Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa sababu ya muda nitakwenda moja kwa moja kwenye hotuba ambayo tunaijadili hapa.

Mheshimiwa Spika, nimesoma vizuri hotuba zote mbili; ya Bunge la Kumi na Moja na Bunge la Kumi na Mbili. Kusema kweli kama ukizipitia vizuri unaona dhahiri kwamba yale mambo aliyoyasema Mheshimiwa Rais katika Bunge la Kumi na Moja na utekelezaji wake katika Bunge la Kumi na Mbili unathibitisha kwamba Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ameweza kutembea katika maneno yake. Kwa hiyo, tunampongeza sana kwa kazi hiyo nzuri na kwa namna ambayo sasa nchi inakwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme jambo moja; Watanzania wengi tunafika mahali tunasahau, zamani hata katika nchi zingine walikuwa wanasema Tanzania ni nzuri kwa kuweka mipango mizuri, ikishaweka ile mipango inatekelezwa katika nchi za wenzetu, majirani zetu. Lakini leo hao waliokuwa wanasema hivyo hiyo nafasi hawana maana wanashangaa jinsi ambavyo tunapanga mambo na jinsi ambavyo utekelezaji wake unavyokwenda. Kwa hiyo ukiangalia nchi zote, ziwe na Afrika mpaka kwa wale wenzetu wa Ulaya, wanatutamani, wanatamani Tanzania jinsi inavyokwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama hivyo ndivyo sasa ni vizuri tukaendelea tu kufanya tafakari kwamba hata huko tuendako hivi baadae mambo haya tutaendelea ku- maintain hii pace tuliyonayo au baadae mambo yatakuja yatushinde. Nadhani hilo ni jambo ambalo huko mbeleni tunahitaji kuendelea kulitafakari katika mustakabali wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, baada ya hilo sasa mimi nitoe tu mchango katika maeneo mawili kwa sababu ya muda. Eneo la kwanza ambalo tunahitaji sasa tuliangalie katika hiki kipindi tunachoenda nacho kwa kweli tatizo la ajira kwa vijana wetu bado ni tatizo kubwa kwa sababu vijana wengi wanamaliza chuo, lakini mwisho wa yote ajira imekuwa ni tatizo.

Kwa hiyo, ninadhani ni vizuri sasa Serikali ingejiangaliza huko, itengeneze programu maalum kwa ajili ya vijana hawa wanaotoka sekondari, wanaoshindwa kuendelea, lakini na wale vijana wanaomaliza vyuo vikuu, kwamba namna gani sasa tunaweza kuwa-accommodate katika kupunguza hili tatizo la ajira. Kwa hiyo, hilo ni moja ya eneo ambalo tunahitaji kuliangalia.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, viko vitu vingine ambavyo vilevile hata sasa hivi yawezekana hatuoni impact yake lakini bado impact yake ni kubwa. Leo ukipita katika vituo vyote vya polisi, maana yake vilevile tumezungumza kwamba kati ya watu tunaohitaji kuwasaidia ni hawa waendesha bodaboda. Kuna bodaboda zaidi ya 1,000 katika kila kituo cha polisi. Sasa ukija kuzijumlisha katika nchi nzima ziko nyingi sana na ziko pale zinaoza. Na unakuta wakati mwingine bodaboda mwingine alishikwa na ile bodaboda alikuwa hana leseni akakimbia na ameshindwa kwenda kuitoa ile pikipiki.

Kwa hiyo, nadhani Serikali inahitaji izianglie kwamba badala ya zile rasilimali kuendelea kupotelea pale, basi ni vizuri ikaangalia utaratibu mzuri wa kuunda tume au kamati fulani hivi ambayo inapita katika kila Wilaya iziangalie zile bodaboda zote zilizoko pale pamoja na makosa waliyofanya halafu waamue kwamba badala ya kufia pale ama Serikali izitaifishe au basi wale wa kurudishiwa waweze kurudishiwa kuliko ambavyo tunaendelea kutumia fedha za kigeni kuagiza bodaboda zingine, lakini tuna bodaboda nyingi zimejaa kule kituoni. Kwa hiyo, nadhani upande huo napo Serikali inahitaji kuliangalia namna ya kulisaidia zaidi.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, ukienda kwa hawa vijana wetu wa JKT, kusema kweli mimi ule mpango niliupenda na ni mpango ambao niliufurahia kwamba wale vijana wanakaa pale JKT ile miaka mitatu baadae kati ya hao vijana wanapata ajira. Lakini wale vijana wakitumiwa vizuri, wakifundishwa vizuri elimu ya ujasiriamali, wao wenyewe wana uwezo wa kuzalisha na kile watakachokizalisha na kwa kuwa watakuwa wamepata mafunzo, basi hicho hicho bado wanaweza kupewa tena baada ya ile miaka mitatu na wakaenda kuanza maisha na tunadhani kwamba kwa kufanya hivyo itawasaidia sana kuliko ile ambayo wakishatoka pale chuoni, wakishatoka JKT baada ya ile miaka mitatu halafu wengine tunawarudisha nyumbani.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)