Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, nami nachukua nafasi hii nikushukuru wewe, lakini kipekee sana namshukuru Mwenyezi Mungu na nimshukuru sana Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Magufuli kwa kazi kubwa ambayo ameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wote ni mashahidi kwamba wakati Mheshimiwa Dkt. Magufuli anaingia, nchi yetu ilikuwa inakusanya mapato machache sana. Hivi sasa tuna uwezo wa kukusanya zaidi ya shilingi trilioni mbili kwa mwezi. Haya ni mafanikio makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya maombi yetu yote ambayo tunayatoa hapa ya maji, elimu na barabara hayawezi kutokea iwapo hatutamuunga mkono Rais katika kusimamia ukusanyaji wa mapato. Kwa hiyo, nawaomba Wabunge wenzangu, tutakapofika Bunge la Bajeti, tuweke mikakati ya kuisaidia Serikali ili tuwezekuongeza mapato, ili haya mahitaji ya Watanzania ambayo wote tuna azma kubwa ya kuitimiliza, yaweze kufanikiwa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Rais, lakini pia nampongeza kwa kuja na approach ya kuanzisha Mamlaka ya Maji yaani RUWASA. Sisi sote ni mashahidi, kabla hatujaanzisha Wakala wa RUWASA, maji na upatikanaji wa maji katika vijiji vyetu ilikuwa shida sana.

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo langu la Manyoni Mashariki, tuna mradi mmoja mkubwa wa shilingi bilioni 11 wa Kitinku/Lusilile. Huu mradi una-cover vijiji 11 na tayari tumeshapata takribani shilingi bilioni mbili. Mbali ya kwamba tumeanzisha hizi Wakala, bado nina ushauri kwa Wizara ya Maji. Ushauri wa kwanza ni kwamba nadhani tusiwe na utitiri wa miradi ya maji. Tujitathmini kwa miradi ambayo tumeianzisha, tutengeneze acceleration plan, kwamba kwa kipindi gani tutamalizia ile miradi ambayo tayari tumeshaianzisha.

Mheshimiwa Spika, Rais wetu ni mtu wa matokeo, anataka kuona matokeo kwa kitu alichokianzisha. Kwa hiyo, naishauri sana Wizara ya Maji, kwa miradi ambayo tumeianzisha, tusikimbilie kuanzisha mradi mpya, tutengeneze acceleration plan ya lini tutamalizia ile miradi, halafu tuangalie ni jinsi gani tunaweza ku-scale up hii approach ambayo tumeanza nayo kwenye maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, vilevile naomba Wizara ya Maji iongeze wigo wa financing ya Mfuko wa Maji. Kutegemea chanzo kimoja ku-finance miradi ya maji, bado naona tunaipa mzigo sana Serikali. Naomba wakati Bunge la Bajeti likifika Wabunge tuangalie jinsi gani tutaisaidia Wizara ya Maji, tuje na options mbalimbali za kupanua wigo wa kuongeza financing mechanism ya miradi ya maji.

Mheshimiwa Spika, suala la TARURA, vilevile namuunga mkono Rais hasa kwa kuanzisha Wakala wa Barabara (TARURA). Sote ni mashahidi, kulikuwa na tatizo kubwa sana la ujenzi wa barabara za TARURA, lakini wachangiaji wengi wameelezea suala la kuongeza na kubadilisha allocation formula ya 70 kwa 30.

Mheshimiwa Spika, nina hoja mbili; hoja ya kwanza, nadhani tatizo ni ile fixed approach, kwa sababu tunatumia 70 kama ilivyo na 30 kama ilivyo. Nashauri tuwe flexible. Mahitaji ya utengenezaji wa barabara yanategemeana na demand ya mwaka huo. Kuna kipindi demand ya barabara ya vijijini ni kubwa kuliko demand ya barabara za mjini ambazo zinasimamiwa na TANROADS. Nashauri sasa kwamba inapofika kipindi ambacho tunahitaji kupeleka bajeti TARURA na TANROADS, basi mfuko wa barabara usikilize mawazo ya TARURA na TANROADS, wa-present waone kwamba je, kweli TARURA wanahitaji asilimia 30 au wanahitaji zaidi ya asilimia 30? Hiyo ndiyo hoja yangu.

Mheshimiwa Spika, lingine nashauri kwamba, tuna- depend sana kwenye chanzo kimoja cha ku-finance TARURA. Tuna-depend sana kwenye fuel levy, ambacho nadhani kimelemewa. Nashauri Bunge lako tukufu tutafute options nyingine za ku-finance TARURA. Badala ya kusema tuongeze asilimia 30, nadhani kuna haja sasa ya kuhakikisha tunaongeza wigo.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Chaya.

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Rais. (Makofi)