Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. KABULA E. SHITOBELO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na amani tele hasa kwa kunipa kibali cha kuwa katika Bunge hili lako tukufu la Kumi na Mbili. (Makofi)

Napenda kukishukuru Chama changu cha Mapinduzi hasa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Rais Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wote wa chama bila kusahau viongozi wangu wote wa chama wa UWT Mkoa na Taifa, bila kuwasahau wapiga kura wangu wote wakinamama wa mkoa wa Mwanza, ahsanteni sana kwa kuniamini nije kuwawakilisha katika Bunge hili tukufu la Kumi na Mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia napenda kuishukuru familia yangu kwa kuwa wamenipa faraja sana kipindi cha kutafuta kura na siku zote za maisha yangu na mpaka leo niko hapa ni kwa sababu ya faraja zao, ninawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nipo hapa kwa dhati kabisa kuunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, nimesoma hotuba hizi zote mbili ya mwaka 2015 na 2020.

Mheshimiwa Spika, naomba nijikite zaidi kwenye suala la afya. Katika ukurasa wa 32 miaka mitano iliyopita (Awamu ya Tano) ya Serikali hii imefanya mengi katika afya kama kujenga vituo vya afya na kutoa huduma ya afya kwa vituo 1887, zahanati 1198, vituo vya afya 487 na Hospitali za Wilaya 99 pamoja na Hospitali za Mkoa 10 na Hospitali za Rufaa Kanda tatu. Pia imeweza kupunguza vifo vya akinamama wajawazito, miaka mitano iliyopita ilikuwa kila mwaka wakinamama 11,000 wanafariki kwa mwaka mmoja. Lakini kutoka mwaka 2015 mpaka 2020 limeweza kupungua kabisa tatizo hilo na kurudi kuwa wanawake wajawazito wanaofariki dunia ni watu 3,000 tu kutoka kwenye 11,000. Kwa hiyo napenda kuipongeza sana Serikali na Wizara ya Afya kwa ujumla kwa kujitahidi kwa jitihada zao hizo nzuri ya kumuokoa mama mjamzito. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuiomba Serikali sasa iweke kipaumbele zaidi kumaliza kabisa tatizo hili kama ambavyo imeweza kupunguza tatizo kutoka wanawake 11,000 kwa mwaka kufikia wanawake 3,000 ninajua kwa jinsi spidi tuliyonayo Serikali hii ikisimamia vizuri na Waziri wa Afya, Mheshimiwa Dorothy Gwajima namuamini mama huyu ni shupavu, akisimama kama yeye pia ni mwanamke ambaye ameshaingia labor anaujua uchungu wa mama mjamzito jinsi gani anapata matatizo. Kwa hiyo, ninaomba Serikali iliangalie kwa umakini kabisa jambo hili ili kumaliza kabisa vifo vya mwanamke na mtoto. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niko mbele yako pia kuomba suala la pili katika hospitali zetu za wilaya za Mwanza Wilaya zote hasa Wilaya ya Ukerewe jiografia yake ya kufikika au ya kutoka kuja Mwanza kwenye Hospitali ya Rufaa ni ngumu. Mfano Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe hakuna chumba maalum au wodi maalum kwajili ya mtoto njiti. Sasa pale complication yoyote au mtoto akizaliwa kabla ya muda, kwa hiyo kumuokoa yule mtoto inakuwa taabu sana. Ombi langu kwa Serikali nilitaka niombe ikiwezekana kujengwe japo wodi ambayo ya kulingana na Wilaya ile kwa ajili ya kuokoa mtoto njiti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante na naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)