Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ASYA MWADINI MOHAMED: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kuweza kunipa nafasi jioni ya leo nami kuchangia hoja ya Mheshimiwa Rais ambayo aliutubia siku ya uzinduzi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini hapa Dodoma.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kunipa pumzi na mimi leo nikasimama mbele yako ili kuweza kuchangia hayo ambayo yanakuja juu yako. Katika hotuba ya Mheshimiwa Rais nimeipitia, amezungumza vitu vingi, lakini mimi ninaomba kurudia ukurasa wa 13 na 14 ambao Mheshimiwa Rais alisisitiza zaidi kuhusu ulinzi wa amani, umoja, kuyalinda Mapinduzi matukufu ya Zanzibar, lakini vile vile suala zima la Muungano.

Mheshimiwa Spika, mimi nataka kuzungumza kipengele kidogo kuhusiana na kero kubwa za Muungano ambazo zinakumba Taifa hili. Tangu ninapata ufahamu na kulifahamu Bunge lako tukufu na nikiwa nikilifuatilia vipindi mbalimbali nimesikia watu sana Wabunge waliopita walikuwa wakilalamika juu ya mustakabali mzima wa kero za Muungano, lakini bado kero zinaendelea na hadi sasa tunaona kwamba kuna changamoto hizi zinaweza kuondoka kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, vikao vinakaliwa mbalimbali kujadili mustakabali mzima wa kero za Muungano lakini bado kuna kero ambazo tunakutana nazo asubuhi na jioni, na niweze kutoa mfano, kwenye kero kubwa ya masuala mazima ya biashara. Wazanzibari tunafahamu kwamba tumelelewa na utamaduni mkubwa wa masuala mazima ya ufanyaji wa biashara. Suala hili kwenye kero za Muungano linaudhi sana kwa sababu ndugu zetu kutoka Tanzania Bara hawawezi kuja kununua vitu kutoka Zanzibar, wakisafirisha kufika bandarini wanadaiwa malipo (charged) wanaambiwa hiyo ni mali ya Wazanzibari.

Sasa tunaona hapa ni jinsi gani kunakuwa na stofahamu kati ya bande hizi mbili wakati Mheshimiwa Rais kwenye hotuba yake amesema anasisitiza kuweka sawa suala hili nzima na kusema kwamba hatahakikisha usawa na maendeleo yatapatikana.

Mheshimiwa Spika, lakini maendeleo pia yawezi kupatikana bila kuwa na elimu, tunaziona changamoto za elimu kati ya Tanzania Visiwani na Tanzania Bara kitu ambacho ukiangalia syllabus ya msingi wa Tanzania Bara ambao unakuwa umetengenezwa na Wizara ya Elimu ya Tanzania bara lakini syllabus ya elimu ya msingi kwa upande wa SMZ syllabus hii pia inatengenezwa maana yake iko tofauti. Lakini syllabus hiyo hiyo ukienda kwenye sekondari wanatumia syllabus moja, lakini inapelekea kwamba bara wanasoma vitabu vyao na Tanzania Visiwani wana vitabu vyao. Hii ni changamoto kubwa kwa watoto wetu wa Kizanzibari inawapelekea sana na siku zote katika drop failure ya school huwa tunawaona watoto wa Kinzanzibari wana- fail sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Wizara husika inayosimamia masuala mazima ya Muungano naomba walichukue na walifanyie kazi kiukweli ni kero kubwa na inawaumiza sana Wazanzibari.

Kwa kuwa ni muda ni mchache sana naomba nichangie hotuba ya Mheshimiwa Rais ukurasa wa 46 unaozungumzia issue nzima za utalii. Mheshimiwa Rais alituambia kwamba mwaka 2015 kulikuwa na wageni ambao wanaingia 1,137,182 lakini kutoka gap ya mwaka 2015 mpaka 2019 ametuambia tena kuna gap ya wageni ambao waliokuwa wanaingia 1,510,051.

Mheshimiwa Spika, hapo unaoiona hii distance ambayo inaonekana bado miaka mitano yaani interval ya wageni kuongezeka ndani ya Tanzania imekuwa ndogo sana. Nishauri kwa Wizara husika ambazo zinasimamia masuala ya utalii waweze kuongeza nguvu za ziada kuweza kukaribisha wageni, waweze kufika ndani ya Tanzania, lakini vilevile tuna vivutio vingi ndani ya Tanzania yetu, kitu ambacho vitu hivi havisimamiwi ipasavyo na havitengenezwi vizuri, kwa hiyo, tunakosa wageni kufika. Mimi mwenyewe nimefika katika Makumbusho ya Bagamoyo na nimekwenda, hali ilikuwa hainiridhishi. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa Asya, dakika zako zimeshakwisha.

MHE. ASYA MWADINI MOHAMED: Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie…

SPIKA: Unga mkono hoja.

MHE. ASYA MWADINI MOHAMED: Mheshimiwa Spika, suingi mkono hoja. (Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Vedastus Mathayo Manyinyi.

MHE. ASYA MWADINI MOHAMED: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)