Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuunga hoja iliyoko mezani. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kunijalia kibali kuwa mahali hapa. Lakini nikishukuru Chama changu Cha Mapinduzi kwa kuniamini hususani Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kiupekee sana Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Simiyu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hotuba ya Rais imeeleza mambo mengi ambayo yametoa dira na vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano ambayo imewapa Tanzania matumaini makubwa hususan kwenye sekta mbalimbali za kiuchumi. Mambo haya yote yatafanikiwa endapo sisi tulioaminiwa kuwa wawakilishi wa wananchi wenzetu tutafanya kazi kwa bidii katika kumsaidia Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nijikite zaidi katika hotuba ya Mheshimiwa Rais hususan kwenye suala zima la mikopo itolewayo na Halmashauri zetu. Mikopo hii lengo la Serikali kuwaweza vijana lilikuwa ni nzuri zaidi endapo kama tutaendelea kuwajengea vijana uwezo hususan kwa kutoa elimu ya kutosha, lakini na mafunzo ya ujasiriamali. Kwa sababu kitu kinachotokea vijana wanapounda makundi wanakuwa hawana uzoefu na elimu ya kutosha hususan kwenye ujasiriamali wanakuwa hawana. Hivyo basi kama ambavyo tulivyo na miradi ya maendeleo ya kimkakati basi tulibebe na hili liwe ni fursa ya kimkakati hususan katika kuwaajiri vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ningependa kuishauri Serikali hususan kwenye hii mikopo isiwe ni sehemu muafaka sasa tuunde benki kwa ajili ya vijana ambapo hela zote ambazo zinatoka kwenye halmashauri ziingie kwenye ile benki ambayo tutaifungua lakini pia na mifuko hii ya uwezeshaji mifuko 18 ambayo ipo kwenye Ofisi ya Waziri iingie kwenye benki ambayo tutaianzisha. Nina imani kupitia kuanzisha benki hii itaweza kutoa mikopo kwa mtu mmoja tofauti na ambavyo inatolewa mikopo kwa vikundi. Kwa sababu kwenye vikundi kila mtu ana idea zake tofauti tofauti, unajikuta vijana hao wanashindwa kurudisha marejesho ya pesa wanazopewa Halmashauri zetu. Mwisho wa siku tunakuwa tunapoteza fedha ambazo zinakuwa ni changamoto kwenye Halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja, ahsante sana. (Makofi)