Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa hii nafasi ili na mimi niungane na Wabunge wenzangu katika kuchangia hii hotuba madhubuti, imara iliyojaa kila aina ya maelezo sahihi ya dira ya taifa letu kwa miaka mitano ijayo. Lakini nikiri pia kwamba baada ya kuangalia hotuba zote mbili kuna kitu kimoja ambacho Wabunge wengi hawajakiongelea mimi kimenigusa sana. Ni kwamba Rais wetu katika kupanga vipaumbele ametanguliza katika hotuba zote haja ya kuendelea kulinda na kusimamia tunu za Taifa ambazo ni amani, umoja, mshikamano pamoja na kuimarisha Muungano wetu na Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, mimi hivi vitu hasa amani imenigusa sana kwa sababu ni rahisi sana watu kuchukuwa for granted kitu ambacho wanacho kizuri bila kujuwa dhamani. Uki-imagine nchi ambazo zina vita katika dunia hii, nchi ambazo hazina, amani, umoja, mshikamano halafu sisi Watanzania tangu Uhuru tume-enjoy hivyo vitu na Rais alivyoji- commit kwamba moja ya kipaumbele chake namba moja ni kuendeleza amani ya nchi hii na umoja na mshikamano mimi nawiwa kusema kwamba tumpigie Rais makofi kwa sababu amelinda kwa dhati hayo mambo yanayohusu umoja wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia kwa sababu ametoa dira ya vipaumbele mbalimbali na muda huu wa dakika tano hautoshi kupitia vyote acha nichukue ya sekta inagusa roho ya wapiga kura yangu sekta ya mifugo. Napenda kumpongeza Rais kwa sababu ameelekeza kabisa na ameona umuhimu wa sekta hii ya mifugo kwa uchumi wa nchi yetu na ndiyo maana amekusudia kuongeza hekta zinazopatikana kwa ajili ya ufugaji kutoka milioni 2.8 mpaka zifike hekta milioni sita.

Mheshimiwa Spika, hivyo kwa kweli kwa jamii ya wafugaji wa nchi hii na uhakika ni faraja kubwa sana na niombe kuishauri Serikali basi kwa sababu Rais ameshaonesha dira kwamba tunahitaji kukuza sekta ya mifugo kama moja ya vyanzo vikuu vya kuongeza mapato ya nchi hii na kutuelekeza kwenye uchumi wa kati, ningeomba sera zingine za Serikali kama za uhifadhi kwa mfano basi waangalie vizuri hili suala kwa maana Rais ameshaonesha nia ya kuongeza maeneo ya malisho.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa masikitiko kuna maeneo mengine ambayo Wizara zingine niki-refer Wizara ya Maliasili wao wako katika harakati ya kupunguza maeneo ya malisho ili waongeze maeneo ya uhifadhi na wakati kiutamaduni au sijui kiasilia mifugo na wanyamapori vinarandana. Wilaya kama Wilaya yangu ya Longido ambayo asilimia 95 ni eneo la ufugaji na ni eneo pia la wanyamapori, tangu kuanzishwa kwa dunia imekuwa hivyo na ndiyo maana walioanzisha game controlled areas walianzisha tu wakijuwa kwamba ni maeneo ya wafugaji, lakini kulikuwa na proposal ya kutaka kumegua lile eneo la Longido asilimia isiyopungua 30 kwa sababu ni vijiji 14 kuvifanya viwe ni game reserve.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi nikafikiri kwamba hiyo itakuwa inaenda kinyume na azma ya Rais ya kuongeza maeneo ya malisho, maana ukishatengeneza game reserve maana yake mifugo hawana nafasi na bahati mbaya sana katika eneo kama lile la Longido yale maeneo ambayo game reserve ingetengenezwa ndiyo yale maeneo ya kimbilio ya wafugaji wakati wa kiangazi, milima kama ya Gelai, Ketumbeine, milima ile ya … ambayo inatokeza mpaka upande wa Namanga na maeneo ya Lake Natron. Kwa hiyo, ningefikiri hiyo dhana ya game controlled pamoja na sheria iliyopo ambayo napendekeza pia ifanyiwe marekebisho ili mifugo na wanyamapori pale ambapo matumizi mseto yanaendelezeka yanaendelee kuachwa hivyo hivyo maana sasa hivi game controlled areas kwa sheria iliyopo ndiyo watu wasiishi ndani lakini zimekuja tu sheria zimeweka wakati watu mule na maeneo ya wafugaji tu, hakuna shughuli nyingine na mimi naomba kwamba hii azma ya Rais ya kupanua maeneo ya malisho ya mifugo iendelee kuungwa mkono asilimia mia moja kuhakikisha kwamba Wizara zingine haziingilii Wizara nyingine katika kuhakikisha kwamba maeneo haya yapo, yanahifadhiwa maana yanahifadhiwa kwa ajili ya mifugo na siyo kwa matumizi mengine.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hiyo nigusie eneo la kilimo, kwa kweli linahitaji nalo tuangalie namna ya kuondokana na kilimo duni cha jembe la mkono twende kwenye kilimo cha kisasa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Dkt. Kiruswa.

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii naunga mkono hoja.