Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema ambaye kwa kweli amemwezesha kila mmoja wetu kufika mahali hapa. Jambo la pili, nichukue nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Rais pamoja naChama changu Cha Mapinduzi ambacho kwa kweli kimeweka imani kubwa kwa sisi vijana, kimetuamini katika umri huu, ni jambo kwa kweli kwa kumshukuru Mheshimiwa Rais na Chama chetu Cha Mapinduzi. Kwa kweli ni jambo ambalo mimi katika umri huu nisiposhukuru tena mara ya pili nitakuwa sijamfanyia haki Mheshimiwa Rais kwa kusema ahsante sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na hotuba zake mbili ambazo alizitoa Mheshimiwa Rais nitajikita kuchangia sanasana katika hotuba yake aliyeitoa Novemba 13 mwaka 2020. Kumekuwa na jambo ambalo ningependa nizungumzie katika hotuba ya Rais na jambo lenyewe ni juu ya kilimo. Jambo la mafuta ya kula limekuwa nicross cutting issue na imekuwa ni current matter ambayo kwa kweli inaendelea kujitokeza mwaka hadi mwaka na mimi leo nitakuwa na mchango kidogo juu ya suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, upungufu wa mafuta ya kula hapa nchini naomba iwe ni ishara ya Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi na chini ya Jemedari Dkt. John Pombe Magufuli kuwa ni ishara ya kutuonyesha kwamba tunahitajika kufunga kamba ndani ya viuno vyetu ili tuweze kufikia azma ya viwanda kikamilifu. Kwa takwimu tu haraka haraka nchi yetu inaonyesha kabisa kwamba inazalisha tani laki mbili za mafuta ya kula, lakini mahitaji yetu ni tani laki tano kwa mwaka, hivyo tunakuwa na upungufu wa tani laki tatu ambazo nchi yetu inaagiza tena hasa katika nchi za bara la Asia san asana Malaysia na nchi ya Indonesia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa tafsiri hiyo inaonyesha kabisa kwamba tunachukua pesa nyingi za kigeni kwa ajili ya kuagiza bidhaa hii ya mafuta ambayo nikisoma hotuba ya Mheshimiwa Rais ukurasa wa 15, naona hii ni aibu kubwa kwa nchi kama Tanzania ambayo ina ardhi yenye rutuba kuagiza mafuta nje. Kwa hali halisi ilivyo nakulingana na matamko mengi ambayo Serikali imekuwa ikitoa, naomba nijielekeze kuionesha Serikali kwamba kuna wajibu mkubwa wa kuelekeza katika zao hili la mbegu ambapo mafuta yanatokana na mbegu hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano, mwezi Mei, 2017 aliyekuwa Waziri wa viwanda wakati huo Mheshimiwa Mzee wangu Mwijage alinukuliwa akisema: “Takribani asilimia 70 ya mafuta ya kula yanayohitajika kutumiwa hapa nchini huagizwa kutoka nje ya nchi, maana mafuta yanayozalishwa na viwanda vyetu hayatoshelezi kabisa.”

Mheshimiwa Naibu Spika, si hivyo, tarehe 4 Septemba2018bado kauli hii imeonyesha kabisa kwamba bado hatujajitosheleza katika kuzalisha mafuta ambayo yanatosha kutumiwa na watu wetu. Hivyo Mheshimiwa Waziri Mkuu alinukuliwa naye pia akisema kauli ambayo inafanana nahiyo nami nitamnukuu kwa kifupi sana, anasema: “Hivi sasa nchi yetu inatumia takribani dola za kimarekani milioni mia mbili tisini na nne kila mwaka kuagiza mafuta nje ya nchi.”

Mheshimiwa Naibu Spika, tafsiri ya hali hii inaonyesha kwamba pamoja na kuwa na janga la corona ambalo limeikumba dunia na limelikukumba dunia na limezikumba baadhi ya nchi bado inaonyesha changamoto hii imekuwa ikijirudia mwaka hadi mwaka, nini kifanyike na ushauri ambao naona nishauri Serikali yangu. Naona kwamba ni vema zaidi ikajielekeza kwenye kilimo cha mazao ya mbegu, kama karanga, zao la chikichi ambalo kwa kweli nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu amekuwa akionesha jitihada kubwa, amefika Kigoma katika kulishughulikia zao hili la chikichi. Itoshe tu kusema kwamba zao hili la chikichi linaonesha katika takwimu za kidunia kwamba ndilo ambalo limeziwezesha nchi zingine kamaNchi za Malaysia kuweza ku– supplykwetu mafuta haya ya kula na hata kusambaza duniani kote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna faida kadhaa tukijielekeza katika kilimo cha mazao yanayotokana na mbegu. Faida ya kwanza ni jambo la uhakika ambalo soko letu la ndani tutaweza kulihudumia kwa kujitosheleza na hatimaye tutaepuka kuagiza mafuta haya ya mchikichi. La zaidi sana, itakuwa ni ishara tosha ya kwenda kutekeleza ndoto madhubuti ambayo ya kutibu aliyonayo Mheshimiwa Rais ya kuweza kuzalisha ajira milioni nane alizozisema katika Ilani ya Uchaguzi kwenye ukurasa wa tano.

Vile vile tukifanya hivyo kuwekeza katika mazao haya, itakuwa ni ishara tosha kabisa kwamba tutaifanya nchi yetu kuweza ku-export zaidi mafuta na hatimaye kutoka kwenye kundi lakuwa importation country na hiyo hiyo itatuwezesha hata kuimarisha shilingi yetu na hali ya shilingi yetu itakuwa imara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nirudie kauli ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa katika hotuba yake ya Novemba 13, amesema kabisa: “Kwa haya machache ninaona ni vyema zaidi Wizara husika ikachukua hatua madhubuti na kujielekeza katika mazao haya ya mbegu ili tuweze kuepukana na changamoto hii ya mafuta ambayo inajitokeza mwaka hadi mwaka”. Kwa nchi nilizozitaja kama Malaysia na Indonesia lakini nchi kama Malaysia walichukua mbegu kwetu Kigoma katika Kata ya Simbo na wakapeleka kwao kwa ajili ya kuzalisha mafuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, naona kengele imelia, nilikuwa na mengi ya kuchangia ila mchango wangu nitauleta kwa maandishi ili Serikali waweze kuona mawazo yangu juu ya hotuba ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)