Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ASYA SHARIFU OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza napenda nitumie nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, lakini kipekee nikishukuru Chama changu cha Mapinduzi ambacho kimeniamini na kikanipa nafasi na mimi nikawa Mbunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kipekee naomba niwashukuru Wajumbe Wanawake wa UWT wa Mkoa wa Kaskazini Pemba wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi ambao nao walinipa imani ya kuweza kufika katika Bunge lako hili tukufu la Kumi na Mbili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa upekee naomba nichangie hoja ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Mimi binafsi nikiwa Mbunge wa Bunge hili tukufu ambaye natokea Mkoa wa Kaskazini Pemba nasema hoja ile ya Mheshimiwa Rais ambayo ameiwasilisha katika Bunge hili naipongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kisiwa cha Pemba kwa mara hii wameonesha umahiri na wameandika historia katika kisiwa chetu. Hii ni kutokana na utekelezaji wa Ilani ambao ulionesha imani kubwa kwa wananchi na Watanzania kwa ujumla wakiwemo wananchi wa Pemba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niipongeze Tume ya Uchaguzi, Tume hii ilifanya kazi nzuri ambayo wananchi wale waliweza kutumia haki yao ya demokrasia kwa uwazi na uhuru bila kulazimishwa wala kuonewa. Vyombo vya habari, nitakuwa mwizi wa fadhila kama sikuvishukuru, vilifanya kazi nzuri sana bila upendeleo. Hii ni kuonekana kwamba nchi yetu ina amani, utulivu na mshikamano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa heshima kubwa ya Bunge hili tukufu, niishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano mkubwa ambao umetujengea uwezo sisi Wabunge kushirikiana na Bunge letu hili na kuunganisha Watanzania wote bila ubaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi wanawake wa Mkoa wa Kaskazini Pemba wengi tunajishughulisha na shughuli za kilimo na uvuvi. Lakini ni juzi tu kupitia Muungano huu tuliokuwa nao Serikali imeweza kusaini suala zima la uwekezaji wa utalii.

Mheshimiwa Spika, kama unavyofahamu Kisiwa chetu cha Zanzibar kinajishughulisha sana na masuala ya utalii, ni imani yangu kwamba wanufaika wakubwa tutakuwa sisi wanawake na vijana, kama ulivyosema Bunge hili huwezi kuliita ni Bunge la vijana au ni Bunge la wazee. Sasa sisi kule Pemba, wanaume hao kutokana na mambo ya dini, tunaolewa, tunakuwa na wake wenza wanne au watano. Sasa fursa hizi za Serikali… (Makofi)

Mheshimiwa Spika, samahani ni wanne. Kwa sababu fursa za Serikali zimeweza kutoa suala la ujasiriamali na kweli lazima tuseme ukweli wanawake wajane tuko wengi sana. Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba Serikali itaendelea kutusaidia katika kuona nyanja hizi za uchumi ambazo zitawezesha wanawake kupata ajira.

MBUNGE FULANI: Sawa sawa.

MHE. ASYA SHARIFU OMAR: Mheshimiwa Spika, haiwezekani wanawake wote waajiriwe kwenye Serikali, ni lazima na ajira binafsi ziwepo. Tunampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa imani yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)