Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. DKT. RITTA R. KABATI: Mheshimiwa Spika, Ahsante naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi lakini moja kwa moja niende kwenye point nimshukuru Mwenyezi Mungu, nikishukuru Chama changu cha Mapinduzi lakini pia niwashukuru wajumbe walionichaguwa nikiwemo humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hotuba yake aliyotoa hapa Bungeni kwa sababu kwanza alitoa dira na maelekezo nini tufanye na na Serikali nini ifanye kwa hiyo kwetu sisi kazi yetu kufanya.

Mheshimiwa Spika, hotuba ambayo imekuwa elekezi kwa viongozi wote vilevile naomba nichukue nafasi kupongeza ya uchaguzi kwa kusimamia zoezi lile vizuri kwa kuwa uchaguzi ulikuwa uhuru na haki na viongozi wote walioingia humu ndani wameingia kwa uhuru na haki, niwapongeze Wabunge wote wa Chama cha Mapinduzi lakini pia wa vyama vya upinzani kwa sababu wote tunajenga nyumba moja.

Mheshimiwa Spika, naomba moja kwa moja nielekeze katika miradi ya maji kwa sababu sisi ni Wabunge Wanawake ambao tunawakilisha wanawake tumeona hotuba hii imelenga moja kwa moja kuhusiana na miradi ya maji. Ujenzi wa miradi ya maji imefanya wanawake wengi sana sasa hivi hawahangaiki kutafuta maji, tunaona kwamba katika Mkoa wetu wa Iringa kulikuwa na tatizo kubwa hasa miradi ya vijijini kwamba miradi ya Kilolo, kule Mufindi, Isimani, wanawake walikuwa wanapata shida sana hata katika Mkoa wetu wa Iringa unaona maji yalikuwa yanatuletea adha kubwa, kuna ndoa nyingi sana ziliweza kupata matatizo kwa sababu maji ni uhai, lakini mwanamke anaamka asubuhi time ambayo anatakiwa ailinde ndoa yake anaenda kuiangaikia maji. Kwa hiyo, kwa kweli Mheshimiwa Rais amelinda hata ndoa zetu katika Mkoa wetu wa Iringa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba tu hata mimi nitowe ushauri kwamba Serikali sasa hivi ianze kuangali uvunaji wa maji kwa sababu maji kumekuwa na upotevu wa maji mkubwa, tukitengeneza miundombinu ya kuvuna maji hasa katika mabwawa tutasaidia hata mifugo yetu wakati ule hakuna mvua itapata maji, lakini vilevile tunaona kwamba hizi mvua zimekuwa zikija na mafuriko makubwa, kwa hiyo, tukivuna haya maji yatasaidia pia kuzuia uharibifu katika mito yetu, lakini pia hata mabarabara na madaraja wakati wa mvua za masika.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kuhusu suala la afya niipongeze sana Serikali yetu imeweza kujenga zahanati 1,998, vituo vya afya 487, Hospitali za Wilaya 96, Hospitali za Kanda tatu lakini maboresho ya afya yamesababisha hata kupunguza vifo vya akinamama na watoto. Tunaona mwaka 2015 vifo vilikuwa 11,000 lakini sasa hivi mwaka 2020 unaona vifo vingi vimepungua vimefikia mpaka vifo 3,000 kwa mwaka, hii yote ni kwa sababu ya maboresho mazuri ya vituo vya afya, lakini vilevile Serikali ihakikishe kwamba inaweka watumishi kwenye vituo vya afya, inaleta madawa ya kutosha, lakini naomba ili kupunguza vifo vya watoto njiti iwekeze kwenye vituo vya afya kwa sababu tunaona katika vituo vya afya hakuna zile incubator kwa ajili ya watoto, watoto wengi sana wamekuwa wakipoteza maisha katika vituo vya afya, kwa hiyo naomba sasa Serikali iwekeze sana kwenye vituo vya afya mambo incubator.

Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye ukurasa wa 27, imezungumzia kuhusu kilimo, Serikali inakusudia kuongeza tija na kufanya kilimo kuwa cha biashara. Karibu asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima, kwa hiyo, tukiwekeza kwenye kilimo ina maana kwamba sasa hivi tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda na kwenye kilimo ndipo ambapo tutapata malighafi. Kwa hiyo, kwa kweli tukiondoa changamoto nyingi ambazo zipo kwenye kilimo, ndipo ambapo tunaona hata Mheshimiwa Rais amesema kwamba ni aibu kubwa kuwa na njaa kwenye nchi yetu. (Makofi)

Lakini sasa hivi nchi yetu ya Tanzania ina uwezo hata wa kupeleka vyakula katika nchi nyingine. Lakini kuna mkakati mahususi kuhakikisha kwamba sasa hiviā€¦

(Hapa kengele ililia kaushia kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)