Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. JULIANA D. MASABURI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii name niweze kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais alipofungua Bunge letu la Kumi na Mbili.

Mheshimiwa Spika, kwanza na mimi kwa vile ni mara ya kwanza kusimama hapa kwenye Bunge lako tukufu napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kunipa kibali kuwa mmoja wa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, nikishukuru Chama changu cha Mapinduzi, kwa kutupa nafasi za upendeleo hasa sisi mabinti vijana kuja kwenye Bunge lako kuwawakilisha vijana wote Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niende moja kwa moja kwenye kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais, kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais wakati anafungua Bunge aliongelea kuhusu ukuzaji wa uchumi, katika ukuzaji wa uchumi aligusia kuhusu Serikali kuongeza jitahada za kuwezesha wananchi wake kiuchumi, lakini pia alisema kuwapatia mikopo ambayo haina riba au yenye riba nafuu. Hii mikopo napenda kuwapongeza Serikali kwamba Halmashauri zetu kote nchi inatoa hii mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, akinamama na walemavu, na inafanya vizuri sana kusema kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini bado hii mikopo haitoleta matokeo chanya kama tuvyotarajia, kwa sababu kwanza zile pesa ambazo zinatolewa na Halmashauri ni ndogo lakini pia Halmashauri au Serikali imesema kwamba mikopo hii itolewe kwa vikundi mbali za vijana, akinamama na walemavu, kwenye vikundi sio kila kijana wana idea ya kuwa pamoja na jinsi gani ya kufanya biashara. kwa hiyo, wanajikuta wanachukua hii mikopo baada ya kuchukua hii mikopo wanaanza kugombana kwa sababu kila mtu ana idea yake na kikundi kinavunjika. Vikundi vinavyovunjika pia mikopo ile iliyochukuliwa kwenye Halmashauri haiwezi kurejeshwa kwa wakati, kwa hiyo, inapelekea hii mikopo kutoonekana faida yake kubwa kwa vikundi ambavyo vinachukua mikopo na hasa vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ningependa pia kuishauri Serikali ingeangalia ni jinsi gani inaweza kumwezesha kijana mmoja mmoja kuchukua hii mikopo amesema Mbunge mwenzangu wa vijana pale Mheshimiwa Asia kwamba kijana mmoja akiji- commit akachukua mkopo akaaminiwa akachukua mkopo ni rahisi kurejesha kwa wakati ili kijana mwingine au watu wengine waweze kukopa zaidi. Lakini yule kijana pia ataajiri vijana wengine nyuma yake, watano au kumi atakuwa ameongeza ajira kwa vijana zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ningependa kuishauri Serikali iangalie jinsi gani inamsaidia sasa kijana benki zetu nchini Tanzania hazi-support vijana sana. Unakuta benki wanakwambia ukienda na business idea wanakwambia kwamba ni lazima uwe na collateral au uwe na bank statement kuanzia miezi sita, mwaka au miaka mitatu. Sasa kijana kama mimi nimetoka kwenye chuo VETA nina ujuzi, nina kila kitu, sina hiyo collateral, sina hiyo bank statement sina cash flow nitawezaje kuanzisha biashara bila kuangalia mfumo mzuri wa kutu-support vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia benki zetu zimekuwa rahisi sana kukopesha wafanyabiashara wakubwa, sisi Wabunge na wafanyakazi wa Kiserikali, lakini vijana imeweka kwamba ni lazima wawe na security. Ningependa kuishauri Serikali iangalie ni jinsi gani itakaa na hizi taasisi za kifedha itaangalia ni jinsi gani inaweza kumsaidia kijana mwenye idea nzuri ya kibiashara iweke tu uaminifu, kijana ana business idea nzuri, anachokiongea anakijua, anaweza kufanya biashara imuamini imwezeshe afanye biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wakati anafungua hili Bungeā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. JULIANA D. MASABURI: Mheshimiwa Spika, ahsante naunga mkono hoja. (Makofi)