Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. HADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi hii. Ikiwa leo ni siku ya kwanza nazungumza katika Bunge lako hili tukufu naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu sana, mwingi wa rehema na mwenye kurehemu amenijalia mimi kuwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba kumshukuru Mheshimiwa Rais na chama chake, Chama Cha Mapinduzi, Wajumbe wa Baraza wa Dodoma hii Mkoa, Wajumbe wa Baraza wa Taifa, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Ndugu Heri James na Umoja wa Vijana na Wazazi wote ahsante sana, muda hautoshi kushukuru wote, lakini naomba niishukuru familia yangu sana kwa support kubwa ambayo wamenionesha mpaka sasa kufikia hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ikiwa leo ni siku saratani duniani, mimi kama mtu mwenye ualbino nimeomba niongee leo ili niwaambie umma kwamba Mheshimiwa Rais amefanya kazi nzuri sana kwa watu wenye ulemavu au watu wenye ualbino, amefanya kazi nzuri sana. Amenunua mashine ambazo zinasaidia kuondoa tatizo la saratani. Hizi mashine ziko saba katika mikoa ya Singida, Iringa, Mara, Lindi, Zanzibar na kwingineko, lakini naomba nimuombe Mheshimiwa Rais kwa huruma yake, kwa uwezo wake, kwa kupenda kwake wanyonge, aongeze hizi mashine zitapakae mikoa yote kwa sababu hizi mashine mimi ni shuhuda wa hizi mashine. Nilikuwa na alama hapa shingoni kwangu ambayo ingeweza kunisababishia kupata saratani, hii mashine imenisaidia mimi kupona leo hii ninavyozungumza hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba Serikali yako tukufu, Serikali ya Chama Cha Mapinduzi, naomba kwa sababu ni sikivu sana, iongeze idadi ya lotions kwa watu wenye ualbino. Hizi lotions zinatusaidia sana kuondoa tatizo la kupata mionzi ya jua, hili tatizo ambalo linatufanya sisi tusiishi kwa amani tupate saratani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, natamani kila Mbunge aliyekuwepo hapa aende Ocean Road aone jinsi gani saratani ya ngozi inavyotumaliza na namna gani saratani ya ngozi inavyotuua. Na hata life span yetu ni miaka 35. Hapa nipo nina miaka 33 naingia miaka 34 tarehe 7 Februari, keshokutwa nashukuru Mungu kwa sababu familia yangu imeweza kunitunza na labda pia wamekuwa na uwezo kwa muda mrefu kunipa haya mafuta, lakini si kila familia ina uwezo wa kupata haya mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na yote haya naomba nimshukuru Rais mara ya mwisho kabisa. Nimwambie Mheshimiwa Rais ahsante sana kwa miaka mitano aliyoingia yeye ameondoa lile janga kubwa lililokuwa linaumiza Watanzania, lililokuwa linawaumiza na kuwaliza, lilimliza Waziri wetu Mkuu katika Bunge hili tukufu, janga la kuwauwa watu wenye ualbino. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, imani ile potofu imeondoka na sasa hivi tunaishi kwa raha, tunaishi kwa amani, tunajidai.

Ahsante sana Mheshimiwa Rais, lakini naomba nikwambie tena umejali sana watu wenye ulemavu, sasa hivi kila shule inajengwa kwa kuzingatia mazingira mazuri kwa watu wenye ulemavu kupita, lakini Mheshimiwa Rais pia nakuomba uboreshe mazingira ya vyoo kwa ajili ya afya. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. HADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba niunge hoja, naungana na hoja, ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Nimepata taabu kukatiza Mheshimiwa Keisha.

MHE. HADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, basi naomba niendelee.

SPIKA: Hapana, basi tena. Siku nyingine nitakufikiria leo muda umebana kidogo. (Kicheko)