Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia katika hoja hii muhimu ya Wizara ya TAMISEMI Ofisi ya Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwanza kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujaalia uzima na afya tumeweza kuendelea kushiriki kujadili hoja zetu muhimu katika Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza Rais wetu, Jemedari wetu tingatinga, burudoza namba moja yetu si mwingine tena bali ni namba moja yetu Dkt John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii pia kumpongeza Waziri Mkuu niwapongeze Mawaziri wote, niwapongeze Naibu Mawaziri wote, niwapongeze Makatibu Wakuu wote, niipongeze Serikali yote kwa ujumla kwa kazi kubwa na nzuri walizofanya ndani ya kipindi cha miaka minne kazi zenye weledi kazi zinazoonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuzisoma kazi zilizofanywa na Serikali yetu sikivu Serikali ya Chama cha Mapinduzi ndani ya miaka minne imeweza kuleta elimu bure bila malipo kuanzia shule ya msingi na sekondari watoto wanasoma bure na ndiyo maana watoto wengi wameweza kujitokeza kwenda shule kwa sababu kabla ya hapo watoto walikuwa wanabaki nyumbani wazazi walikuwa wanashindwa kulipa hiyo elfu 10, elfu 40, elfu 50. Lakini baada ya kuleta elimu bila ada watoto wamekuwa ni wengi wamejitokeza kwa wingi, naipongeza sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya miaka minne na ushee imeweza kuboresha upatikanaji wa madawa mahospitalini, ndani ya kipindi cha miaka minne imeweza kukarabati na kujenga vituo vya afya takriban 433 si kazi ndogo hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imefanya kazi kubwa sana kwa watanzania imeweza kuleta mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu imeweza kununua ndege takriban nane na zingine zinaendelea kuja tuseme nini mbele ya macho ya Mungu? Mungu atupe nini atupe kidonda bado watu wanasema hawaoni kilichofanyika bado watu wanasema hiyo elimu bure haina maana kwa kweli Mwenyezi Mungu anawaona. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi kwa kazi kubwa lakini nikupongeze wewe pamoja na Mheshimiwa Spika kwa kazi kubwa ya kuliendesha Bunge hili kwa utulivu mpaka tunaenda kumaliza kipindi chetu cha miaka mitano nakupongezeni sana wewe pamoja na Spika wetu wa Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizi ninaenda sasa kwenye hoja zangu za msingi nianze na TARURA. TARURA imefanya kazi nzuri sana TARURA imefanya kazi nzuri sana lakini kutokana na changamoto ya mvua nyingi za mwaka huu barabara nyingi zimeweza kuharibika na madaraja mengi yameweza kuharibika kwa hiyo, naiomba Serikali iweze kuongeza zile 30% iweze kuwa 50 na TANROADS pia iweze kupewa fungu la kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bado barabara nataka niiongelee barabara ya kutoka Tunduma kwenda Sumbawanga. Barabara ile ina mabonde ni barabara nzuri sana lakini ina bumps nyingi sana kiasi kwamba wanaume wanaoendesha magari kwenye barabara ile na wanawake viuno vyao sasa hivi wanaumwa. Barabara ile imezidi sana zile bumps ni kilo mita zaidi 280, 300 lakini ma-bumps yamekuwa mengi matuta ni makubwa yamekuwa karibu karibu kiasi kwamba mabasi yanayokwenda kule yanaharibika yanayobeba abiria yanaharibika hata magari madogo madogo na yenyewe kila wakati yanaharibika kutokana na matuta makubwa yaliyokithiri kwenye ile barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri alipokuja Mheshimiwa Rais kwenye Mkoa wa Rukwa alitamka mbele ya mkutano wa hadhara kwamba matuta yatapunguzwa sasa ninaomba atakapokuja kuhitimisha atuambie ni lini matuta hayo yatapunguzwa hata kama siyo kuyamaliza yote basi yapunguzwe yanaharibu sana magari lakini binadamu pia wanarushwa sana wanaposafiri kwenye ile barabara wanaumwa ninavyosema hivyo ukiwapima wanaume wanaosafiri safiri kwenda kule viuno vyao haviko salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee tena suala la ukubwa wa Jimbo ukumbwa wa Majimbo. Mkoa wa Rukwa umebarikiwa sana kuwa na Majimbo makubwa Jimbo la Kwela maarufu kama Sumbawanga DC ni kubwa sana tunamshukuru Mheshimiwa Rais alipokuja alirudisha halmashauri ikapelekwa kwenye mji mdogo wa Laela tunamshukuru. Lakini bado kuna changamoto kubwa lile Jimbo limegawanyika katika sehemu mbili Ufipa wa Juu na Ufipa wa Chini, lile Jimbo lina kata 28 sasa Ufipa wa chini huku sasa hivi madaraja yamebomoka na Mwenyezi Mungu aliligawa automatically lile Jimbo aliligawa katika sehemu mbili upande wa chini, ziwani kuna kata 14 na upande wa juu kuna kata 13 kwa hiyo, wananchi wanapata tabu sana kufuata huduma wanapata shida kufuata huduma huku juu ambako halmashauri imepelekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tulikuwa tunaomba na kule wapelekewe mamlaka ili waweze kujitegemea kwasababu kipindi hiki wakati wa mvua hakuna mawasiliano kabisa madaraja yamebomoka hakuna kabisa watu wanapata tabu kwenda kufuata huduma ufipa wa juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba sana suala hili ni kilio kikubwa sana cha wananchi wa Jimbo la Kwela, wanaomba mamlaka igawanywe aidha Jimbo ligawanyike katika sehemu mbili na wenyewe huku chini wapate mamlaka na huku juu iendelee mamlaka kama Mheshimiwa Rais alivyotupelekea halmashauri yetu pale mji mdogo wa Laela.

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa kengele ya pili imeshagonga.

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi)