka zetu za Serikali zinakuwa supplied na wafanyabiashara, sasa wafanyabiashara wanapokuwa wame-supply Serikalini ukichelewa kuwalipa maana yake unajichelewesha mwenyewe kuchukua kodi yako. Ni bora hata ukafanyika utaratibu kama fedha ya kuwalipa inakuwa haijapatikana, ile component ambayo ina kodi ndani ilipwe kwanza halafu ndiyo waendelee na procedures nyingine. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Reuben Kwagilwa.

MHE KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)