Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kutumia nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwani hii ni mara yangu ya kwanza kuchangia katika Bunge hili Tukufu. Vilevile niwashukuru zaidi Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Bahi na niwashukuru wananchi wa Bahi kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba ya Mheshimiwa Rais inaonesha dira ya namna gani taifa letu linapotaka kwenda. Tumeshuhudia nchi yetu imefanya uwekezaji katika sekta mbalimbali. Serikali imewekeza kwenye afya, elimu na sasa inawekeza kwenye miundombinu ya reli na umeme, ni mabilioni ya shilingi yanatumika katika uwekezaji. Katika nchi yetu takribani asilimia 75 ya wananchi wetu wako kwenye kilimo, kwa maana hiyo unavyowezesha afya, elimu, ni ili uwe na productive force ambayo itaweza sasa ku-engage kwenye uchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wote tunafahamu kilimo kwa maana ya uhai wa taifa lakini kilimo tangu historia ndiyo habari ya national security. Serikali nyingi duniani zimeangushwa kwa sababu ya kulegalega na kukosa chakula. Sote tunafahamu historia ya mkate ulivyoangusha utawala pale Ufaransa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuchangia hivi na hili nasisitiza siyo kwamba tulete wawekezaji kwenye kilimo, tunataka Serikali iwekeze kwenye kilimo. Maana yangu ni kwamba tumekuwa na Benki ya Kilimo lakini bado haijawasaidia wakulima. Mchango mwingi wa wenzangu waliopita wamechangia kwamba tunaagiza kwa kiasi kikubwa ngano, mafuta lakini hata sukari yenyewe bado hatujakaa sawasawa kuhimili utoshelevu katika taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kilo moja ya korosho mkulima anaiuza kwa dola moja, lakini kilo moja hiyohiyo ikishakuwa processed inakwenda kuuzwa kwa dola 20. Ireland walianza na model inaitwa vertical forward integration kwamba mkulima wa alizeti atapeleka alizeti kwenye kiwanda cha kukamulia mafuta kwa huduma ya kukamuliwa mafuta, siyo kwenda kuuza alizeti yake. Ikishatoka pale sasa ile alizeti inakwenda katika mlolongo wa kwenda kuuzwa na hela ile mkulima ndiyo anaipata. Pamoja na hilo, kwenye kiwanda kile mkulima anapata hata mashudu. Kwa hiyo, ni vyema Serikali ikawekeza hasahasa kwenye ushirika, kwamba kama tunaitumia Benki ya Kilimo tuweze kuwa-empower watu wetu kwa kuanzisha vyama vya ushirika ambavyo vitakuwa na mashine za kufanyia processing.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, suala la ngano; tunatumia takribani shilingi milioni 300 kwa mwaka, hivyohivyo kwenye mafuta. Kwa hiyo, bado soko la ndani ni kubwa kwa hiyo ni vyema sasa Serikali iwekeze yenyewe si kuleta wawekezaji kwenye kilimo. Bado tuna nafasi ya sisi wenyewe kuwekeza kama Serikali ili tupate utoshelevu wa bidhaa hizi ambazo tunaagiza kwa kiasi kikubwa kutoka nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, total importation ya chakula katika Bara la Afrika ilikuwa ni dola bilioni na zaidi kwa mwaka kwa takwimu za mwaka 2018. Maana yake nini? Maana yake ni kwamba hata soko la Afrika bado ni kubwa kwa sisi Watanzania tukaweza ku-export. Tumeshuhudia tani na tani za mchele zinapita hapa kwenda Kongo, mchele kutoka Asia unapita kwenye nchi yetu kwenda Kongo. Kongo wame-import mchele kwa thamani ya dola milioni 65 lakini fedha hizi za Wakongoman zilitoka hapa na kwenda katika Bara la Asia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalize kwenye export. Nchi ya Vietnam ni ndogo kwelikweli katika Bara la Asia, ni nchi ya tatu duniani lakini kwa ujumla wake ina-export mchele kuliko Bara la Afrika, yaani chukua nchi zote za Bara la Afrika, ziunganishe, hazifikii kiwango cha Vietnam inacho-export. Vietnam ina-export kiasi cha 1.4 billion dollars kwa mwaka; hizo ni takwimu za mwaka 2019 lakini kwa combination ya Afrika hawaifikii Vietnam, Vietnam ni nchi ndogo sana. Niliwahi kwenda Hanoi, ukitoka kidogo kama hapa ukienda Area C tayari kuna majeruba ya mpunga. Kwa hiyo, wenyewe mpunga is everywhere lakini kama navyosema, ni aibu kwa Bara zima la Afrika kwamba tunashindwa na nchi kama Vietnam.

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee kilimo cha mpunga kwenye Jimbo langu la Bahi.Bahi tuliwahi kujengewa skimu na FAO na IFAD. FAOwalitujengea skimu mwaka 1997; hakujawahi kufanyika tena ukarabati tangu kipindi hicho. IFAD walitujengea skimu mwaka 2004, mvua ya kwanza ilikuja ikavunja tuta, hakujawahi kufanyika tena repair na kilimo hakiendelei katika skimu ile ya Mtita.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu Bodi ya Mikopo. Nataka tubadilishe model ya kuwafadhili vijana wetu. Vijana wetu tukiwapa hela, hela ile hawawezi kuitunza, ndani ya wiki mbili, tatu wameshazimaliza na hela zinavyotoka wengi wanajaa mjini huku kwa ajili ya kugonga bia. Sasa kwa nini tusiwe na mfumo, kwa mfano nchi ya Japan, anakuwa na kadi ya kwenda ku-swipe kwenye chakula.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii itarahisisha ku-manage economy, hasa vijana wetu wasiweze kushinda njaa kwenye vyuo vikuu. Badala ya kuwapa hela washike sasa tufanye utaratibu wa ku-swipe katika huduma mbalimbali, iwe kwenye chakula, hostel, hii itarahisisha vijana wetu wasome, hata book allowance siku hizi kuna vitabu electronic, wataweza ku-swipe na kununua vitabu. Suala hili litatusaidia kwanza Watanzania wengi wapata mkopo lakini vilevile itasaidia zaidi vijana wetu waweze kusoma kwa uhakika.

Mheshimiwa Niabu Spika, ahsante sana. (Makofi)