Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, na mimi nichukue nafasi hii kwanza kukushukuru. Kwanza kabisa namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema; nakishukuru Chama changu cha Mapinduzi na wananchi wa Jimbo la Ilala kwa kunirudisha tena kuwa mtumishi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Rais ametoa hotuba kubwa sana. Ameshatoa vision ya nchi, kazi kubwa sasa ya wasaidizi wa Rais pamoja na Bunge ni kuweka road map ya utekelezaji wa mambo aliyoyatoa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais, katika hotuba yake aliyoitoa kwenye Bunge hili la Kumi na Mbili, ametoa maelekezo ya kupunguza au kufuta kodi za kero katika utalii. Utalii unaleta fedha nyingi sana Tanzania. Sasa hivi kutokana na Covid 19, watalii wengi ambao walikuwa wanakuja Tanzania, mishahara yao na mapato yao kwenye nchi walizotoka, nazo zimeathirika kutokana na kutokuweza kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali, waanze kufanyia kazi kuona ni kodi zipi za kero wanaweza kuzipunguza. Nataka nijue na niiulize Serikali, je, watalii hao wanaokuja nchini mwetu, mamlaka zinazohusika au Wizara zinazohusika wanayo data ya watalii wanaokuja Tanzania kwa maana ya anuani zao, majina yao na nchi zao ili kuweza kuwafuatilia, kuwasalimia kwenye siku za sikukuu au siku zao za kuzaliwa ili kuweka kama undugu wao na Tanzania ili waweze kuwa na hamu ya kurudi?

Mheshimiwa Spika, taarifa zinasema watalii hawarudi Tanzania. Je, tumejua kwa nini watalii hawarudi? Kama kodi ni kubwa, kama kuna kodi za kero na Rais ameshatoa maono yake, basi wataalam wetu wajitahidi kutekeleza.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Rais, kafanya mapinduzi makubwa sana kwenye mapato ya mawasiliano nchini mwetu, makubwa sana. Miaka ya nyuma Serikali ilikuwa haiwezi kuingia kwenye network cooperating center za vendors wa simu kwa sababu walikuwa hawana uwezo huo na Serikali ilikuwa haina appetite na makampuni hayo yalikuwa yanafanya self assessment kwenye kulipa kodi.

Mheshimiwa Spika, leo Serikali hii ya Dkt. Magufuli inaweza kujua every revenue user kwa kila mteja wa simu, kwa maana kodi sasa zinaku-cessed kitaalam na Mamlaka za Mapato. Ndiyo maana mapato ya kodi ya simu yamekuwa makubwa. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuliona hili na ninamshukuru kwa kuanzisha Wizara hii nzuri na imepata Waziri mzuri ambaye anachapa kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzi Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuwa kwenye shamba la mkonge. Miaka 60 mkonge ulikuwa unazalishwa Tanzania tani 130,000; Watanzania walikuwa 6,000,000. Leo tunazalisha mkonge tani 30,000 na Watanzania tuko milioni 60. Lazima Serikali ije na affirmative action ya kunyanyua mkonge, kunyanyua mazao ya mawese ili Taifa liweze kujitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba vilevile kuwe na programu ya kuwafanya vijana kupenda kilimo. Tuwe na machinga duka na tuwe na machinga kilimo. Kuna siku zitakuja, walimaji sasa hivi wana umri mkubwa sana. Itakuja kuwa na hatari Tanzania itakosa walimaji kwa sababu vijana wengi hawana programu au mapenzi na kilimo. Serikali ije na programu; Ethiopia wamefanya, wamechukua vijana zaidi ya 15,000, wamewaingiza kwenye programu na sasa vijana wengi wanajua umuhimu wa kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)