Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kukushukuru sana wewe kwa kunipa nafasi hii. Pia nianze kwanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema ambaye amenijalia kibali kusimama mahali hapa. Vilevile nakishukuru Chama changu cha Mapinduzi kwa heshima na imani ambayo walinipa. Pia nawashukuru sana wapiga kura wangu wa Momba kwa kuniamini na kunituma mahali hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niendelee kuwashukuru sana wazazi wangu kwa kunilea na ushirikiano mkubwa ambao walinipa kipindi cha uchaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais kwa asilimia 101. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Rais huyu na kusema kwamba ni miongoni mwa viumbe ambao wamemkopesha Mungu kwa kiasi kikubwa sana. Maandiko matakatifu yanasema kwamba anayemsaidia mnyonge na maskini anakuwa amemkopesha Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika kipindi chake cha miaka mitano amefanya mambo mengi ambayo amewagusa wanyonge na maskini wengi sana na watu ambao walikuwa hawana watu wa kuwasemea, yeye amekuwa ni msemaji wao. Kwa hiyo, ninaamini hata katika vipindi vyake vigumu ambavyo atapitia, Mungu atazikumbuka na kuzitakabali hizo sadaka zake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, ni kwa sababu ya muda, nilitamani kuchangia kwa kirefu kuhusiana na eneo la biashara. Kwenye eneo la biashara nitaenda kuongelea zaidi kwenye masuala ya mipaka. Sehemu nyingi ambazo ni za border kumeonekana kuwa na mwamko mzuri sana wa biashara. Nikitolea mfano kwa border ya Namanga na Tunduma, ni sehemu ambazo zina wafanyakazi ambao wamesoma na kuajiriwa wachache sana kuliko wafanyabiashara wanaokuwepo pale. Hivyo, inapelekea kuwepo kwa maendeleo mbalimbali ya kijamii, pia hata vijana na watu mbalimbali kuendelea kupata riziki na watu wengi kupata ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye ukurasa wa 26 nataka ku- quote kipengele kidogo tu kwa sehemu, Mheshimiwa Rais anasema hivi; “…na kwa bahati nzuri tangu mwaka jana tumeanza kutekeleza mpango wetu wa kuboresha mazingira ya biashara nchini, yaani blueprint for regulatory reforms to improve the business environment in Tanzania.”

Mheshimiwa Spika, nataka kusema hivi, nitolee mfano wa mpaka wa Zambia na Tanzania ambapo kidogo angalau nimekuwepo kwa hizi nchi za Kusini mwa Afrika na Afrika ya Kati. Naomba kuishauri Serikali na kuiomba, kama mawazo haya yanaweza yakawa chanya na yakasikilizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali iweze ku-expand mipaka yake. Pamoja na kuipongeza kwamba imepiga hatua sana katika kujenga hizi One Stop Border, mfano border ya Namanga na Tunduma, zimejengwa katika kipindi cha miaka mitano, lakini ipo hasara kubwa sana ambayo Serikali inapata kwenye hii mipaka. Bado biashara nyingi ambazo ni haramu, biashara za magendo, kutoroshwa kwa mazao vinaendelea kufanyika kwenye hii mipaka kiasi kwamba kama Serikali ingeamua ku-expand ile mipaka tungeweza kuzuia biashara haramu nyingi na biashara nyingi za magendo ambazo zinafanyika kwenye hii mipaka, ikasababisha Taifa likaendelea kukusanya fedha ya kutosha ambayo itaendelea kutusaidia.

Mheshimiwa Spika, nikitolea mfano mpaka wa Zambia na Tanzania, ndiyo mpaka ambao unabeba karibu nchi zote ambazo ziko Kusini mwa Afrika. Mfano, tunapoongelea mji mmoja wa Livingstone pale Zambia, ndiyo mji ambao unapokea mpaka wa Botswana, Namibia na Zimbabwe. Kwa hiyo, nitolee mfano labda bidhaa za magendo zinapotaka kupitia lile jengo la SADC zinapitaje?

Mheshimiwa Spika, nitoe mfano wa kwenye Jimbo langu na hapa ninaiomba Serikali ikiwapendeza tupewe geti. Kwenye mfano huu naeleza, unapotoka pale Livingstone, kwenye zile nchi tatu, tuchukulie amekuja na biashara za magendo, anataka kukwepa kodi ya Serikali… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)