Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. JACKLINE K. ANDREA: Mheshimiwa Spika, nami nashukuru kwa kunipatia nafasi hii niweze kuchangia Bunge lako tukufu Bunge la Kumi na Mbili. Awali ya yote nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kunijalia kuwepo humu kama Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Napenda niweze kushukuru Chama changu cha Mapinduzi kwa kuniamini na kunipa nafasi yakuwa mwakilishi wa wanawake kutoka Tabora, pia niweze kuwashukuru akinamama wa Mkoa wa Tabora kwa kuniamini kuwa mwakilishi wao na mimi nawahahidi sitawahangusha. (Makofi)

Vilevile naomba nitowe shukrani zangu za dhati kwa familia yangu mume wangu mpenzi Mr. Seleman Sungi pamoja na watoto wangu watatu Tarik Seleman Sungi, Lion Seleman Sungi na Cairo Selemani Sungi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kutoa shukrani hizo naomba name nichangie hotuba ya Mheshimiwa Rais. Hotuba nzuri nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa hotuba nzuri iliyojaa matumaini kwa wananchi watanzania wote lakini niende moja kwa moja eneo la afya, niipongeze wizara ya afya kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuboresha sekta ya afya, tukiangalia miundombinu wachangiaji wa mwanzo waliona hilo na mimi pia naona nigusie hapo.

Mheshimiwa Spika, kuboresha miundombinu katika zahanati na vituo vya afya kutoka zahanati 1,198 na vituo 487; tunaona hayo ni maendeleo ndani ya miaka mitano iliyopita. Lakini vilevile niipongeze wizara ya afya na Serikali kwa kuweza kupunguza vifo vya akinamama wajawazito wakati wa kujifungua kutoka 11,000 kwa mwaka 2015 na mpaka kufikia 3,000 tunaona kwa miaka mitano tayari tumeokoa wa mama idadi 8,000 kwa mwaka. Kwa hiyo niombe Serikali kwa idadi hii iliyobaki Mungu akitujalia Inshallah hotuba ijayo tuweze kupata asilimia sifuri ya vifo vya akinamama wajawazito wakati wa kujifungua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naipongeza Wizara ya Afya kwa namna ambavyo wameweza kuboresha na kuweza Hospitali za Kanda za Rufaa kama Bugando, KCMC, Muhimbili, Benjamin Mkapa pamoja na Mbeya Refferal Hospital.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naiomba Serikali iweze kuangalia kanda ya Magharibi yenye Mikoa ya Katavi, Kigoma pomoja na Tabora. Jambo najuwa mpango upo basi Serikali iweze kutusaidia kwa haraka ili wananchi hawa wa Kanda hii ya Magharibi waweze kunufaika na wao kutokana na adha wanaoyopata ya hospitali ya rufaa kutoka Mkoa wa Katavi aende Mwanza basi iwepo kwenye Kanda yao ya Magharibi.

Naomba niongelee suala la maji napenda niipongeze Serikali na Wizara ya Maji kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kumtua ndoo mwanamke wa kitandania na nimpongeze Mheshimiwa Rais tarehe 30 Januari, 2021 ameweza kuzindua Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria, Mkoa wa Tabora. Lakini nilikuwa naiomba Wizara husika iweze kuangalia kwenye Wilaya na maeneo ambayo bado maji ya mradi huu wa Ziwa Victoria haujafika kama Urambo, Sikonge, Kaliua, Jimbo la Igalula ili wanawake hawa/akinamama wa Kinyamwezi waweze kupumzika na ndoo kichwani.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hivyo naomba niunge mkono hoja naunga asilimia zote nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa hotuba nzuri. (Makofi)