Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

Hon. Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha Wabunge wote, tumepata ushindi wa kishindo na Mwenyezi Mungu ametuwezesha kuwepo hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuunga mkono hoja Hotuba ya Mheshimiwa Rais ambayo imegusa nyanja zote; ametupa uelekeo wa nchi nzima na baada ya miaka mitano kama haya tutayasimamia kama Wabunge kwa nia njema ya maono na kumsaidia Mheshimiwa Rais, nadhani nchi ya Tanzania tutapiga hatua kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi natokea Mkoa wa Rukwa. Mkoa wa Rukwa ni tajiri kama maono ya Mheshimiwa Rais anaposema anataka mabilionea. Mkoa wa Rukwa ni matajiri kwa sababu hali ya hewa ni nzuri, ni wazalishaji wazuri, tatizo ni miundombinu. Naomba Wizara inayohusiana na miundombinu hasa upande wa barabara, baadhi ya barabara, mfano kwenye Jimbo langu la Nkasi Kusini, mimi sina mjini; ni vijijini, porini, ni wazalishaji tu, lakini hakuna barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukija Jimbo la Nkasi Kusini upande wa Ziwa Tanganyika, bado hatujalitumia. Ziwa Tanganyika bado linatumika ndivyo sivyo. Namshukuru Mheshimiwa Rais amesema ataweka meli ya mizigo, sasa meli ya mizigo ikija na miundombinu hamna, itakuwa bado ni shida.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara hizi ziangalie maeneo ambayo ni economic zone kila jimbo. Kuna barabara ambazo ni economic zone, ndiyo mhimili, ndiyo mgongo wa Jimbo. Mfano ni barabara ya Wampembe, Ninde, Kala na Mpasa. Zile ndiyo mwambao mwa Ziwa Tanganyika ambazo wale watu wamejikarantini kiuchumi. Tunaongea masuala ya kujikarantini, lakini kwenye Jimbo langu baadhi ya kata kama nne zimejikarantini, masika hakuendeki, labda utumie pikipiki; kwingine pikipiki haifiki inabidi utembee kwa mguu.

Mheshimiwa Spika, nadhani Mheshimiwa Jafo anapafahamu Wampembe. Naomba sana hizi barabara za Ninde, Kala na Wampembe ziingizwe TANROADS, hakuna namna, TARURA wamezidiwa, naungana na mama yangu Mheshimiwa Malecela. TARURA wamezidiwa, tuwapunguzie mzigo; baadhi ya barabara ziingie TANROADS na nyingine zibaki TARURA. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia katika mikoa inayozalisha ni pamoja na Rukwa; na katika Rukwa, Jimbo la Nkasi Kusini. Tukija upande wa pembejeo ni gharama mno kwa mkuma mdogo (peasant). Kwa nini isifike mahali kupata maeneo vijengwe hata viwanda vya mbolea? Wizara ikae, i-sort maeneo, kuwe na zone za kujenga viwanda hasa mikoa ile inayozalisha sana mazao ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Wizara ya Maji, katika Jimbo langu kuna watu bado wanaishi maisha ya ujima. Kipindi cha ujima tulisoma kwenye historia, lakini katika Jimbo langu watu wapo wana-depend on nature. Naomba Wizara hii; nilipita na watendaji wengi ambapo najua ni kilio cha nchi nzima; Wizara ya Maji inabidi ikae pembeni ifanye kama special operation, kwa sababu kilio cha wafanyakazi kule ni wachache, wataalam wa maji hakuna. Ingefanywa tathmini angalau hata robo kwenye baadhi ya miradi, Mheshimiwa Rais anahangaika anatuma fedha na fedha zipo nyingi sana lakini watendaji hakuna. Kuna mradi kama wa Wampembe, Mradi wa Kala, Mpasa na Mradi wa Chala, maeneo yote hayo fedha zipo ila wataalam wako wachache, wanazidiwa. Kwa hiyo, naomba Wizara ya Maji ikae chini iwe na special operation upande wa maji katika majimbo yetu, ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda sana kumshukuru Mungu, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Rais, sisi sote humu Mzee amesema alikuwa ana hofu sijui ni successor au nini, sisi ndiyo walinzi wa nchi hii. Maono ya Mheshimiwa Rais, ametukabidhi sisi Wabunge ambao ndiyo wanasiasa, ndiyo wa kusimamia kile kilichoanzishwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli. Ahsante sana. (Makofi)